Tumain
JF-Expert Member
- Jun 28, 2009
- 3,154
- 70
MWONGOZO wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi unamtaka kila mwalimu kufundisha, kwa wiki vipindi, visivyozidi 28 na visivyopungua 24. Vipindi kwenye ratiba hujaa vizuri bila mgongano na wanafunzi hufaidi uwepo wa walimu.
Mwalimu yeyote anayekuwa na vipindi zaidi ya 28 huwa na mzigo mkubwa na ili kusiwe na mgongano na vipindi vya walimu wengine atalazimika kuwarundika wanafunzi wa madarasa mawili au zaidi katika darasa moja. Pia mwalimu anayekuwa na vipindi chini ya 24 hufikiriwa kuwa hatumiki ipasavyo.
Mwongozo huo unaweza kuwa unafanya kazi katika shule mbalimbali za msingi na sekondari lakini si katika shule ya msingi ya Saninga iliyoko kisiwa cha Saninga wilaya ya Rufiji mkoa wa Pwani ambako Omary Hamisi anafundisha.
Hamisi ndiye mwalimu pekee aliyeko shuleni hapo kwa hiyo anapaswa kulitendea haki kila darasaâkufundisha, kutoa kazi za kufanya nyumbani, kutoa majaribio, kusahihisha na kusimamisha shughuli nyingine kama usafi, michezo na shughuli nyingine za kujitegemea. Mwalimu Hamisi hakupenda kubaki pekee yake katika shule hiyo bali amejikuta akikimbiwa na walimu wengine waliopangwa kufundisha. Mazingira magumu ya kufanyia kazi yalioko katika eneo hilo la delta ndiyo chanzo hasa na ili aonekane anawatendea haki wanafunzi wote imemlazimu kufundisha madarasa yote peke yake.
"Nimekuwa katika wakati mgumu wa kufundisha hasa kipindi cha kwenda kwenye mishahara, kipindi cha kilimo na ninapougua kwani nalazimika kufunga shule kwa kipindi hicho," anasema Mwalimu Hamisi. Mwalimu Hamisi hawalaumu walimu wanaokimbia shule hiyo ila mazingira. "Mazingira ya walimu katika visiwa hivi hayamhamasishi mwalimu kufundisha labda serikali ione haja sasa ya kuongeza pesa za mishahara na marupurupu mengine kwa walimu wanaoletwa katika visiwa hivi," anaeleza.
Mwalimu huyo, ambaye anafundisha kuanzia darasa la kwanza hadi la saba, anasema, "Asikudanganye mtu, mazingira ya kazi ni magumu sana, ukweli nimeelemewa na mzigo wa vipindi kuanzia darasa la kwanza hadi la saba bila ya kupata msaada wowote hata kutoka katika shule jirani,"anasimulia.
Ni dhahiri pendekezo lake la kupata walimu wa msaada kutoka shule za jirani ni gumu pia kwani shule nyingine za jirani yaani visiwa vingine nako hali ni ngumu, kuna kilio kama chake.
Kwa mfano, shule za Ruma na Kiechuru zina walimu wawili wawili, Kiongoroni, Msala, Twasalie, Maparoni na Mbuchi zina walimu watatu watatu na zinazoonekana kuwa na nafuu ni Kiasi, Saalale, Nyamisati na Mchinga zenye walimu wane kila moja, Pombwe, Jaja na Kiomboni zenye walimu watano watano na yenye utajiri wa walimu ni Mfisini ambako wako sita. Lakini hakuna anayependa kwenda Saninga.
Baadhi ya walimu wanaopangwa kufundisha shule hiyo huripoti, lakini baada ya kujionea mazingira huondoka na wengine huamua kutoripoti kabisa pale anapoambiwa kituo chake cha kazi ni katika kisiwa hicho.
Halmashauri ya wilaya ya Rufiji, kwa ushirikiano na wananchi, Mwalimu Hamisi anasema imejitahidi kuboresha majengo ya shule na nyumba za walimu, lakini kinachowakimbiza ni mazingira iliko shule.
"Walimu tunaishii kwa shida sana. Nikiumwa au kupata dharura yoyote basi inabidi wanafunzi wabaki peke yao na shule inafungwa mpaka nitakaporudi," anasema mwalimu huyo huku aliyekuwa anajiandaa kwenda likizo nyumbani kwao Ikwiriri.
"Afadhali sana sasa nimetulia, lakini ungekuja hapa kati ya Januari 2009 na Septemba 2009, ungenionea huruma jinsi nilivyokuwa napata shida ya kuwafundisha watoto hawa.
Nikifundisha darasa hili wengine wanalazimika kubaki peke yao hasa madarasa makubwa," anaeleza Hamisi aliyehojiwa mwishoni mwa 2009. Wanaokimbia mazingira katika visiwa hivyo si walimu pekee bali hata watumishi wengine. Ukosefu wa huduma za usafiri, miundombinu mibovu, ugumu wa kupata mishahara, bidhaa na huduma nyingine kama za afya. "Kila kitu ukiwa huku ni shida, hata sehemu ya kununua vitu muhimu ni shida, bidhaa zinapatikana kwa gharama kubwa hivyo inabidi tugharamie kwa kukodi mtumbwi au boti.
"
Nasisitiza kwamba mazingira haya hayamhamasishi mwalimu yeyote awe wa kike au wa kiume kufundisha katika mazingira haya isipokuwa ni kwa yule mwenye roho ngumu kama mimi ndiye naweza kuishi katika mazingira magumu kama haya.
"Ndiyo maana naishauri serikali iangalie namna ya kuwapa motisha walimu wanaofundisha katika visiwa hivi na kuweka kipindi maalumu cha kukaa ili kumfanya mwalimu awe na moyo wa kufundisha.
"Serikali iangalie uwezekano wa kuongeza marupurupu kwa walimu wanaoishi kando kando ya miji na wale wanaofundisha katika mazingira magumu kama sisi kutuongezea fungu la pesa ili kujikimu na hali ngumu iliyoko katika visiwa."
Kwa mujibu wa mwalimu Hamisi, baadhi ya walimu huamua kugoma kuripoti kutokana na taarifa kwamba walimu wanaopangwa kufanya kazi visiwani humo husahauliwa kabisa hivyo hukaa bila kuhamishwa kwa muda mrefu.
Anasema mpango huo ni tatizo mojawapo kwani walimu katika maeneo haya wamekuwa wakisahaulika kabisa kiasi cha kukata tamaa kwani kama wapo wawwili wataendelea kuwa hivyo kwa muda mrefu na kama yuko mmoja basi ataendelea kukaa hivyo hivyo. Tatizo jingine analiliona Mwalimu Hamisi ni ugumu wa kupata maji safi kwa kuwa visima vilivyochimwa ni vifupi sana. "Ukitaka maji yaliyo salama ni lazima ununue dumu moja kwa Sh 700 hadi Sh1,000 kutoka katika kisiwa kingine kilicho mbali. Maji huletwa kwa mitumbwi ambayo wakati mwingine si salama,ââ anasema.
Alisema hata huduma ya afya bado ni tatizo kwa kuwa hospitali iko mbali sana na kisiwa hicho na upatikanaji wa dawa ni mgumu pia na hivyo humlazimu kutembea umbali wa siku nzima kufuata huduma ya matibabu.
Mwamko
Uhaba wa walimu unasababisha wanafunzi wengi kutokuwa na mwamko wa elimu. Baadhi huamua kuacha masomo na kujishughulisha na shughuli kama za uvuvi na kilimo. Wakati wa msimu wa kilimo baadhi ya wanafunzi huandamana na wazazi wao kwenda mashambani na wakati wa mavuno pia huenda kuwasaidia wazazi wao kuvuna. Mahudhurio ya wanafunzi katika misimu hiyo huwa madogo sana na ya kukatisha tamaa.
"Hali huwa mbaya zaidi inapofikia wakati wa kilimo kwa sababu wazazi huondoka na watoto hao na kwenda kwenye kilimo kwa takribani miezi sita na bado mwalimu ukienda kufuata mshahara, lazima ufunge shule hadi urudi ndipo ufungue shule. Pengine hutumia hata wiki mbili."
Mwalimu yeyote anayekuwa na vipindi zaidi ya 28 huwa na mzigo mkubwa na ili kusiwe na mgongano na vipindi vya walimu wengine atalazimika kuwarundika wanafunzi wa madarasa mawili au zaidi katika darasa moja. Pia mwalimu anayekuwa na vipindi chini ya 24 hufikiriwa kuwa hatumiki ipasavyo.
Mwongozo huo unaweza kuwa unafanya kazi katika shule mbalimbali za msingi na sekondari lakini si katika shule ya msingi ya Saninga iliyoko kisiwa cha Saninga wilaya ya Rufiji mkoa wa Pwani ambako Omary Hamisi anafundisha.
Hamisi ndiye mwalimu pekee aliyeko shuleni hapo kwa hiyo anapaswa kulitendea haki kila darasaâkufundisha, kutoa kazi za kufanya nyumbani, kutoa majaribio, kusahihisha na kusimamisha shughuli nyingine kama usafi, michezo na shughuli nyingine za kujitegemea. Mwalimu Hamisi hakupenda kubaki pekee yake katika shule hiyo bali amejikuta akikimbiwa na walimu wengine waliopangwa kufundisha. Mazingira magumu ya kufanyia kazi yalioko katika eneo hilo la delta ndiyo chanzo hasa na ili aonekane anawatendea haki wanafunzi wote imemlazimu kufundisha madarasa yote peke yake.
"Nimekuwa katika wakati mgumu wa kufundisha hasa kipindi cha kwenda kwenye mishahara, kipindi cha kilimo na ninapougua kwani nalazimika kufunga shule kwa kipindi hicho," anasema Mwalimu Hamisi. Mwalimu Hamisi hawalaumu walimu wanaokimbia shule hiyo ila mazingira. "Mazingira ya walimu katika visiwa hivi hayamhamasishi mwalimu kufundisha labda serikali ione haja sasa ya kuongeza pesa za mishahara na marupurupu mengine kwa walimu wanaoletwa katika visiwa hivi," anaeleza.
Mwalimu huyo, ambaye anafundisha kuanzia darasa la kwanza hadi la saba, anasema, "Asikudanganye mtu, mazingira ya kazi ni magumu sana, ukweli nimeelemewa na mzigo wa vipindi kuanzia darasa la kwanza hadi la saba bila ya kupata msaada wowote hata kutoka katika shule jirani,"anasimulia.
Ni dhahiri pendekezo lake la kupata walimu wa msaada kutoka shule za jirani ni gumu pia kwani shule nyingine za jirani yaani visiwa vingine nako hali ni ngumu, kuna kilio kama chake.
Kwa mfano, shule za Ruma na Kiechuru zina walimu wawili wawili, Kiongoroni, Msala, Twasalie, Maparoni na Mbuchi zina walimu watatu watatu na zinazoonekana kuwa na nafuu ni Kiasi, Saalale, Nyamisati na Mchinga zenye walimu wane kila moja, Pombwe, Jaja na Kiomboni zenye walimu watano watano na yenye utajiri wa walimu ni Mfisini ambako wako sita. Lakini hakuna anayependa kwenda Saninga.
Baadhi ya walimu wanaopangwa kufundisha shule hiyo huripoti, lakini baada ya kujionea mazingira huondoka na wengine huamua kutoripoti kabisa pale anapoambiwa kituo chake cha kazi ni katika kisiwa hicho.
Halmashauri ya wilaya ya Rufiji, kwa ushirikiano na wananchi, Mwalimu Hamisi anasema imejitahidi kuboresha majengo ya shule na nyumba za walimu, lakini kinachowakimbiza ni mazingira iliko shule.
"Walimu tunaishii kwa shida sana. Nikiumwa au kupata dharura yoyote basi inabidi wanafunzi wabaki peke yao na shule inafungwa mpaka nitakaporudi," anasema mwalimu huyo huku aliyekuwa anajiandaa kwenda likizo nyumbani kwao Ikwiriri.
"Afadhali sana sasa nimetulia, lakini ungekuja hapa kati ya Januari 2009 na Septemba 2009, ungenionea huruma jinsi nilivyokuwa napata shida ya kuwafundisha watoto hawa.
Nikifundisha darasa hili wengine wanalazimika kubaki peke yao hasa madarasa makubwa," anaeleza Hamisi aliyehojiwa mwishoni mwa 2009. Wanaokimbia mazingira katika visiwa hivyo si walimu pekee bali hata watumishi wengine. Ukosefu wa huduma za usafiri, miundombinu mibovu, ugumu wa kupata mishahara, bidhaa na huduma nyingine kama za afya. "Kila kitu ukiwa huku ni shida, hata sehemu ya kununua vitu muhimu ni shida, bidhaa zinapatikana kwa gharama kubwa hivyo inabidi tugharamie kwa kukodi mtumbwi au boti.
"
Nasisitiza kwamba mazingira haya hayamhamasishi mwalimu yeyote awe wa kike au wa kiume kufundisha katika mazingira haya isipokuwa ni kwa yule mwenye roho ngumu kama mimi ndiye naweza kuishi katika mazingira magumu kama haya.
"Ndiyo maana naishauri serikali iangalie namna ya kuwapa motisha walimu wanaofundisha katika visiwa hivi na kuweka kipindi maalumu cha kukaa ili kumfanya mwalimu awe na moyo wa kufundisha.
"Serikali iangalie uwezekano wa kuongeza marupurupu kwa walimu wanaoishi kando kando ya miji na wale wanaofundisha katika mazingira magumu kama sisi kutuongezea fungu la pesa ili kujikimu na hali ngumu iliyoko katika visiwa."
Kwa mujibu wa mwalimu Hamisi, baadhi ya walimu huamua kugoma kuripoti kutokana na taarifa kwamba walimu wanaopangwa kufanya kazi visiwani humo husahauliwa kabisa hivyo hukaa bila kuhamishwa kwa muda mrefu.
Anasema mpango huo ni tatizo mojawapo kwani walimu katika maeneo haya wamekuwa wakisahaulika kabisa kiasi cha kukata tamaa kwani kama wapo wawwili wataendelea kuwa hivyo kwa muda mrefu na kama yuko mmoja basi ataendelea kukaa hivyo hivyo. Tatizo jingine analiliona Mwalimu Hamisi ni ugumu wa kupata maji safi kwa kuwa visima vilivyochimwa ni vifupi sana. "Ukitaka maji yaliyo salama ni lazima ununue dumu moja kwa Sh 700 hadi Sh1,000 kutoka katika kisiwa kingine kilicho mbali. Maji huletwa kwa mitumbwi ambayo wakati mwingine si salama,ââ anasema.
Alisema hata huduma ya afya bado ni tatizo kwa kuwa hospitali iko mbali sana na kisiwa hicho na upatikanaji wa dawa ni mgumu pia na hivyo humlazimu kutembea umbali wa siku nzima kufuata huduma ya matibabu.
Mwamko
Uhaba wa walimu unasababisha wanafunzi wengi kutokuwa na mwamko wa elimu. Baadhi huamua kuacha masomo na kujishughulisha na shughuli kama za uvuvi na kilimo. Wakati wa msimu wa kilimo baadhi ya wanafunzi huandamana na wazazi wao kwenda mashambani na wakati wa mavuno pia huenda kuwasaidia wazazi wao kuvuna. Mahudhurio ya wanafunzi katika misimu hiyo huwa madogo sana na ya kukatisha tamaa.
"Hali huwa mbaya zaidi inapofikia wakati wa kilimo kwa sababu wazazi huondoka na watoto hao na kwenda kwenye kilimo kwa takribani miezi sita na bado mwalimu ukienda kufuata mshahara, lazima ufunge shule hadi urudi ndipo ufungue shule. Pengine hutumia hata wiki mbili."