Mwalimu alisema....

MwanaFalsafa1

JF-Expert Member
Feb 26, 2008
5,565
836
Katika siku ya wafanyakazi May 1995, rais mstaafu na mwenyekiti mstaafu wa CCM Mwl. Julius K. Nyerere ndiyo alikuwa mgeni rasmi. Alitoa hotuba ndefu kidogo iliyo jaa maono na muongozo.

Lakini mimi kuna sehemu moja tu ya hiyo hotuba ndiyo ilinikuna kupita zote. Mwl. alisema kwamba wakati yeye anaingia madarakani na wenzake walikua hawana model ya kufuata. Kila kitu kili takiwa kujengwa kuanzia juu kwenda chini yani "trial & error".

Akaendelea kusema kwamba anakubali serikali yake ilikuwa na mabaya yake lakini pia ilikuwa na mazuri yake. Akasema serikali ya Mwinyi ilipaswa kuchukua yale mazuri na kuyaacha yale mabaya. Hali kadhalika akasema nao serikali ya Mkapa inatakiwa kuchukua yale mazuri ya kipindi cha Mwinyi na kuyaacha mabaya.

Haya maneno yalinigusa sana kwa sababu ni maneno rahisi lakini magumu kuelewa. Leo hii inashangaza serikali yetu inafanya kinyume na kuchukua mabaya yote ya serikali zilizopita na kuyaacha mazuri. Inasikitisha kwamba baada ya miaka hamsini ya uhuru tunarudi nyuma badala ya kusonga mbele.

Je ni mazuri yapi ya serikali za Nyerere, Mwinyi na Mkapa yalitakiwa kuendelezwa?


[video=youtube;iokLuPXv33]http://www.youtube.com/watch?v=iokLuPXv33[/video]
 
huyu jamaa alikuwa kichwa sana, namheshimu.

Very true mkuu. Ninachompendea ni kwamba jamaa alikua na uwezo wa kuona mbali si hawa wa leo wanaoona urefu wa pua tu. Japo alikuwa na mapungufu yake tungechukuwa yale mazuri yake tungekuwa mbali. He was a political genius and he is my political idol.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Mazuri yao lao kuwanufaisha machangu na wapenda vya bure kwa kuwaweka chakula cha mkuu.....
 
Mwanafalsafa1,

Kwa sababu leo ni Easter sitakuwa na muda mwingi wa kukaa kwenye mtandao. Lakini umeuliza tungechukua mazuri gani, hapa nitakupa mfano mmoja tu. Mwalimu alitaka Tanzania tuwe na viwanda vyetu, na alituwekea misingi ya viwanda hivyo. Licha ya kwamba viliendeshwa hohe-hahe (makosa) misingi ya kuwa na viwanda vyetu haikuwa kosa. Sasa wakaja wenye akili zaidi ( Mwinyi na Mkapa) na badala ya kuangalia ni wapi tulifanya makosa, tuyarekenishe, ili viwanda viendelee kuwa vyetu, wakaamua kubinafsisha, au kugeninasisha. Kuna wakati nilimwuuliza Mkapa kwa nini hawasaidii Watanzania wawekeze badala ya wageni, akanijibu kwa jeuri, "Watanzania ndio walioua viwanda. Afadhali tuwape Makaburu waviendeshe." Sasa tunavuna matunda ya mtazamo huo.

Ni hilo tu moja kwa leo. Happy Easter.
 
Tanzania tumshukuri Mungu kwa kutujalia kiongozi huyu, Laiti kama tutayachukua mazuri yake aliyosema na kutenda na tukayafanyia kazi, Tanzania tungekua mbali sana, Tutamkumbuka sana huyu baba!
 
Very true mkuu. Ninacho mpendea ni kwamba jamaa alikua na uwezo wa kuona mbali si hawa wa leo wanao ona urefu wa pua tu. Japo ali kuwa na mapungufu yake tunge chukua yale mazuri yake tunge kuwa mbali. He was a political genius and he is my political idol.

Kabisa Mkuu unaweza kusikiliza hotuba ya Mwalimu ya miaka 20 au 25 iliyopita lakini hotuba hiyo ingeweza kabisa kutolewa jana au juzi kutokana na mazingira tuliyonayo nchini mwetu kwa sasa
 
Mwanafalsafa1,

Kwa sababu leo ni Easter sitakuwa na muda mwingi wa kukaa kwenye mtandao. Lakini umeuliza tungechukua mazuri gani, hapa nitakupa mfano mmoja tu. Mwalimu alitaka Tanzania tuwe na viwanda vyetu, na alituwekea misingi ya viwanda hivyo. Licha ya kwamba viliendeshwa hohe-hahe (makosa) misingi ya kuwa na viwanda vyetu haikuwa kosa. Sasa wakaja wenye akili zaidi ( Mwinyi na Mkapa) na badala ya kuangalia ni wapi tulifanya makosa, tuyarekenishe, ili viwanda viendelee kuwa vyetu, wakaamua kubinafsisha, au kugeninasisha. Kuna wakati nilimwuuliza Mkapa kwa nini hawasaidii Watanzania wawekeze badala ya wageni, akanijibu kwa jeuri, "Watanzania ndio walioua viwanda. Afadhali tuwape Makaburu waviendeshe." Sasa tunavuna matunda ya mtazamo huo.

Ni hilo tu moja kwa leo. Happy Easter.

Mkuu Jasusi asante kwa kuchukua muda wako kuchngia mada. Ni ukweli usiofichika kwamba Mkapa alikuwa ana jeuri na kiburi sana. Kama viongozi wengine wa Afrika alikuwa na mentality ya kwamba uongozi ni milele. Leo hii yuko wapi? Anaishia kuzomewa na msafara wake kutupiwa mawe. He will die with no respect.

Wengi wanamsifia Mkapa kwa kupunguza deni ya taifa. Watu hao ni wale wasiojua kwamba madeni yale tulisamehewa na IMF na WB kwa conditions za kubadili sera zetu ili kuruhusu mfumo utakaoruhusu wawekezaji wa Magharibi waingie kwa urahisi zaidi. Matokeo yake ni sera za "ubinafsishaji" na "utandawazi". Hivi Watanzania hawajiulizi kwanini rais wa WB ni lazima awe Mmarekani? Na hii ni sheria kabisa kwamba moja wapo ya vigezo vya kuwa rais wa WB ni lazima uwe raia wa Marekani (anyone can verify this easily).

Kiukweli kabisa Mkapa failed the average Tanzanians. Sera zake zilinufaisha wageni na viongozi wachache waliokuwa wanapewa 10% kupitisha hizi sera.
 
Kuna wakati mzee huyu alizungumzia katiba, alihoji kwanini ccm wanakaa pekeyao kuandaa katiba mpya, vile vile alizungumzia suala la mgombea binafsi......mazuri ni mengi sana
 
Ukitaka uamini kuwa jamaa alikuwa kichwa na kiona mbali, ebu sikiliza hotuba zake za miaka zaidi ya 20 iliyopita. Utashangaa utakapoona kuwa hadi sasa maneno yake ni VALID. Marais waliofuata baada ya hapo sijui kama walikuwa wanaona mbali. Lakini yote katika yote, huyu tuliye nae sasa ndiyo basi kabisa. Anaona pungufu ya urefu wa pua yake.
 
Huyu mzee mnamtukuza bure lakini ametawala nchi kibabe na kidikteta sana.

Baada ya kuona mambo yanamkalia vibaya na Watanzania wanaanza kuamka ndio akaanza kuzungumza lugha hizi za kujipendekeza kwa wananchi na kuwafanya waliokuja baada yake wabaya.

Chukua huo mfano wa Katiba unayosema Mkuu. Si Nyerere huyu huyu alieteua wajumbe wa CCM na Zanzibar kuandaa Katiba ya Chama chao na baadae akatumia Kamati hiio hio ya Chama chake kuunda Katiba ya Tanzania?

Si Nyerere huyu huyu aliekiuka Mkataba wa Muungano na kuligeuza Bunge letu la Kawaida na kulifanya kuwa Bunge la Katiba na kuipitisha?

Si Nyerere huyu huyu alievunja Mkataba wa Muungano na kiongezea madaraka SMT kwa kuifisidi Zanzibar?

Huyu Nyerere tutamkumbuka daima kwa chuki zake dhidi ya Zanzibar mpaka kwa kushindwa kujizuia akasema,

"If i could tow that island out into the middle of Indian Ocean, i could do it" - JK Nyerere

Huyu Nyerere ndio tutamkumbuka sana kwa mabaya yake na hakuna jema alotufanyia zaidi ya kutusaidia kumuondoa Mkoloni lakini kumbe kwa yeye kuifanya Zanzibar Koloni la Tanganyika.

Huyu ni mtu mbaya sana na hastahiki kusifiwa ila na wakoloni wenzake.
 
Huyu mzee mnamtukuza bure lakini ametawala nchi kibabe na kidikteta sana.

Baada ya kuona mambo yanamkalia vibaya na Watanzania wanaanza kuamka ndio akaanza kuzungumza lugha hizi za kujipendekeza kwa wananchi na kuwafanya waliokuja baada yake wabaya.

Chukua huo mfano wa Katiba unayosema Mkuu. Si Nyerere huyu huyu alieteua wajumbe wa CCM na Zanzibar kuandaa Katiba ya Chama chao na baadae akatumia Kamati hiio hio ya Chama chake kuunda Katiba ya Tanzania?

Si Nyerere huyu huyu aliekiuka Mkataba wa Muungano na kuligeuza Bunge letu la Kawaida na kulifanya kuwa Bunge la Katiba na kuipitisha?

Si Nyerere huyu huyu alievunja Mkataba wa Muungano na kiongezea madaraka SMT kwa kuifisidi Zanzibar?

Huyu Nyerere tutamkumbuka daima kwa chuki zake dhidi ya Zanzibar mpaka kwa kushindwa kujizuia akasema,

"If i could tow that island out into the middle of Indian Ocean, i could do it" - JK Nyerere

Huyu Nyerere ndio tutamkumbuka sana kwa mabaya yake na hakuna jema alotufanyia zaidi ya kutusaidia kumuondoa Mkoloni lakini kumbe kwa yeye kuifanya Zanzibar Koloni la Tanganyika.

Huyu ni mtu mbaya sana na hastahiki kusifiwa ila na wakoloni wenzake.

Hatutaki humu JF vijitu vyenye visa binafsi. Hata uwe so -ve, Nyerere will remain the Father of our Nation. Alikuwa na mapenzi ya dhati kwa nchi yake na alikuwa adui mkubwa kwa vijitu (nahisi na wewe ni miongoni mwao) vilivyotaka kutanguliza maslahi binafsi badala ya taifa. Misingi ya utaifa aliyoijenga ndiyo inayoifanya Tanzania angalau isurvive mpaka sasa katikati ya maadui wa ndani (kama wewe) na wa nje.
 
Hatutaki humu JF vijitu vyenye visa binafsi. Hata uwe so -ve, Nyerere will remain the Father of our Nation. Alikuwa na mapenzi ya dhati kwa nchi yake na alikuwa adui mkubwa kwa vijitu (nahisi na wewe ni miongoni mwao) vilivyotaka kutanguliza maslahi binafsi badala ya taifa. Misingi ya utaifa aliyoijenga ndiyo inayoifanya Tanzania angalau isurvive mpaka sasa katikati ya maadui wa ndani (kama wewe) na wa nje.

Taifa lipi are you reffering to Dume? Kijitu nadhani ni matusi au tuseme ni dharau na nikimuona mtu badala ya kujadili issue anajadili mtu, huanza kumdharau sana tu.

JF ni ukumbi huru wa mtu kutolea mawazo yake lakini wewe baada ya kujadili hoja, unanijadili mmi.

Wewe unamuona Nyerere hivyo, usinilazimishe na mimi kumuona hivyo.

Hapa si ubinafsi hata kidogo, ni hoja kwa hoja.
 
Taifa lipi are you reffering to Dume? Kijitu nadhani ni matusi au tuseme ni dharau na nikimuona mtu badala ya kujadili issue anajadili mtu, huanza kumdharau sana tu.

JF ni ukumbi huru wa mtu kutolea mawazo yake lakini wewe baada ya kujadili hoja, unanijadili mmi.

Wewe unamuona Nyerere hivyo, usinilazimishe na mimi kumuona hivyo.

Hapa si ubinafsi hata kidogo, ni hoja kwa hoja.

Wala huna hoja mkuu ila ni vurugu tu na chuki binafsi tena za kukalili.
 
Mkuu Makaimati,

Nyerere alikuwa mtu tofauti kwa kila mtu. Hakika kama binadamu huwezi pendwa na kila mtu. Na hakika kama kiongozi huwezi boresha maisha ya kila mtu. Wale waliohisi kusahauliwa. Nadhani kiongozi yoyote mwenye hulka ya kupenda kupendwa na kila mtu sana ata fedheheka na uongozi utamshinda kwa kujaribu kumridhisha kila mtu.

Ila tofauti kubwa ni kwamba kuna wanao angalia nchi na kuona Tanzania katika ujumla wake. Na kuna wale wanao angalia nchi wanaona maeneo, majimbo, dini, ukabila, ukanda, lugha na kadhalika. Hawa ndiyo wanaangalia Nyerere kaifanyia nini ukanda wangu, kaifanyia nini kabila langu na kaifanyia nini dini yangu.

Kwa tunao angalia taifa zima hata kama uongozi wa Nyerere haukunufaisha mikoa yetu binafsi, au makabila yetu binafsi au dini zetu binafsi, tuna tambua mchango wake kwa taifa. Na hakika siwezi kukulazimisha kuona hilo kama tayari mentality yako ni kuangalia tu ni nini kaifanyia Zanzibar. Sina neno na hilo kwa maana natambua kuna tunao jitambulisha kama Watanzania na kuna mnao jitambulisha kama Wazanzibar na hakika kuna wengine pia wanao jitambulisha kama Wakristo na Waislamu.

Hatumtukuzi Nyerere kwa maana yeye mwenyewe alikiri makosa mengi tu. Ila tunamshukuru kwa moyo wake wa dhati, tuna yaenzi na kujaribu kuendeleza yale mazuri na pia tuna jikumbusha mara kwa mara maneno yake ambayo mpaka leo yana mshiko.
 
Mazuri ya Nyerere nipamoja na kuweka misingi ambazo ni tunu kwa Taifa Letu. Tuni hzi zimechakachuliwa!
 
Siasa zake zilibuniwa kulinda mali ya watanzania wote kwa faida ya wote. kwa bahati mbaya siasa za ujamaa zilishindwa kutekelezeka na naamini kama waliomfuatia wangekuwa makini wangebadili mifumo ya siasa zile bila kuamua kugawa mali za nchi kwa matapeli kwa visingizo vya uwekezaji
 
Hatutaki humu JF vijitu vyenye visa binafsi. Hata uwe so -ve, Nyerere will remain the Father of our Nation. Alikuwa na mapenzi ya dhati kwa nchi yake na alikuwa adui mkubwa kwa vijitu (nahisi na wewe ni miongoni mwao) vilivyotaka kutanguliza maslahi binafsi badala ya taifa. Misingi ya utaifa aliyoijenga ndiyo inayoifanya Tanzania angalau isurvive mpaka sasa katikati ya maadui wa ndani (kama wewe) na wa nje.

brain washed...
 
Kabisa Mkuu unaweza kusikiliza hotuba ya Mwalimu ya miaka 20 au 25 iliyopita lakini hotuba hiyo ingeweza kabisa kutolewa jana au juzi kutokana na mazingira tuliyonayo nchini mwetu kwa sasa
Si hivyo tu bali pia hotuba zake zinavutia kusikiliza hata siku nzima kwani hazikuwa za kinafiki kama ilivyo kwa hawa wanaojichubua magamba kwa sasa.
 
Back
Top Bottom