Mtaka Haki
JF-Expert Member
- Oct 1, 2010
- 492
- 149
Mpendwa Dr. Mwakyembe, Umekuwa rafiki wa watanzania wa vyama vyote na wa kila mahali. Ushujaa wako ulitokana na yanayoendelea sasa ambayo kama mashujaa hawatasimama basi mafisadi ( Dowans) watalipwa.
1. Kwa kuwa wewe ndiye uliyefunua mapema uovu uliokuwepo wa Richmond basi tafadhali usinyamaze. Mwenzako Sita ameweka maslahi ya taifa mbele ya cheo chake na kanuni za kawaida.
2. Tafadhali jitokeze useme chochote au tupe tu taarifa tuzitumie ipasavyo.
3. Ukinyamaza kabisa wakati huu Mungu atatokeza mlango na wokovu kwa njia nyingine, lakini wewe hutakuwa salama kuliko watanzania wengine wasio mawaziri. Walakini ni nani ajuae kuwa hukuujilia ufalme ( uongozi) kwa ajili ya wakati kama huu?
4. Usikubali kuvunjwa moyo kuwa unaibu uliopewa ni hongo ya kukufunga kinywa bado inawezekana.
1. Kwa kuwa wewe ndiye uliyefunua mapema uovu uliokuwepo wa Richmond basi tafadhali usinyamaze. Mwenzako Sita ameweka maslahi ya taifa mbele ya cheo chake na kanuni za kawaida.
2. Tafadhali jitokeze useme chochote au tupe tu taarifa tuzitumie ipasavyo.
3. Ukinyamaza kabisa wakati huu Mungu atatokeza mlango na wokovu kwa njia nyingine, lakini wewe hutakuwa salama kuliko watanzania wengine wasio mawaziri. Walakini ni nani ajuae kuwa hukuujilia ufalme ( uongozi) kwa ajili ya wakati kama huu?
4. Usikubali kuvunjwa moyo kuwa unaibu uliopewa ni hongo ya kukufunga kinywa bado inawezekana.