Mwakyembe na Magufuli wizara moja; Je kunani?

Njowepo, nadhani una ugonjwa wa Phobia. Dalili mojawapo ya phobia ni kuogopa kila jambo. Kwani majembe mawili hayawezi kufanya kazi pamoja? Au ulitaka wakae vilaza watupu. ACHA HIZO

Nchimbi na Mwakyembe nani bora!!
 
makandarasi fake wa kichina kazi wanayo, watanyang`anywa vifaa ka ile meli ya uvuvi!!!!!!!!!!!!
 
ccm wameona ili kuwanyamazisha wapigania ufisadi kutoka ccm ni kuwapa uwaziri/naibu tu....na wamefanya hivyo...kwa maana nyingine hutasikia tena mwakyembe au sitta akiwa agaist serikali yake......tumekwisha...............na pia ni njia moja wapo ya kuwatafutia njia ya kutosha kwani hawatakuwa na muda mwingi wa kuwatetea wananchi wao na hivyo baadaye wananchi wataanza kusema hutukusikia wakitutetea kwa hiyo hatuwataki......itakuwa furaha kwa lowasa na rostamu hawa jamaa wasiposikika ktk bunge hili............
 
Bado sijaelewa huu ushabiki wa "uzuri" wa waziri mteule John Pombe Magufuli unatoka wapi. Madudu yake Ardhi na Ujenzi yanarudi tena. Msidanganyike na vile vitakwimu vyake mkafikiri ni mchapakazi. Swali moja, hivi ile hasara ya samaki ilifikia kiasi gani?[/QUOT
magufuli sio kwamba ni mchapa kazi bali ni bingwa wa kughani na kukariri vina kama wakina jay z na eminem au tupac wanavyoweza kumeza nyimbo ndefu bila kukosea alininyima raha sana kwa kuuza nyumba zetu zilizoachwa na mkoloni na mpaka leo hajuti bali anatete aule uamuzi,samaki wake wametia hasara taifa kwa kuwaifadhi kuliko unavyodhani
 
magufuli anakandamizaga wanyonge,
Sikuona samaki alizokamata zilimsaidiaje mvuvi mdogo wa Tz.
Takwimu zake hazina tija.

we ulitaka awaite mmojammoj awagawie?uwe unafikiri kabla ya kuropoka ww.takwimu ni muhimu ktk jambo lolote ili kujua ulikuwa wapi,uo wapi na uelekee wap.sawa?
 
Uteulizi niliopenda ni hii wizara ya ujenzi. sas barabara zitajengwa tena na tutaona na hapa ndipo JK alipoweza kushituka na kukubali kuwa miaka mitano iliyopita barabara zilidorora kabisa na kwa maksi alipata 20%.
Lakini sasa kazi zitafanyika na tutaona mafanikio tena ya Road Fund
 
Frankly speaking,hawa jamaa wanaweza kufanya vizuri. Kuna mtu mmoja aliwashawahi kunidokeza kuwa Mwakyembe ni mtu ambaye huwa hapendi rushwa na alishawahi kukataa rushwa ya pesa nyingi miaka ya nyuma wakati akiwa na wadhifa fulani( sikumbuki vizuri wadhifa huo). Hii ni moja ya wizara muhimu sana nchini.Kwa upande wa Mzee Sam Sitta kupewa Wizara ya East Africa Cooperation hiyo kwake ni demotion(my personal view).

nakubaliana na ww hata mi wamenikera sana hawa jamaa kwa kumfanyia sita uzandiki huo.ila atang'ara tu
 
Bado sijaelewa huu ushabiki wa "uzuri" wa waziri mteule John Pombe Magufuli unatoka wapi. Madudu yake Ardhi na Ujenzi yanarudi tena. Msidanganyike na vile vitakwimu vyake mkafikiri ni mchapakazi. Swali moja, hivi ile hasara ya samaki ilifikia kiasi gani?

Ni watanzania wengi sana wanaamini kuwa Magufuli ni mmoja wa viongozi wachache Taifa limebaki nao wachapakazi kama wewe siyo mmoja wao siyo vibaya ukahifadhi msimamo wako.
 
School Name/Location Course/Degree/Award Start Date End Date Level University of Dar es Salaam B.Sc Ed. (Hons) Chem.&Maths 1985 1988 GRADUATE Universities of Dar es Salaam, TZ &Salford -U.K. MSc. (Chem) 1991 1994 MASTERS DEGREE University of Dar es Salaam. PhD (Chem) 2006 2009 PHD Mkwawa College of Education Diploma in Education (Sc.) Chem., Maths&Edu. 1981 1982 DIPLOMA Mkwawa High School A-Level Education 1979 1981 HIGH SCHOOL Lake Secondary School � Mwanza O-Level Education 1977 1978 SECONDARY Katoke Seminary Biharamulo, Kagera O-Level Education 1975 1977 SECONDARY Chato Primary School Primary Education 1967 1984 PRIMARY
 
Hiyo ya magufuli na mwakyembe imetulia mana wakandarasi walishaaza kuvuna kwenye shamba la bibi kama zao na kutimka zao uchina uko.hapo jk kafanyia maoni ya watanzania walio wengi mana mwakyembe lawyer ,pombe enginia hapo pako powa hakuna mikataba feki.ilaaaaaa mhhhhhhhhhhhhhh kwa sita kupewa east africa amechakachuliwa kisiasaaaaaa baibaiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii sitaaaaaaaaa

magufuli hajawahi kuwa engineeer, ila akiitwa engineer anakaa kimya, tutamkumbuka kwa jinsi alivyokuwa anakula rushwa na jeshi kupitia SUMA JKT. watu Wana msifia sana kwa kuwa hawajui kuna nini nyuma ya pazia
 
Hapo JK amefanya sahihi... wala rushwa na wazembe ndani ya wizara hiyo kuanzia leo waanze kujirekebisha mapema ili barabara bora nyingi zijengwe bila kusahau viwanja vya ndege!
 
Bado sijaelewa huu ushabiki wa "uzuri" wa waziri mteule John Pombe Magufuli unatoka wapi. Madudu yake Ardhi na Ujenzi yanarudi tena. Msidanganyike na vile vitakwimu vyake mkafikiri ni mchapakazi. Swali moja, hivi ile hasara ya samaki ilifikia kiasi gani?
Kazi yake ilikuwa kuwezesha kukamatwe watuhumiwa, period. Yaliyoendelea na yanayoendelea kwenye hiyo kesi usimuhusishe, kuna polisi na mahakama ndio wanaopaswa kuulizwa hizo habari!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom