Mwakyembe kufukuzwa CCM

Msharika

JF-Expert Member
May 15, 2009
947
69
Jamani huyu akifukuzwa CCM atabaki mbunge gani tena, au ndiyo YES men and women watabaki???????? Tafakari

SIKU moja baada ya Spika wa Bunge, Bw. Samuel Sitta kupata tumaini jipya kwa kuungwa mkono huku akihakikishiwa msaada kurudi kwenye nafasi hiyo na mwanasiasa mkongwe nchini, Bw. John Malecela, hali si shwari kwa Mbunge wa Kyela, Dkt. Harrison Mwakyembe.

Vyanzo vyetu vya kuaminika ndani ya CCM vinaeleza kuwa Dkt. Mwakyembe amewekwa pabaya na wabaya wake kisiasa ambao sasa wamehamishia nguvu zao katika vikao vya chama wilayani Kyela kwa lengo la kummaliza kisiasa.

"Wabaya wa Mwakyembe wamehamisha nguvu zao zote jimboni na wilayani kwake Kyela. Ndani ya CCM Kyela kuna mkakati mzito wa kumng'oa Dkt. Mwakyembe si ubunge tu bali hadi uanachama. Vikao vinafanyika, wameapa kwamba kuwepo Mwakyembe ndani ya bunge lijalo ni kikwazo cha urais kwa baadhi ya wanasiasa wanaosaka nafasi hiyo kwa udi na uvumba," kilisema chanzo chetu.

Imeelezwa kwamba kundi linalomshughulikia Dkt. Mwakyembe limesoma alama za nyakati na kubaini kuwa njia pekee ya kummaliza kisiasa ni kitumia vikao vya chini vya chama hususan ngazi ya wilaya.

Hofu kuu ya kundi hilo ni kwamba iwapo Dkt. Mwakyembe atashinda kipindi kijacho ana uwezo mkubwa wa ushawishi na kutumia vifungu kadhaa vya sheria kukwamisha mipango ya urais kwa baadhi ya wanachama wanaosaka nafasi hiyo mwaka 2015.

"Kuna mikakati michafu inafanyika Kyela hata kutumia vyombo vya habari kutoa ujumbe wa 'kummaliza' kabisa kisiasa Dkt. Mwakyembe, lakini uongozi wa juu umekaa kimya,"kilisema chanzo hicho.

Mbinu zingine zinazodaiwa kuandaliwa dhidi ya Dkt. Mwakyembe ni kupewa alama ndogo, kudaiwa kuwa ana kundi linalokigawa chama wilayani na kama atalalamika, vikao hivyo vitatoa mapendekezo ya kumvua uanachama kwa madai ya kukivuruga chama

"Tayari kazi imekamilika kila kata kinachoendelea sasa ni kampeni za matawi, akipona kwenye kura za maoni lazima akwame katika vikao maalum vya ngazi za wilaya na mkoa,lengo ni kumfukuza kabisa ndani ya chama,"kilisema chanzo hicho na kuongeza;

"Taarifa hizi zote zinajulikana ngazi za juu lakini hakuna hatua zinazochukuliwa, sijui kama mbinu hizi zina baraka au mamlaka ya juu inaogopa nini wakati mambo yanaharibika?"alisema Mjumbe mmoja wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC) kwa sharti la kutoandikwa jina gazetini.

Majira lilipomtafuta Dkt. Mwakyembe ili kujua kama ana taarifa juu ya mpango huo na msimamo wake, alikiri kuwa na taarifa hizo huku akikataa kutoa ufafanuzi kwa kile alichodai kwamba wananchi ndio watatoa jibu.

"Ninajua kila kinachoendelea, ninajua akina nani wanahusika, mimi siyo mjinga hata sasa niko huku Kyela, mngetaka kujua kwa undani hayo unayoniuliza ungekuja Kyela,"alisema Dkt. Mwakyembe bila kutoa ufafanuzi wa kina.

Alipoulizwa hatua alizokwishachukua juu ya suala hilo alisema "Nakumbuka niliwahi kusema kwamba taarifa zote nilishatoa sasa ukitaka fuatilia huko mbele, lakini naomba usisahau kitu kimoja, uamuzi wangu wa mwisho utatolewa na wananchi siku ikifika, mafisadi watumie mamilioni au mabilioni, wafanye nini uamuzi wa mwisho utatolewa na wananchi,"alisisitiza.

Majira ilipomtafuta Katibu wa CCM Itikadi na Uenezi Mkoa wa Mbeya Bw. Basiru Madodi, ili kujua ukweli wa suala hilo, alikiri kusikia taarifa hizo mitaani lakini si rasmi.

"Na mimi nimesikia tu hizo taarifa kama ulivyosikia wewe, hivi sasa tunaendelea kufanya uchunguzi ili kujua ukweli maana Jimbo la Mbeya inaonekana kuna makundi tunataka tujiridhishe kwanza kabla ya kusema chochote,"alisema Bw. Madodi.

Alipoulizwa makundi hayo alisema yanatokana na makovu ya Uchaguzi Mkuu mwaka 2005.

Akizungumza na Majira kwa njia ya simu jana, Mwenyekiti wa Kamati ndogo ya Udhibiti ya Kamati ya Usalama na Maadili ya Taifa ya CCM, Bw. Pius Msekwa, alikiri kupokea malalamiko mengi kuhusu njama hizo za kuangushwa wabunge.

Alisema malalamiko hayo yanashughulikiwa na kwamba kabla ya Uchaguzi Mkuu kila kitu kitakuwa hadharani huku akikataa kuzungumzia suala la Dkt. Mwakyembe pekee kwa maelezo kwamba ana malalamiko mengi mezani kwake.

"Hatujapuzia malalamiko ya Waheshimiwa wabunge, ni kweli nimepokea malalamiko mengi sana siwezi kusema ni ya fulani na fulani yapo mengi sana na tunaendelea kuyashughulikia, tayari tumetoa taarifa inayoonesha ratiba ya kushughulikia na tutatoa taarifa baada ya kumaliza kazi,"alisema Bw. Msekwa.


source: Mwakyembe kufukuzwa CCM
 
CCM ya Kikwete haina ubavu huo. Akimnyooshea kidole mtu, vidole vingine vitatu vinamnyooshea yeye mwenyewe.

Bible Quote:
John 8:7
But Jesus bent down and started to write on the ground with his finger. When they kept on questioning him, he straightened up and said to them, "If any one of you is without sin, let him be the first to throw a stone at her."
 
Wanaweza kumfukuza kwani CCM inaendeshwa kwa nguvu za giza. Nia yao wabakie maharamia watupuuuu!
 
Hata wakiumfukuza, lakini kazi kubwa kabisa aliyoifanya ya kutuondolea madarakani yule fisadi No 1 wa Monduli inampa sifa kubwa. Angezidi kuwa madarakani sijui nchi hii ingekuwa vipi!!!
 
hawa watu ni hatari hiyo kumfukuza tusiichukulie wepesi sana, isipokuwa ni fukuza ya style gani?

daima CCM wanapenda sana kulinda uovu wao, na ndiyo maana kauli ya kwanza unapoapishwa kama
kiongozi uliyetokana CCM, ni kwamba, nitalinda na kutete maslahi ya chama, kutotoa siri za Chama nje,
na siri za chama cha CCM ni uizi mtupu
 
Kama alivyosema Dr. Slaa hawa waliojiita wapambanaji wa ufisadi toka ccm, walitumiwa kuharibu hoja ya upinzani juu ya ufisadi wa ccm kwani walidhihilisha pale waliposhindwa kuihitimisha bungeni na kukubaliana na wenzi wao wengine wa ccm bungeni kuwa wakubaliane yaishe!! Hawa jamaa akiwamo Mwakyembe walikuwa na beef zao na EL na wakapata mwanya wakamfix na kama kweli walikuwa wapambanaji wa kweli kwanini wasiondoke CCm na kujiunga na upinzani wa kweli badala ya kungoja wafukuzwe kama itakavyowatokea? Opportunism yao itaonekana pale wakina Mwakyembe wakifukuzwa CCM halafu kutaka kujiunga na vyama vingine ili tu waukwae ubunge!! Hali ndio hiyo watulie humo humo CCM halafu waamue kunyoa au kusuka.
 
Hivi mbona watu wanawa-underestimate wapiga kura wa Kyela na utashi wa kufanya maamuzi? Hata siku moja matakwa ya viongozi hayawezi kuwa ndiyo maamuzi ya wananchi. Mimi naamini kwamba kama Mwakyembe amewawakilisha vema wapiga kura wa Kyela basi fitna nyingine haziwezi kumng'oa madarakani.
 
uyu jamaa inabidi awe MP

Kama vile hujakosea,hauko mbali na ukweli.
Jamaa anahofiwa sana kama ataingia bunge lijalo la wabunge vijana basikuna uwezekano mkubwa sana
jamaa akampa uwaziri mkuu.kazi aliyoifanya siyo ndogo.
Na sisi wanamtandao na wanablogs tumpe suport ya nguvu maana maana kumtoa waziri mkuu madarakani siyo mchezo.Bigup Dkt Mwakyembe ( Hon MP & Advocate)
 
Tuna imani wananchi wake hawatamwangusha Mwakyembe, jamii ya sasa sio wajinga kiasi hicho kuendelea kudanganywa na mafisadi kila siku:A S-eek:
 
.............litakuwa kama kosa la Obama kumtoa Gen. McChrystal... Mwakyembe hadi sasa wengi hatujakuona umekuwa fighter kwa 100% labda 60% so malizia hizo 40% ukiwa CHADEMA (anti-mafisadi) tena uje sasa kabla hawajakuvua.
 
Jamani huyu akifukuzwa CCM atabaki mbunge gani tena, au ndiyo YES men and women watabaki???????? Tafakari

SIKU moja baada ya Spika wa Bunge, Bw. Samuel Sitta kupata tumaini jipya kwa kuungwa mkono huku akihakikishiwa msaada kurudi kwenye nafasi hiyo na mwanasiasa mkongwe nchini, Bw. John Malecela, hali si shwari kwa Mbunge wa Kyela, Dkt. Harrison Mwakyembe.

Vyanzo vyetu vya kuaminika ndani ya CCM vinaeleza kuwa Dkt. Mwakyembe amewekwa pabaya na wabaya wake kisiasa ambao sasa wamehamishia nguvu zao katika vikao vya chama wilayani Kyela kwa lengo la kummaliza kisiasa.

"Wabaya wa Mwakyembe wamehamisha nguvu zao zote jimboni na wilayani kwake Kyela. Ndani ya CCM Kyela kuna mkakati mzito wa kumng'oa Dkt. Mwakyembe si ubunge tu bali hadi uanachama. Vikao vinafanyika, wameapa kwamba kuwepo Mwakyembe ndani ya bunge lijalo ni kikwazo cha urais kwa baadhi ya wanasiasa wanaosaka nafasi hiyo kwa udi na uvumba," kilisema chanzo chetu.

Imeelezwa kwamba kundi linalomshughulikia Dkt. Mwakyembe limesoma alama za nyakati na kubaini kuwa njia pekee ya kummaliza kisiasa ni kitumia vikao vya chini vya chama hususan ngazi ya wilaya.

Hofu kuu ya kundi hilo ni kwamba iwapo Dkt. Mwakyembe atashinda kipindi kijacho ana uwezo mkubwa wa ushawishi na kutumia vifungu kadhaa vya sheria kukwamisha mipango ya urais kwa baadhi ya wanachama wanaosaka nafasi hiyo mwaka 2015.

"Kuna mikakati michafu inafanyika Kyela hata kutumia vyombo vya habari kutoa ujumbe wa 'kummaliza' kabisa kisiasa Dkt. Mwakyembe, lakini uongozi wa juu umekaa kimya,"kilisema chanzo hicho.

Mbinu zingine zinazodaiwa kuandaliwa dhidi ya Dkt. Mwakyembe ni kupewa alama ndogo, kudaiwa kuwa ana kundi linalokigawa chama wilayani na kama atalalamika, vikao hivyo vitatoa mapendekezo ya kumvua uanachama kwa madai ya kukivuruga chama

"Tayari kazi imekamilika kila kata kinachoendelea sasa ni kampeni za matawi, akipona kwenye kura za maoni lazima akwame katika vikao maalum vya ngazi za wilaya na mkoa,lengo ni kumfukuza kabisa ndani ya chama,"kilisema chanzo hicho na kuongeza;

"Taarifa hizi zote zinajulikana ngazi za juu lakini hakuna hatua zinazochukuliwa, sijui kama mbinu hizi zina baraka au mamlaka ya juu inaogopa nini wakati mambo yanaharibika?"alisema Mjumbe mmoja wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC) kwa sharti la kutoandikwa jina gazetini.

Majira lilipomtafuta Dkt. Mwakyembe ili kujua kama ana taarifa juu ya mpango huo na msimamo wake, alikiri kuwa na taarifa hizo huku akikataa kutoa ufafanuzi kwa kile alichodai kwamba wananchi ndio watatoa jibu.

"Ninajua kila kinachoendelea, ninajua akina nani wanahusika, mimi siyo mjinga hata sasa niko huku Kyela, mngetaka kujua kwa undani hayo unayoniuliza ungekuja Kyela,"alisema Dkt. Mwakyembe bila kutoa ufafanuzi wa kina.

Alipoulizwa hatua alizokwishachukua juu ya suala hilo alisema "Nakumbuka niliwahi kusema kwamba taarifa zote nilishatoa sasa ukitaka fuatilia huko mbele, lakini naomba usisahau kitu kimoja, uamuzi wangu wa mwisho utatolewa na wananchi siku ikifika, mafisadi watumie mamilioni au mabilioni, wafanye nini uamuzi wa mwisho utatolewa na wananchi,"alisisitiza.

Majira ilipomtafuta Katibu wa CCM Itikadi na Uenezi Mkoa wa Mbeya Bw. Basiru Madodi, ili kujua ukweli wa suala hilo, alikiri kusikia taarifa hizo mitaani lakini si rasmi.

"Na mimi nimesikia tu hizo taarifa kama ulivyosikia wewe, hivi sasa tunaendelea kufanya uchunguzi ili kujua ukweli maana Jimbo la Mbeya inaonekana kuna makundi tunataka tujiridhishe kwanza kabla ya kusema chochote,"alisema Bw. Madodi.

Alipoulizwa makundi hayo alisema yanatokana na makovu ya Uchaguzi Mkuu mwaka 2005.

Akizungumza na Majira kwa njia ya simu jana, Mwenyekiti wa Kamati ndogo ya Udhibiti ya Kamati ya Usalama na Maadili ya Taifa ya CCM, Bw. Pius Msekwa, alikiri kupokea malalamiko mengi kuhusu njama hizo za kuangushwa wabunge.

Alisema malalamiko hayo yanashughulikiwa na kwamba kabla ya Uchaguzi Mkuu kila kitu kitakuwa hadharani huku akikataa kuzungumzia suala la Dkt. Mwakyembe pekee kwa maelezo kwamba ana malalamiko mengi mezani kwake.

"Hatujapuzia malalamiko ya Waheshimiwa wabunge, ni kweli nimepokea malalamiko mengi sana siwezi kusema ni ya fulani na fulani yapo mengi sana na tunaendelea kuyashughulikia, tayari tumetoa taarifa inayoonesha ratiba ya kushughulikia na tutatoa taarifa baada ya kumaliza kazi,"alisema Bw. Msekwa.


source: Mwakyembe kufukuzwa CCM

hivi mtaacha lini kuwa vibaraka?kwani akifukuzwa yeye ni nani to this country leave alone Kyela?na afukuzwe tu na wala sio kikwazo kwa mtu yoyote yule...just rubbish na kuogopa kivuli chake
 
Kwani CCM ni mama yake Mwakyembe? Acha wamfukuze uanachama, tena wafanye haraka kama wanataka upinzani utwae kiti cha Kyela tena kwa kumtumia Mwakyembe huyohuyo.
 
.............litakuwa kama kosa la Obama kumtoa Gen. McChrystal... Mwakyembe hadi sasa wengi hatujakuona umekuwa fighter kwa 100% labda 60% so malizia hizo 40% ukiwa CHADEMA (anti-mafisadi) tena uje sasa kabla hawajakuvua.

McChrystal kuondolewa ni kosa kivipi?mi sijakuelewa
 
Back
Top Bottom