Mwakyembe apuuza data za JamiiForums!

Status
Not open for further replies.
mwakyembe ajielewi kwani hata mgogoro uliokuwapo kwenye chama chake yeye ndie aliyechangia kwa kiasi kikubwa baada ya kuteuliwa kuongoza kamati alitoa mapendekezo ya kisiasa badala ya kisheria (alichanganya siasa na sheria) pale alipomwambia aliekuwa waziri mkuu ajipime badala ya kumwambia tumekuona na dosari hizi hivyo ama aufai,ashitakiwe au vyovyote kwa mujibu wa sheria.

Baada ya Edward Lowasa kuanza kampeni ya kujisafisha aliomba mjadala urudi bungeni ili waweze kueleza mambo waliyoyaficha.Je anajua wakati wa uchunguzi walikuwa wanatumia kodi za wananchi,pia waliacha kwa manufaa ya nani? Kitendo hicho ndio kimewapa sifa mafisadi kuonyesha walionewa.

Kwa kipindi chote alichoumwa alikataa kujiuzuru nafasi yake ili ateuliwe mtu mwingine kitendo hicho kiliigharimu serikali pesa nyingi kwani ilikuwa inamlipa mtu asiye na mchango wowote.

Naomba ajipime kabla ya kukurupuka wamempa uwaziri kwa sababu wanajua alichokuwa anatafuta ni sifa
 
It is good to know that na yeye Mwakyembe anasoma Jamii Forums, vinginevyoa aliijuaje?
 
Sishangai yeye kusema hivyo, tuna msubiri kwani wote wanao ibeza jf wanaumbuka.
Kwani msema kweli hupingwa! Sitegemei serikali kuipenda jf kwani uongo wao unachambuliwa vizuri hapa na kuwekwa wazi.

Hawezi kuwa wa kwanza kutoikubali jf, anatakiwa awaulize

1:Shigongo
2:Mama Rwakatare


Hajui atendalo, angejua kuwa kupona kwake kuna mkono wa JF angeishukuru na kuichangia mara dufu!

Jf ndio inayofichua maovu ya nchi hii na ndio kisima cha hekima kwa wanasia machipuko, na zaidi jf ndio iliyofichua njama za jaribio la yeye kuuawa na kila aina ya hila dhidi yake lakini leo anaiona si chochote?

Aje ajiunge huko tumpige msasa huyo!
 
Mimi nina amini, mtu yoyote anayeitaja JF ima kwa mabaya au mazuri ni mwanachama wa JF....na kwa hy inawezekana habari za JF zinamuathiri negatively or positively...Mwakyembe kaonyesha kuwa uwa anapitaga hapa JF mara kwa mara na aliiona hiyo habari. Viva JF...
 
Nimefanya research zaidi ya 12 mpaka sasa na most of informations nimezipata hapa JF. Anayeipuuza JF na alaaniwe!!
 
Alichoongea kina ukweli. Kuna threads nyingi zinaanzishwa zinakuja kuishia hewan. Mfno.
1.kashfa ya Gen. Shimbo na mabillion ya fedha ya wanajeshi waliopo dafur...
2.kufumaniwa kwa simbachawene na mke wa mtu singida na kujeruhiwa mkono wake...
Lazima tukubali ukweli.
3...
 
Kaka,

Uko serious? Hizo data ni za JamiiForums?

Mkuu Maxence Melo,

Hilo swali kuniuliza mie ni kunionea heading ya hii thread ni "Mwakyembe apuuza data za JamiiForums!"

Haya sio maneno yangu mie binafsi naamini maoni ya members wa JF sio kauli ya JF.
 
Last edited by a moderator:
Mwakyembe anapaswa kuomba radhi . Uzi tayari nimeuweka kuhusu hizo data aseme tena zitawekwa na za ziada punde kuhusu yeye na wizara yake mpya.
 
Akimjibu Mh. Wenje kuhusu uwepo wa mpango wa kuwapatia wageni bandari ya Mtwara kw fidia ya deni la serikali Waziri Mwakembe alikanusha kata kata kuwepo kwa mpango huo na akaongeza kuwa "Taarifa kama hizi ndiyo matokeao ya kufuatilia habari za Jamii Forum".

Wana jamii tunakubaliana na hilo kwamba hapa JF ni mahali pa kupika taarifa za uwongo wakazitumia wabunge?
Hiyo bahari ya batter trade waliyopendekeza wachina waliotaka kujenga terminal three alishaisema Zitto tangu kikao cha April ndio zikafika hapa JF. Wenjer na yeye amekuwa mvivu tu wa kuuliza vema swali lake
 
Kazi ipo nchi hii!!!

Dudumizi linazidi kuota kirija ya unyonyaji damu!!!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom