sir.JAPHET
JF-Expert Member
- May 18, 2012
- 699
- 133
[h=2] Mwakilishi wa CCM azomewa kwenye kongamano [/h] Jumatatu, Septemba 03, 2012 05:27 Na Arodia Peter
MWAKILISHI wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Godwin Kunambi, juzi alipata wakati mgumu wakati alipokuwa akitoa maoni yake kuhusu msimamo wa chama chake kuhusu Katiba mpya.
Tukio hilo lilitokea jijini Dar es Salaam wakati wa mjadala wa Katiba mpya ulioandaliwa na Jukwaa la Katiba.
Kabla Kunambi hajazomewa, alianza kwa kueleza msimamo wa chama chake na kusema ni mambo gani yanayotakiwa kuendelea kuwamo katika Katiba mpya inayoandaliwa.
Sisi kama chama, tunaona tuendelee kuheshimu misingi ya kikatiba kwa maana ya mihimili mitatu ya dola, umuhimu wa kuendelea kuwa na muungano wa Serikali mbili na zaidi misingi mikuu kama vile ardhi kuendelea kuwa mikononi mwa miliki ya Serikali,alisema Kunambi.
Wakati akiendelea kusema hayo na mengine, ukumbi mzima ulilipuka na kukatiza hotuba yake huku baadhi ya washiriki wakimzomea na kumtaka akae chini.
Wakati wa tukio hilo, Kibamba alipata wakati mgumu kuwatuliza, lakini waliendelea kupiga makofi mfululizo na kufanya yale aliyokuwa akiyazungumza yasisikike kabisa.
Awali, Mwenyekiti wa Baraza la Katiba Zanzibar, Profesa Abdul Sharif, alisema Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, matatizo yake hayatokani na wananchi wa pande mbili, isipokuwa ni mfumo ulioasisi muungano huo.
Alisema kwamba, muungano uliopo, uliharibiwa tangu mwanzo na waasisi wa wake kwa kuwa hakuna chombo chochote cha kisheria visiwani humo kilichoridhia muungano huo.
Katika hili Zanzibar ilipunjwa zaidi kwa sababu hakuna chombo chochote cha kisheria kilichoridhia uhalali wa muungano huo, hakuna tangazo lolote lililotolewa katika Gazeti la Serikali kuarifu umma kuhusu maridhiano ya Muungano huo, mambo yote yalikwenda kienyeji na hii ndiyo sababu nchi zingine kama Zambia ambazo awali zilitaka kuungana nasi zilisita kufanya hivyo,alisema Profesa Sharrif.
Naye Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba Tanzania, Deus Kibamba, alisema wataendelea kuongoza Watanzania kufuatilia hatua kwa hatua kwa umakini mkubwa ili ipatikane Katiba nzuri zaidi katika historia ya Tanzania.
Hamida Issa kutoka Biharamulo, Kagera alisema, Katiba mpya ijayo inatakiwa kutamka wabunge wa Viti Maalum wanapaswa kuwajibika kwa wanawake wote na si vyama vyao kama ilivyo sasa.
Naye Adam ole Mwarabu, ambaye amejitambulisha kuwa mwakilishi wa jamii ya wafugaji, alisema Katiba ijayo inapaswa kutambua sehemu ya mila, desturi, tamaduni na ujuzi wa asili ili uhifadhiwe na kutambuliwa na katiba hiyo.
Mshiriki mwingine, Martina Kabisama, kutoka Taasisi ya Masuala ya Haki za Binadamu Kusini mwa Afrika (SAHRINGON), alisema Tume Huru ya Uchaguzi lazima itamkwe kwenye Katiba.
Tusipokuwa na Tume huru ya Uchaguzi, haki ya raia inakuwa imeminywa, alisema.
[h=4]Toa Maoni yako kwa habari hii[/h]
MWAKILISHI wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Godwin Kunambi, juzi alipata wakati mgumu wakati alipokuwa akitoa maoni yake kuhusu msimamo wa chama chake kuhusu Katiba mpya.
Tukio hilo lilitokea jijini Dar es Salaam wakati wa mjadala wa Katiba mpya ulioandaliwa na Jukwaa la Katiba.
Kabla Kunambi hajazomewa, alianza kwa kueleza msimamo wa chama chake na kusema ni mambo gani yanayotakiwa kuendelea kuwamo katika Katiba mpya inayoandaliwa.
Sisi kama chama, tunaona tuendelee kuheshimu misingi ya kikatiba kwa maana ya mihimili mitatu ya dola, umuhimu wa kuendelea kuwa na muungano wa Serikali mbili na zaidi misingi mikuu kama vile ardhi kuendelea kuwa mikononi mwa miliki ya Serikali,alisema Kunambi.
Wakati akiendelea kusema hayo na mengine, ukumbi mzima ulilipuka na kukatiza hotuba yake huku baadhi ya washiriki wakimzomea na kumtaka akae chini.
Wakati wa tukio hilo, Kibamba alipata wakati mgumu kuwatuliza, lakini waliendelea kupiga makofi mfululizo na kufanya yale aliyokuwa akiyazungumza yasisikike kabisa.
Awali, Mwenyekiti wa Baraza la Katiba Zanzibar, Profesa Abdul Sharif, alisema Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, matatizo yake hayatokani na wananchi wa pande mbili, isipokuwa ni mfumo ulioasisi muungano huo.
Alisema kwamba, muungano uliopo, uliharibiwa tangu mwanzo na waasisi wa wake kwa kuwa hakuna chombo chochote cha kisheria visiwani humo kilichoridhia muungano huo.
Katika hili Zanzibar ilipunjwa zaidi kwa sababu hakuna chombo chochote cha kisheria kilichoridhia uhalali wa muungano huo, hakuna tangazo lolote lililotolewa katika Gazeti la Serikali kuarifu umma kuhusu maridhiano ya Muungano huo, mambo yote yalikwenda kienyeji na hii ndiyo sababu nchi zingine kama Zambia ambazo awali zilitaka kuungana nasi zilisita kufanya hivyo,alisema Profesa Sharrif.
Naye Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba Tanzania, Deus Kibamba, alisema wataendelea kuongoza Watanzania kufuatilia hatua kwa hatua kwa umakini mkubwa ili ipatikane Katiba nzuri zaidi katika historia ya Tanzania.
Hamida Issa kutoka Biharamulo, Kagera alisema, Katiba mpya ijayo inatakiwa kutamka wabunge wa Viti Maalum wanapaswa kuwajibika kwa wanawake wote na si vyama vyao kama ilivyo sasa.
Naye Adam ole Mwarabu, ambaye amejitambulisha kuwa mwakilishi wa jamii ya wafugaji, alisema Katiba ijayo inapaswa kutambua sehemu ya mila, desturi, tamaduni na ujuzi wa asili ili uhifadhiwe na kutambuliwa na katiba hiyo.
Mshiriki mwingine, Martina Kabisama, kutoka Taasisi ya Masuala ya Haki za Binadamu Kusini mwa Afrika (SAHRINGON), alisema Tume Huru ya Uchaguzi lazima itamkwe kwenye Katiba.
Tusipokuwa na Tume huru ya Uchaguzi, haki ya raia inakuwa imeminywa, alisema.
[h=4]Toa Maoni yako kwa habari hii[/h]