VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Ni kituo cha Mabasi ya Mikoani Ubungo. Naingia kukata tiketi ya Arusha. Nimeshaipata. Sasa wakati natoka nje,nawakuta madereva wa taksi na bajaji wanawazonga vijana wawili:mmoja msichana,mmoja mvulana. Nikasogea kuona na kusikia. Walikuwa wanazongwa ili wapande kwenye ima bajaji au taksi ili wapelekwe UDSM kwakuwa ndio wamefika kama wanafunzi wa mwaka wa kwanza.
Kwa uzalendo wangu kama mwana-UD wa zamani nikaingilia kati na kuinunua kesi. Nikawasogeza pembeni wanafunzi wale. Wakaniarifu mengi. Kubwa ni kwamba wanataka kufika UDSM. Wamebeba unga,mchele,maharage,mafuta ya kupikia na mafuta ya taa. Wa kike amebeba na sufuria na baadhi ya vyombo vya chakula. Si mchezo!
Sasa kituko: wakaniarifu kuwa wao ni ndugu wanaotokea Bukoba. Wakasema kuwa wameambiwa nyumbani kuwa wakae chumba kimoja ili kupunguza gharama. Wahakikishe inakuwa hivyo. Ni lazima. Itawezekanaje ikiwa UDSM kuna hosteli za kike na za kiume? Mwisho mwishoni,nikawachukua garini mwangu hadi UDSM. Nimewashusha stendi ya Utawala.Nikawauliza:mnahitaji msaada wowote mwingine? Wakajibu:'hapana kaka.Hapa tumeshafika.Asante sana'. Kazi ipo...
Kwa uzalendo wangu kama mwana-UD wa zamani nikaingilia kati na kuinunua kesi. Nikawasogeza pembeni wanafunzi wale. Wakaniarifu mengi. Kubwa ni kwamba wanataka kufika UDSM. Wamebeba unga,mchele,maharage,mafuta ya kupikia na mafuta ya taa. Wa kike amebeba na sufuria na baadhi ya vyombo vya chakula. Si mchezo!
Sasa kituko: wakaniarifu kuwa wao ni ndugu wanaotokea Bukoba. Wakasema kuwa wameambiwa nyumbani kuwa wakae chumba kimoja ili kupunguza gharama. Wahakikishe inakuwa hivyo. Ni lazima. Itawezekanaje ikiwa UDSM kuna hosteli za kike na za kiume? Mwisho mwishoni,nikawachukua garini mwangu hadi UDSM. Nimewashusha stendi ya Utawala.Nikawauliza:mnahitaji msaada wowote mwingine? Wakajibu:'hapana kaka.Hapa tumeshafika.Asante sana'. Kazi ipo...