shegaboy
JF-Expert Member
- Apr 11, 2011
- 213
- 34
Msomi mmoja alikutana na mvuvi moja katika chombo yaani mtumbwi walikuwa wakivuka kuelekea ngambo ya pili. Yule msomi akamwambia yule mvuvi ndugu yangu wewe umesoma? yule mvuvi akamwambia duu! umepoteza asilimia 20% katika maisha yako. akamuuliza una tv kwako akasema hapana umepoteza asilimia 20% ya maisha yako. akamwambia unatakiwa kuwa na ufahamu katika hayo kama elimu ni muhimu katika maisha na radio na tv unapata taharifa mbali mbali sasa wewe una. Mara hali ya hewa baharini ikaarinika mtumbwi ukaanza kuyumba yumba uku na kule.YULE MVUVI AKAMWAMBIA MWENZANGU UNAJUA KUOGELEA AKASEMA HAPANA. AKAMWAMBIA UMEPOTEZA MAISHA YAKO YOTE.