Mvutano uenyekiti wafukuta chadema

Status
Not open for further replies.

FIKRA MBADALA

Senior Member
Jun 30, 2008
167
16
Hali ya mambo ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), bado si shwari baada ya kuibuka mvutano wa kuwania nafasi ya Mwenyekiti wa Taifa ambayo kwa sasa inashikiliwa na FREEMAN MBOWE.

Habari za uhakika zilizopatikana kutoka ndani ya chama hicho zinaeleza kuwa, mvutano uliopo hivi sasa ni wa kuwania nafasi ya Mwenyekiti wa CHADEMA katika uchaguzi mkuu wa chama hicho unaotarajiwa kufanyika Mwezi Machi mwaka 2009. Awali uchaguzi huo ulipangwa kufanyika mwezi Desemba 2008, kabla ya kuahirishwa kwa kile kinachoelezwa na wafuatiliaji wa siasa ndani ya chama hicho kuwa ni kutokana na mvutano wa uongozi unaofukuta.

Kimsingi, mvutano wa uongozi ndani ya CHADEMA ni mkubwa kiasi cha kusababisha kuibuka kwa makundi matatu yanayogombea kushika wadhifa wa Mwenyekiti. Makundi hayo yana nguvu na kila moja limejiandaa kupigana kwa nguvu zote ili kuhakikisha kuwa linatwaa Uenyekiti wa chama hicho.

Makundi hayo ni lile linalomuunga mkono Mwenyekiti wa sasa, FREEMAN MBOWE na ambalo kwa sehemu kubwa linaundwa na viongozi na wanachama wenye nyadhifa na uhusiano mzuri na Makao Makuu ya CHADEMA. Kundi hili limeanza kujiandaa kuhakikisha kuwa MBOWE anarejea tena katika uongozi wa chama hicho, na ndiye atakuwa mgombea wa Urais wa chama katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.

Taarifa inaeleza kuwa, wafuasi wa kundi hili, wanajua MBOWE amepoteza umaarufu ndani na nje ya chama lakini wanajua kuwepo kwake katika uongozi ni jambo la kheri kwao. Kundi hili, bado linamuona MBOWE kuwa ni kiongozi mwenye mvuto na anaweza kuendelea na uongozi wa chama hicho pamoja na kuwepo kwa tuhuma na migogoro iliyochafua wasifu wake katika siku za hivi karibuni.

Hata hivyo, wafuatiliaji wa mambo ndani ya CHADEMA wanaamini kuwa, MBOWE amepoteza umaarufu hasa kutokana na kutajwa kuwa ndiye chanzo cha migogoro ambayo imekuwa ikijitokeza ndani ya chama hicho.

Kundi la pili na lililoibuka na ambalo linaelezwa kuwa na nguvu zaidi, ni lile linalomuunga mkono katibu wa chama hicho, DR. WILBROAD SLAA. Kundi hili linaloaminika kuwa na ngome yake katika Kanda ya Ziwa, linajenga hoja kuwa DR. SLAA ndiye mtu pekee ndani ya chama hicho ambaye anaonyesha sifa ya kukiongoza chama hicho na kukiletea tija kisiasa.

Kundi la DR. SLAA linaonekana kuwa na nguvu zaidi kwa sababu linaungwa mkono na wanachama wengi ambao wanataka kuona chama kikipata mafanikio zaidi na kurejesha imani yake kwa wananchi. Wafuasi wa DR. SLAA wanamuona kuwa hana kashifa kama alivyo Mwenyekiti wa chama, MBOWE na ndiyo maana wanataka ashike usukani ili kuokoa chama kisisambaratike.

Kambi hii, inadai kuwa CHADEMA inahitaji kupata mtu msafi (ambaye hajachafuka) anayeungwa mkono na wanachama wa kawaida na ndiye atakisadia chama hicho kuimarika katika ngazi za chini badala ya kuwa cha Makao Makuu.

Mbali na makundi hayo mawili ambayo kwa sehemu kubwa ndiyo yanaonekana kuwa na mchuano mkali, lipo kundi la tatu ambalo linaelezwa kuungwa mkono na watu wenye pesa ndani na nje ya chama hicho. Kundi hili ambalo limepachikwa jina la kundi la wenye fedha kutokana na kujumuisha wafanyabiashara matajiri, linaamini kuwa chama kinapaswa kuongozwa na watu wenye umri mkubwa kama MZEE PHILEMON NDESAMBURO.

Habari zinadai kuwa, kundi linalomuunga mkono NDESAMBURO ni lile ambalo limekuwa likinufaika na chama katika kufanya biashara zao. Hata hivyo, wanachama wasiolitaka kundi la NDESAMBURO wanadai kuwa katika kikundi chochote watu hawawi na malengo ya kufanana, wengine wanataka kutumia kikundi kujinufaisha binafsi na wengine wanataka kuona kikundi kikifanikiwa. Hivyo, hata ndani ya CHADEMA kuna wachache ambao wapo humo lakini wanataka kuhakikisha mambo yao yakifanikiwa kupitia chama na hawa ndio wanaounga mkono watu wenye pesa na walio na mawazo ya kibiashara ndani ya chama hicho.

Kuna madai kuwa kuibuka kwa kundi la tatu ni ishara ya kuwa waasisi wa chama hicho hawako tayari kuona chama kikiondoka mikononi mwao na kuwaachia wageni kutoka CCM kama ilivyo kwa DR SLAA. Hata hivyo, watu wanaojenga dhana kuwa kundi hili halina madhara kwa makundi mengine, kwa maana kwamba watu wenye umri mkubwa kama NDESAMBURO hawana jipya linaloweza kuwashawishi na kuwavutia wapiga kura ambao wengi wao ni vijana.

Aidha, kuna kundi la aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, Marehemu CHACHA WANGWE. Kundi hili, linajumuisha wanaCHADEMA waliokuwa wanamtaka CHACHA WANGWE kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa Taifa (CHADEMA). Baada ya kifo cha WANGWE, kambi hii haijaamua mgombea wa kumuunga mkono kati ya kundi la MBOWE, DR SLAA na NDESAMBURO. Hata hivyo, kundi hili limeweka wazi kwamba halitamuunga mkono Mwenyekiti wa sasa, FREEMAN MBOWE.

Habari zaidi zinaonyesha kuwa kuibuka kwa mvutano huu wa kuwania uongozi wa CHADEMA, kumetokana na kubaini kuwa Mwenyekiti MBOWE amechafuka kiasi cha kuwa mzigo kwa chama, viongozi wenzake na Watanzania waliokuwa wakiunga mkono sera za CHADEMA.

Wanaopinga MBOWE wanasema kuwa, baadhi ya kashifa ambazo zinamwandama ni pamoja na ya kuacha majina yaliyopendekezwa na chama kuwa wabunge wa viti maalum na kujaza ya watu aliowataka yeye.

Kashfa nyingine ni ya chama kukimbiwa na viongozi wa juu kwenda CCM au kuanzisha chama kingine kama ilivyotokea kwa aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, DR AMANI WALID KABOUROU ambaye alihamia CCM na PAUL KYARA aliyekuwa Mweka Hazina wa CHADEMA Taifa ambaye kwa sasa ni Mwenyekiti wa chama cha Sauti ya Umma.

Miongoni mwa kashifa hizo, ipo pia ya matumizi mabaya ya pesa za ruzuku ikiwemo kulipa madeni yaliyotokana na matumizi ya Helkopta katika kampeni za Urais kwenye uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005.

Kashfa ambayo imemchafua zaidi MBOWE katika siku za karibuni ni ya kuhusishwa na Kifo cha aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wake CHACHA WANGWE ambaye pamoja na mambo mengine alikuwa akihoji masuala tajwa hapo juu. Kifo cha WANGWE kimesababisha MBOWE kushambuliwa kwa mawe huko Tarime wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo wa Jimbo hilo uliofanyika hivi karibuni. Ikumbukwe pia kuwa MBOWE hakwenda kumzika WANGWE kutokana na sababu hizo hizo.

Kutokana na mlolongo wa matukio haya wana-CHADEMA wanaona ni kwa nini MBOWE asikae pembeni ili kutoa nafasi kwa watu wasio na kashfa?
Wana JF, habari hii inatupa changamoto ya kuanzisha mdahalo (debate) wa kuchanganua mipaka ya kuwajibika kwa viongozi wa kisiasa nchini. Imekuwa ni kawaida na mazoea kwa vyama vya upinzani nchini kudai viongozi wa chama tawala CCM wawajibike wakati wao hawafikirii kufanya hivyo kwa wanachama wao waliowachagua. Nimekuwa sipati jibu ni kwa nini viongozi wa kisiasa wawe wa upinzani au chama tawala ni wagumu kuwajibika ili kuonyesha mfano wa kuigwa? Je, ni udikteta au ni kukosa sifa za uongozi?

Naomba kutoa hoja.
 
Hoja yako haina nguvu kwa sasa labda uzungumzie ushindi wa tarehe na hali ya kisiasa kwa sasa , kwa nini viongozi wetu ambao ni wa CCM sasa wanazomewa na si wapinzani.
hii ni kutaka kupooza machungu wanaopata chama tawala.
 
Kifo cha WANGWE kimesababisha MBOWE kushambuliwa kwa mawe huko Tarime wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo wa Jimbo hilo uliofanyika hivi karibuni. Ikumbukwe pia kuwa MBOWE hakwenda kumzika WANGWE kutokana na sababu hizo hizo.

Inaonyesha hii "hadithi" uliiandika tangu Septemba! au na wewe ni "George Marato" wa JF!!
 
Kuwa na kambi kuwania nafasi ya uchaguzi siyo kosa jamani, tutaachana na mawazo haya hadi lini? Naamini itakuwa vizuri hizo kambi zijulikane wazi na wajikampeni kwa wanachama wao. Na hilo unaweza kuandika na usiwe uchochezi.

Siyo kama kwenye CCM ambapo habari kuwa kuna wanachama wake wanaotaka kuhakikisha JK hagombei tena 2010 zimechukuliwa ni uchochezi!. Itakuwa ni hatari sana kama Chadema haitaruhusu kambi za wagombea kuundwa na kufanya kampeni. Itakuwa vizuri kama watawapa moyo wale wote wanaotaka kugombea nafasi mbalimbali ikiwemo ile ya Uenyekiti.
 
Kuwa na kambi kuwania nafasi ya uchaguzi siyo kosa jamani, tutaachana na mawazo haya hadi lini? Naamini itakuwa vizuri hizo kambi zijulikane wazi na wajikampeni kwa wanachama wao. Na hilo unaweza kuandika na usiwe uchochezi.

Siyo kama kwenye CCM ambapo habari kuwa kuna wanachama wake wanaotaka kuhakikisha JK hagombei tena 2010 zimechukuliwa ni uchochezi!. Itakuwa ni hatari sana kama Chadema haitaruhusu kambi za wagombea kuundwa na kufanya kampeni. Itakuwa vizuri kama watawapa moyo wale wote wanaotaka kugombea nafasi mbalimbali ikiwemo ile ya Uenyekiti.

Mwanakijiji
Huyu fikra mbadala ana lake jambo; sio hoja kama ulivyoiweka. Kugombea nafasi za uongozi, si ni kufuata katiba ya chama chao inasemaje? Naamini Chadema ni chama kinachoongozwa kufuatana na kanuni.
 
hizo ndio kambi zilitoanzishwa na mwanakijiji alivyoenda tarime ? mwanakijiji njoo mbele utueleze najua ulitembelea tarime siku za karibuni na wanachama wenzako wa chama fulani
 
huyu anachokonoa hakuna hoja ndani ya habari yake... mambo ya kifo cha wangwe bado alaizumngumzia.. na mtu anayezungumzia hilo hana hoja
 
Kuwa na kambi kuwania nafasi ya uchaguzi siyo kosa jamani, tutaachana na mawazo haya hadi lini? Naamini itakuwa vizuri hizo kambi zijulikane wazi na wajikampeni kwa wanachama wao. Na hilo unaweza kuandika na usiwe uchochezi.

Siyo kama kwenye CCM ambapo habari kuwa kuna wanachama wake wanaotaka kuhakikisha JK hagombei tena 2010 zimechukuliwa ni uchochezi!. Itakuwa ni hatari sana kama Chadema haitaruhusu kambi za wagombea kuundwa na kufanya kampeni. Itakuwa vizuri kama watawapa moyo wale wote wanaotaka kugombea nafasi mbalimbali ikiwemo ile ya Uenyekiti.

Umeongea kweli mwanakijiji, kuwa na kambi si dhambi ili kuupata uenyekiti. Kwa sababu kufikia lengo lile lile moja kila mtu atakuwa na strategy tofauti anayoona yeye na kundi lake kuwa inafaa, kwa hiyo suala hapa ni kupambanisha mitazamo na fikra mbele ya wanachama wenu na si kununua wanachama.

Suala jingine hivi vyama vinabidi viwe tofauti kidogo na CCM, sio kuwa CCM wakipishwa jina moja kwa nafasi ya Mwenyekiti/Makamu lipigiwe kura ya NDIO au HAPANA na vyama vingine navyo viige hivyo hivyo ...kunakuwa hakuna maana ya kuwa na vyama vingi kama kila kitu mnalingana.

Na mwsho ni kuwa kiongozi anapokuwa anajua kuwa hana hati miliki ya chama kwa kuwa wanachama wakati wowote wanawenza kumuondoa, itambidi achape kazi kujijengea trust kwa wanachama wake na sio kutumia nguvu yako ya pesa au mabavu kulinda himaya yako.
 
Source ya hii habari pls .... kabla ya kurukia na kuanza kuishambulia CHADEMA Kwa kuwa na kambi (kitu ambacho inawezekena sio kweli lakini hakina madhara yoyote kwenye chama) kutokana na hii habari ambayo inaonesha kuwa imeandikwa na watu wale wale ambao walitaka wananchi wa Tarime wapigane kutokana na kifo cha Wangwe.

Hii haina tofauti na kile ambacho TBC1 na magazeti ya Rostam walifanya wakati wa msiba. Wananchi sasa wameelimika na sidhani kama wanachukulia habari za uzushi kama hizi.
 
Naona haka ni ka mkakati ka kutaka kutuhamisha katika hoja za msingi, kwani umeambiwa kuwa na makundi ya kuwania nafasi za uongozi ni mgogoro ama ni hoja? Wacha watu watumie demokrasia yao.
 
Mtizamo wangu, huu uzushi, uchonganishi na usongombingwo.

Kama CHADEMA wanakwenda kwenye uchaguzi, hata mtoa mada unaweza kuchukua fomu kuomba kugombea uongozi na ukatafuta watu wa kukuunga mkono, sio kuleta uchonganishi wenye nia za kurudisha nyuma harakati za Mageuzi Tanzania.

Hoja yako haina nguvu kwani Chadema tumeshuhudia safu mbalimbali za uongozi zikiingia na kukabidhiana vijiti kwa heshima, na tena kwa njia ya kura. Hainashaka kuwa wanaamini kuwa chama ni watu na viongozi ni watumishi wa watu tu.
 
Heshima Zenu Wakuu,

Mimi nadhani hoja hii ina maana sana kwetu, This is the time to be REAL, not EXCITED. Mimi naiishabikia CCM, Nilidhani kuwa JK ALIkuwa serious kuinfluence internal revolution kukirid CHAMA OF the old Gang in exchange of new blood and ideas. But unfortunately JK has succumbed to Power Mongers. This is the only opportunity for any Real Mzalendo to join forces with Chadema under Dr Slaa to push out CCM into political Siberia. Ni kweli Mbowe is past his sellout date.

Once of the toughest political decision is that of replacing a young Dynamic Leader with a Charimatic PRESIDENTIAL HOPEFUL. lets all try to work towards this.
 
Heshima Zenu Wakuu,

Mimi nadhani hoja hii ina maana sana kwetu, This is the time to be REAL, not EXCITED. Mimi naiishabikia CCM, Nilidhani kuwa JK ALIkuwa serious kuinfluence internal revolution kukirid CHAMA OF the old Gang in exchange of new blood and ideas. But unfortunately JK has succumbed to Power Mongers. This is the only opportunity for any Real Mzalendo to join forces with Chadema under Dr Slaa to push out CCM into political Siberia. Ni kweli Mbowe is past his sellout date.

Once of the toughest political decision is that of replacing a young Dynamic Leader with a Charimatic PRESIDENTIAL HOPEFUL. lets all try to work towards this.

Ulikuwa ukiishabikia ama bado unaishabikia?



.
 
Mhh kaazi kwelikweli

Nakumbuka usemi wa Obama kuwa " Kama wewe ni mzungu na boti yako imezama unaelea juu ya pipa akatokea mtu mweusi akakurushia kamba utaidaka akuokoe???
 
Hii habari hata kama ni ukweli, iweje watu kugombea nafasi kwenye uchaguzi igeuke kuwa mpasuko kwenye chama?

Hiyo ndio demokrasia yenyewe na wakati wa uchaguzi ukifika inabidi watu wakubali kwamba ni demokrasia kwa wengine pia kugombea nafasi zao.

Hata CCM itafaa kama watu wengi watajitokeza kumpinga JK.
 
Kama kuna mwanachama yeyote wa CHADEMA hapa nomba anipe muongozo ni jinsi gani naweza kupata kadi ya uanachama wa CHADEMA? Send me text message in my PM. This is serious. Nilikuwa na namba za baadhi ya member wa CHADEMA, I lost all with my other staffs while nasafiri. I would love to work with Mbowe,Zito,dogo, Slaa,Lisu etc

Some one help.siwezi tena jizuia!!!!!!!

waberoya
 
Kutokana na mlolongo wa matukio haya wana-CHADEMA wanaona ni kwa nini MBOWE asikae pembeni ili kutoa nafasi kwa watu wasio na kashfa?
Wana JF, habari hii inatupa changamoto ya kuanzisha mdahalo (debate) wa kuchanganua mipaka ya kuwajibika kwa viongozi wa kisiasa nchini. Imekuwa ni kawaida na mazoea kwa vyama vya upinzani nchini kudai viongozi wa chama tawala CCM wawajibike wakati wao hawafikirii kufanya hivyo kwa wanachama wao waliowachagua. Nimekuwa sipati jibu ni kwa nini viongozi wa kisiasa wawe wa upinzani au chama tawala ni wagumu kuwajibika ili kuonyesha mfano wa kuigwa? Je, ni udikteta au ni kukosa sifa za uongozi?

Naomba kutoa hoja.

Bla blah, na huu ndo uhuru wa kuongea. Si uwaachie wenyewe? CHADEMA si kampuni ni chama. Jiunge kabadilishe mambo brother.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom