Makala Jr
JF-Expert Member
- Aug 25, 2011
- 3,395
- 1,110
Wiki hii imekuwa ni wiki yenye maajabu ambayo sikuwahi kuyafikifiria.Vurugu zilizotokea zanzibar kwa kuchagizwa na kundi la kiislamu liitwalo Jumuiya ya uamsho ni matokeo ya nini? Mara kadhaa kundi hilo limekaririwa na vyombo kadhaa vya habari kuwa kundi hilo linaupinga muungano kwani hauna maslahi kwa zanzibar.Ndugu wana jf naomba ufafanuzi wa kina:mahusiano ya muungano wetu na ukristo.Kama jumuiya ya uamsho wanapinga muungano then,kwa nini makanisa yachomwe? Je,baraza la kuu la waislamu wanalitambua kundi hilo kama jumuiya halali ya kiislamu? Wana jf naomba mwenye habari kamili aelezee endapo jumuiya ya uamsho haina mwonekano kama ule wa Boko haramu,Al-shabab n.k Karibuni tujadili kwa ajili ya hatma ya Tanzania tunayoipenda.