George Kahangwa
JF-Expert Member
- Oct 18, 2007
- 547
- 147
Wakuu,
Naamini sote tunaendelea kufuatilia kwa makini mgogoro wa Mpaka kati ya nchi yetu na majirani zetu Malawi. Tumesikia mengi hadi sasa. Yapo yaliyo dhahiri, matharani, Malawi hawako tayari kwa namna yoyote ile kubadili mtazamo wao, nasi kwa upande wetu hatuko tayari kwa lolote lililo kinyume na msimamo tulionao kwamba mpaka wa ziwa Nyasa uko katikati ya ziwa tajwa.
Japo kwa sasa, pande zote mbili zinadai mazungumzo ya maelewano ndio dawa (sijasikia yanafanyika wapi), yawezekana kabisa mazungumzo hayo yasizae matunda. Wawakilishi wa Malawi watapata wapi ujasiri wa kurejea kwao na kutoa taarifa kwamba wameafiki, mpaka uko katikati ya ziwa? kadhalika wawakilishi wetu wataanzia wapi kutueleza kuwa wamekubali ziwa lote (isipokuwa ile sehemu ya Msumbiji) ni eneo la Malawi?
Matokeo ya kushindwa kuelewana yanaweza yakawa ni pamoja na kupelekana katika mahakama za kimataifa. Hata katika hilo bado kuna maswali, ni serikali gani itakuwa tayari kutoa taarifa kwa wananchi wake kwamba imeshindwa kesi mahakamani?
Kadhalika kushindwa kuelewana kutatupeleka katika lile ambalo wengi wamekwisha kulishabikia, ikiwa ni pamoja na viongozi wetu, yaani option ya vita. Hii ni option nzito na mbaya kabisa kwa mataifa mawili yenye uchumi duni. Yamkini Malawi au hata sisi, twaweza kusema tutashinda vita, lakini hilo haliondoi uwezekano kwamba matokeo yanaweza kuwa kinyume na matarajio. Aidha, japo upande wowote waweza shinda pambano la sasa, lakini ikawa ndio mwanzo wa vita itakayodumu vizazi na vizazi, hata ikawa kwamba mataifa haya mawili yatakuwa yametumbukia katika vilindi vya ufukara ambavyo kamwe hayatajinasua.
Katika mazingira haya, tunapaswa kufikiria option nyingine. Tutakapotafakari zaidi na kukumbuka kuwa si mmalawi wala si mtanzania aliyechora mstari huu unaotaka kutupeleka kubaya, tunaweza kusema; 'wait a minute', sisi ni ndugu, tena hilo halina ubishi, sisi sote tunaamini Afrika ni moja (rejea dhana ya panafricanism), kwa nini tusifute hiki kimstari cha mkoloni?
Tukikubaliana hilo, jambo baya la kugombea mpaka litatuzalia jambo zuri la kuingia sasa katika mazungumzo (no matter how long maungumzo hayo yatachukua) ya kuziunganisha jamhuri zetu mbili. Hatimaye tukawa na taifa moja; MUUNGANO WA MALAWI na TANZANIA.
Wawakilishi wetu kama mnanisoma tafadhali ...
Naamini sote tunaendelea kufuatilia kwa makini mgogoro wa Mpaka kati ya nchi yetu na majirani zetu Malawi. Tumesikia mengi hadi sasa. Yapo yaliyo dhahiri, matharani, Malawi hawako tayari kwa namna yoyote ile kubadili mtazamo wao, nasi kwa upande wetu hatuko tayari kwa lolote lililo kinyume na msimamo tulionao kwamba mpaka wa ziwa Nyasa uko katikati ya ziwa tajwa.
Japo kwa sasa, pande zote mbili zinadai mazungumzo ya maelewano ndio dawa (sijasikia yanafanyika wapi), yawezekana kabisa mazungumzo hayo yasizae matunda. Wawakilishi wa Malawi watapata wapi ujasiri wa kurejea kwao na kutoa taarifa kwamba wameafiki, mpaka uko katikati ya ziwa? kadhalika wawakilishi wetu wataanzia wapi kutueleza kuwa wamekubali ziwa lote (isipokuwa ile sehemu ya Msumbiji) ni eneo la Malawi?
Matokeo ya kushindwa kuelewana yanaweza yakawa ni pamoja na kupelekana katika mahakama za kimataifa. Hata katika hilo bado kuna maswali, ni serikali gani itakuwa tayari kutoa taarifa kwa wananchi wake kwamba imeshindwa kesi mahakamani?
Kadhalika kushindwa kuelewana kutatupeleka katika lile ambalo wengi wamekwisha kulishabikia, ikiwa ni pamoja na viongozi wetu, yaani option ya vita. Hii ni option nzito na mbaya kabisa kwa mataifa mawili yenye uchumi duni. Yamkini Malawi au hata sisi, twaweza kusema tutashinda vita, lakini hilo haliondoi uwezekano kwamba matokeo yanaweza kuwa kinyume na matarajio. Aidha, japo upande wowote waweza shinda pambano la sasa, lakini ikawa ndio mwanzo wa vita itakayodumu vizazi na vizazi, hata ikawa kwamba mataifa haya mawili yatakuwa yametumbukia katika vilindi vya ufukara ambavyo kamwe hayatajinasua.
Katika mazingira haya, tunapaswa kufikiria option nyingine. Tutakapotafakari zaidi na kukumbuka kuwa si mmalawi wala si mtanzania aliyechora mstari huu unaotaka kutupeleka kubaya, tunaweza kusema; 'wait a minute', sisi ni ndugu, tena hilo halina ubishi, sisi sote tunaamini Afrika ni moja (rejea dhana ya panafricanism), kwa nini tusifute hiki kimstari cha mkoloni?
Tukikubaliana hilo, jambo baya la kugombea mpaka litatuzalia jambo zuri la kuingia sasa katika mazungumzo (no matter how long maungumzo hayo yatachukua) ya kuziunganisha jamhuri zetu mbili. Hatimaye tukawa na taifa moja; MUUNGANO WA MALAWI na TANZANIA.
Wawakilishi wetu kama mnanisoma tafadhali ...