Mzalendo Mkuu
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 735
- 191
Ndugu Watanzania wenzangu. Jambo lisipingika kuwa hoja ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar imo mawazoni mwetu karibu kila siku. Mara Watanganyika wanalalamika na mara nyingi sana Wazanzibari wanalalamika zaidi. Wote hawa wanalalamika kwa kuwa kuna nchi mbili na kila moja anaona mwenzake anapata zaidi.
SULUHU YA MATATIZO YA MUUNGANO ni kuwa na NCHI MOJA TU badala ya nchi mbili kama ilivyo sasa. Kwa kuwa na nchi mbili tumesababisha yafuatayo:
1. Malalamiko yasiyoisha
2. Mgogoro wa CCM na CUF uliodumu kwa miaka zaidi ya 10 hivyo kuzorotesha maendeleo,
3. Kuwepo kwa Serikali mbili ya Muungano (ambayo ndani yake pia ziko mbili(Muungano na Tanganyika)) na ya Zanzibar
4. Uwepo wa viongozi wengi. Tunalazimika kuwa na Rais, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu bila sababu hivyo kuongeza gharama kubwa kwenye serikali.
5. Nchi moja kulazimika kuendesha mabunge mawili yaani lile la Muungano na lile Baraza la Wawakilishi.
6. Halama za kamati mbalimbali za pamoja za serikali na za vyama mbalimbali.
Kwa ujumla gharama ni kubwa sana zitokanazo na huu mfumo kuliko faida yake. Wakati tunaangali mchakato wa katibu mpya naomba pia tupate nafasi ya kuuangalia hili suala.
SULUHU YA MATATIZO YA MUUNGANO ni kuwa na NCHI MOJA TU badala ya nchi mbili kama ilivyo sasa. Kwa kuwa na nchi mbili tumesababisha yafuatayo:
1. Malalamiko yasiyoisha
2. Mgogoro wa CCM na CUF uliodumu kwa miaka zaidi ya 10 hivyo kuzorotesha maendeleo,
3. Kuwepo kwa Serikali mbili ya Muungano (ambayo ndani yake pia ziko mbili(Muungano na Tanganyika)) na ya Zanzibar
4. Uwepo wa viongozi wengi. Tunalazimika kuwa na Rais, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu bila sababu hivyo kuongeza gharama kubwa kwenye serikali.
5. Nchi moja kulazimika kuendesha mabunge mawili yaani lile la Muungano na lile Baraza la Wawakilishi.
6. Halama za kamati mbalimbali za pamoja za serikali na za vyama mbalimbali.
Kwa ujumla gharama ni kubwa sana zitokanazo na huu mfumo kuliko faida yake. Wakati tunaangali mchakato wa katibu mpya naomba pia tupate nafasi ya kuuangalia hili suala.