Muungano siyo tena mtaji wa kisiasa (political capital), bali ni shubiri kwa CCM

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
233
Tangu mfumo wa vyama vingi uanze miaka 20 iliyopita, siku zote CCM imekuwa ikiuchukulia Muungano kama mtaji wao wa kisiasa (political capital) dhidi ya vyama vya upinzani.


Walileweshwa na imani hiyo, wakajisahau kabisa kama vile wamekuwa wamejisahau katika mambo mengi tu kwa kuyachukulia for granted.

Hata hili la kuandika Katiba mpya CCM imekuwa inaona kwamba Muungano utawapa nyenzo fulani dhidi ya wapinzani katika azma yao ya kuweka Katiba wanayoitaka – na walianza kwa kusema Muungano usiguswe, na hapo hapo kuwapa Wazenji sauti kubwa katika Tume ya Katiba.


Eneo la watu 1.5m wamepewa ujumbe katika Tume hiyo sawasawa na eneo la watu zaidi ya milioni 40. Ni tofauti kabisa na uwakilishi wao katika Bunge la Muungano, ule wa kuchaguliwa – viti 50 kwa zaidi ya viti 200 kwa upande wa Bara.


Sasa mambo yanabadilika, na Muungano unaanza kuwa ni mzigo kwa CCM yaani liability na unaweza kabisa kuiangusha. Yanayotokea Zenji sasa hivi ni ishara ya hilo ninalolisema. CCM wanaanza kuuona Muungano kama shubiri kwake.

Naleta mada hii kwa ajili ya kujadiliwa.
 
Tangu mfumo wa vyama vingi uanze miaka 20 iliyopita, siku zote CCM imekuwa ikiuchukulia Muungano kama mtaji wao wa kisiasa (political capital) dhidi ya vyama vya upinzani.


Walileweshwa na imani hiyo, wakajisahau kabisa kama vile wamekuwa wamejisahau katika mambo mengi tu kwa kuyachukulia for granted.

Hata hili la kuandika Katiba mpya CCM imekuwa inaona kwamba Muungano utawapa nyenzo fulani dhidi ya wapinzani katika azma yao ya kuweka Katiba wanayoitaka – na walianza kwa kusema Muungano usiguswe, na hapo hapo kuwapa Wazenji sauti kubwa katika Tume ya Katiba.


Eneo la watu 1.5m wamepewa ujumbe katika Tume hiyo sawasawa na eneo la watu zaidi ya milioni 40. Ni tofauti kabisa na uwakilishi wao katika Bunge la Muungano, ule wa kuchaguliwa – viti 50 kwa zaidi ya viti 200 kwa upande wa Bara.


Sasa mambo yanabadilika, na Muungano unaanza kuwa ni mzigo kwa CCM yaani liability na unaweza kabisa kuiangusha. Yanayotokea Zenji sasa hivi ni ishara ya hilo ninalolisema. CCM wanaanza kuuona Muungano kama shubiri kwake.

Naleta mada hii kwa ajili ya kujadiliwa.

Nakubaliana nawe kabisa, CCM wamezoea vya ulaini walivyorithi wakati wa ujio wa vyama vingi. sasa wanatakiwa kufanya maamuzi magumu. natabiri hilo la Znz kama wakili-handle vibaya (na lazima watali-handle vibaya maana hawana busara) ndilo litakuwa pigo lao la mwisho na kuwatupa nje ya ulingo wa siasa. Tusubiri.

By the way nasikia askari polisi wengi walioko huko ni wa kutoka Bara. Hilo lanikumbusha mapema katika miaka ya 70 pale majeshi ya serikali ya Uingereza yalipopelekwa katika jimbo lake la Ireland ya Kaskazini na kuanzisha mapambano yaliyochukuwa miongo miwili baina ya serikali ya Uingereza na kikundi cha IRA.

Je inawezekana sasa hivi twashuhudia mwanzo wa "Ulsterization" ya Zanzibar?
 
Ninavyowafahamu CCM kwa mabavu, basi tutashuhudia kuongezeka kwa askari kule kutoka Bara, kitu ambacho kitazidisha hasira za Wazanzibari dhidi ya watawala wa Bara.
 
Back
Top Bottom