Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
hapa ndipo watanganyika wanapotufanya sie wapumbavu yaani sie wazanzibari tutashindwa kuishi huu si ukweli hata chembe.
wazanzibar tokea asili wanaishi kwa umoja mbali ya kuwa kuna tofauti ndogo ndogo ambazo nchi zote hazikosi, humu tulizungumza matatizo ya wachagga TRA ukweli ubaguzi upo na ukabila bara upo tena sana mbona hampigani, Zanzibar nnaamini tunaweza kujitawala na tukaishi vizuri tu.
mungu atuepushe na civil war leo na kesho. sisi tunaweza kujitawala na tulijitawala wenyewe kabla ya muungano nani alikuja kusuluhisha vita na wapi walikimbilia wakimbizi wa unguja na wapemba kabla ya muungano? nijibiwe masuala haya.
sisi tunataka fairness na si chengine sie tunaamini umoja ni nguvu na hata juzi kama ulifatilia kuhusu suala la Afrika mashariki nini walisema wazanzibari?
wanasema wao wanapenda umoja lakini iweje zanzibar isiwemo hali na wao ni nchi? pili ushiriki wetu kama taifa utakuwaje? wazanzibari daima hutaka fairness na si upendeleo.
au tuseme tuje bara kuomba uhuru tena baada ya kujikomboa 64.
kuna bwana mmoja alikuwa mkuu katika chama tawala alisema huyu hatumtaki kwa sababu baba yake alikuwa dalali wa zanzibar, si kwa maana anamchukua mwanzilishi wa taifa letu la hii hali tunayoenda nayo ni sawa kama ameiuza zanzibar.
na kama hujui historiya ya zanzibar tokea asili wazanzibari ni watu wa matani na maskhara
wapemba huitwa wapemba watu wabara walikuwa wakiitwa wa mrima wanyamwezi na mengi lakini hakupigwa mtu wala kuuliwa mtu waulize wazee wako.
na hii ndio maana hata sisi wazaramu kule zanzibar tulifka na sasa ni wazanzibari.
dhambi kuamini kuwa zanzibar ni waarabu au wapemba tu, tuko wengi wahindi, wamanyema, waburundi, wamalawi,wakenya, waganda na kocho kocho ya anuwai ya watu.
tumeishi na kuchanganyika kwa raha buheri.
ukweli udogo wa nchi yetu isiwe sababu ya kutubana na kutufirigisa
we kalaga bao tu!
niliyoyasema nimeyaona na hiyo ndio tathimini yangu.sasa,nawe una uhuru wa maoni! lakini tusifiche ukweli!huko hakutakalika!
Ni mawazo Tu!!....Ni Mitizamo tu!! ..Dunia Nzima watu wanaishi pamoja!! sasa sisi-Tunacho taka kukivunja Ni Nini?...
Mawazo Kwamba tumeungana!!?
vyo Vyo-te vile itakavyokua maana Itabaki palepale!!