Muungano au Ushirikiano wa Vyama vya Siasa Tanzania: Mungu aepushe mbali!

Albert Msando

JF-Expert Member
Nov 2, 2010
1,019
171
Haya ni mawazo yangu binafsi na hayawakilishi mawazo ya chama changu wala mtu mwingine yeyote.

Suala la CHADEMA, CUF, NCCR, TLP NA UDP kurushiana shutuma mbalimbali limekuwa jambo la kawaida. Kwa wengine ni jambo linalotia hofu. Hofu kubwa ni kwamba itakuwa vigumu kuishinda CCM.

Lakini wenye hofu hiyo hawaoni hofu kwamba muungano au ushirikiano huo pia unaweza kuwa mwisho wa upinzani hapa kwetu.

Hii hofu nyingine ina matokeo yale yale, ugumu wa kuishinda CCM.

Kwa hali ya siasa ya nchi kwetu kwa sasa, CCM itashindwa na chama kimoja chenye nguvu na sio muungano wa vyama vingi visivyo na nguvu badala yake vina wanasiasa (sio viongozi) wanaotafuta ulaji na kuganga njaa kwa kisingizio cha upinzani. Vyama hivyo pia vina wanasiasa ambao uelewa wao ni mdogo au umefunikwa na maslahi zaidi.

Hakuna haja wala sababu ya vyama vilivyo upinzani kuungana au kushirikiana katika hali ya sasa hivi. Huo utakuwa muungano au ushirikiano wa kinafiki sana. Upinzani utakuwa umepata pigo hilo likitokea.

Wote tumeshuhudia kwa muda mrefu mawazo na maono ya wanasiasa walioko upinzani. Kila mmoja anajifikiria yeye, halafu chama chake (ambacho ni yeye pia), halafu wanaomzunguka (ambao ni yeye pia) na mwisho watanzania ambao ni wafuasi wake (sio wananchi).

Sasa wanasiasa hawa wakiungana au kushirikiana nini kitatokea? Kenya vyama vya upinzani viliungana. Wakashinda uraisi. Baada ya hapo? Mpaka sasa hivi wanachojisifia ni Katiba mpya. Katiba ambayo kabla hawajashinda waliahidi itapatikana mapema mno. Watu walikufa na maelfu kukimbia makazi muungano wa upinzani ulipochukua. Kisa? Raila na Kibaki........wanasiasa wa upinzani zamani!

Kama ambavyo tunaona muungano wa Zanzibar na Tanganyika una matatizo yake, basi ni hivyo hivyo muungano au ushirikiano wa vyama vya siasa hapa kwetu. Wanasiasa wetu wana matatizo makubwa. Angalia wanayoyasema, wanavyoyasema na wanaowasemea.

Natoa mifano.

Toka tar. 31/10/10 hawa waliotajwa hapa chini wamesema nini hadharani kuhusu hali ya uchumi ya nchi na dunia, mipango ya ajira, mabadiliko ya hali ya hewa, uhusiano wa kimataifa, mfumo wa elimu nk. Hapa sizungumzii matamko yao kwamba hali ni mbaya au kupinga kwao ufisadi. Hilo wote tunajua na tunaona.

Wamezungumza nini kuhusu kubadilisha hali hiyo mbaya zaidi ya kuongea kwa ujumla? Nani anajua mawazo yao binafsi na uwezo wao kuhusu hayo? Tusirudishane kwenye ilani za vyama.

Augustine Lyatonga.....amesema nini?

John Cheyo..........amesema nini?

James Mbatia........amesema nini?

Ibrahim Lipumba.............amesema nini?

Freeman Mbowe...........amesema nini?

Tumekuwa na wanasiasa mabingwa wa kukosoa bila kutoa suluhisho. Wao kazi yao ni kuhudhuria misiba, sherehe za kitaifa, makongamano, kutoa pole wakati wa majanga, kutembelea watoto yatima na kutoa misaada ya baiskeli. Halafu anajiita kiongozi! Mpinzani!

Nchi inateketea, badala ya kusaidia isiishe yeye anasubiri acha iishe ili nije kuongoza mimi 2015. Nikisema cha kufanya sitaweza kuing'oa CCM. Haya ni makosa makubwa.

CUF wabaki kama CUF na CHADEMA wabaki kama CHADEMA. Kila kimoja kifanye kazi yake ya siasa. Ukweli wa nani bora utajulikana tu.

Mungu aepushe mbali mawazo ya Lipumba, Mbatia, Mrema, Cheyo na Mbowe kuungana au kushirikiana. Hata kwa kusoma hayo majina kwa pamoja utaona mwili unavyosisimka. Mungu atuepushe.

CCM itaondoka madarakani, na hii itakuwa mapema mno. Itatokea haraka na kwa ufanisi mkubwa. Hakuna jinsi wataondoka tu.

La msingi ni nani atachukua nafasi yao baada ya wao kuanguka? Sikubali hao wote kwa pamoja wachukue hiyo nafasi. CHADEMA watachukua. Kama chama na si kama umoja wa vyama.

Naamini.
 
kweli mh diwani mimi nakubaliana nawewe kwa logic ya survivor of the fitest the weak organism will die and the stonger one will survive CUF kwa ubinafsi na vision mbovu ya viongozi wake soon itakua kama NCCR,TLP au UDP Zitabaki kama kampuni tu kwani hata supotaz wake kule nchi jirani wameshaanza kutafakari juu ya chama mbadala baada ya CUF kuwaacha kwenye mataa nilikua ndoto niliyokua naiota kuwa iko siku CUF itakamata dola hasa Zenji imetoweka baada ya kuona walivyoingizwa chaka CDM isifungue milango kwa chama chochote maana sasa watizoo wanajua ipi orginal ipi fake
 
Huo ndiyo ukweli,Muungano wa vyama hauna tija,CDM msikubali kuungana na wahuni,bora tucherewe kuiondoa ccm,kuliko kuungana watu,cdm ikatumia nguvu nyingi,wao wakaja kung'ang'ania madaraka.CDM mnatosha kuiondoa ccm,
 
Nakubaliana na wewe kwa 100%. Chadema ndio chama pekee cha upinzani ambacho kinabeba maana halisi ya upinzani. Nafurahi maana wananchi wengi wameshakielewa! Ndio chama kinachoweza kuing'oa ccm madarakani bila kushirikiana na chama chochote. Vyama vingine wamechanganyikiwa maana vimekuwa vikibebwa na umaarufu wa watu na sasa unafifia kwa kasi! Kitendo cha wagombea wao wa urais kujitoa siku ya mwisho na kutamka kuisapoti ccm kinathibitisha kuchanganyikiwa kwao. Hiyo tu inawaondolea sifa ya upinzani na kuungana nao is a worst mistake tutakayokuwa tumefaeya Mungu ibariki Tanzania
 
Nami naamini ktk 'natural selection'. Watajichuja tu. Kumbuka nlisema tangu uchaguzi wa 2010,kuwa kuungana ni kuharibu Upinzani,bora Cuf,tlg,na Cdm vikae pekee. Nlitoa mfano wa cdm kuungana na Udp,chama ambacho kiko confined mkoa mmoja italeta maana gani?au kuungana na Cuf,ambayo Seif anaongoza serikali ya ccm italeta tija gani? Natumaini Cdm watajipambanua dhidi ya vibaraka wa ccm. Nakumbuka mwaka jana baada ya kuleta thread yangu Malaria Sugu,alipinga sana na akanifananisha na mbaguzi na mdini kwa kufananisha cdm na udini,nlimshangaa sana kwa mchango wa kichokozi ila wengi walielewa na baadae bungeni tumeona jinsi cdm ilivojipambanua. So far imani yangu iko cdm na cdm pekee. Mkuu tusubiri tuone maana cdm inaweza ikatuletea Uhuru wa Tanzania. Kumbuka tangu uhuru wa T'nyika,baadae wa Z'bar, hatuna uhuru mwingine uliopatikana na inawezekana watawala wanajua kuwa Tanzania haina uhuru na ivo masihara yote yanaletwa kwa kukosa uzalendo kwa kuongoza taifa "dhahania".
 
Wewe uamue kuungane na mtu kama Mrema, Lipumba, Mbatia, Cheyo kweli unagemea kitu hapo? kama si migogoro isiyo ya lazima.

Kati ya hawa hakuna hata mpinzani mmoja - wote wanacheza Timu B ya Sisiemu, sasa unaungana na timu B ili kuunda nini? Timu C ?
 
. Chadema ndio chama pekee cha upinzani ambacho kinabeba maana halisi ya upinzani.

Kwa kauli kama hizi, CDM ni chama cha ki-NAZI kinachoongozwa na madikteta wasioamini katika demokrasia, ni hatari kwa nchi hii kuongozwa na chama kinachoamini kuwa chenyewe tu ndio kina haki au kinastihili na wote wenye kupinga/kutofautiana na mawazo yao ni wasaliti..kwa ustawi wa taifa hili, demokrasia na amani hata kama CDM wakishinda uchaguzi kwa kura iwapo bado kitakuwa na misimamo hii ni heri nchi iongozwe na jeshi hadi hapo wananchi watakapo amua vinginevyo.
 
Kwa kauli kama hizi, CDM ni chama cha ki-NAZI kinachoongozwa na madikteta wasioamini katika demokrasia, ni hatari kwa nchi hii kuongozwa na chama kinachoamini kuwa chenyewe tu ndio kina haki au kinastihili na wote wenye kupinga/kutofautiana na mawazo yao ni wasaliti..kwa ustawi wa taifa hili, demokrasia na amani hata kama CDM wakishinda uchaguzi kwa kura iwapo bado kitakuwa na misimamo hii ni heri nchi iongozwe na jeshi hadi hapo wananchi watakapo amua vinginevyo.

kwa hiyo mgefurahi sana kama CHADEMA Kingeongozwa na viongozi wasio na misimamo? na mtakichukia zaidi kwa sababu viongozi wakuu wa CHAMA hiki kwa ghalama zozote hawanunuliki na hawawezi kamwe kukusaliti chama. Hiki ndicho kimekuwa kizingiti kikuu na watu wengi kusema wasemayo.

Sisi wananchi walalahoi tuna imani kubwa kabisa na Uongozi wa juu wa CHADEMA. Kwa taarifa tu ni kwamba hakuna mtu atakaa awe kiongozi wa CHADEMA kama msimano wake haueleweki kwa wanachama na wananchi kwa ujumla.

Sisi wananchi ndiyo tunajua chama gani kiko vipi? njooni na propaganda zenu juu ya CHADEMA kwamba ni chama cha udini, udikteta, ukabila na hata uhaini kama mlivyozusha majuzi lakini haki ya watu haidhurumiwi ki rahisi namna hiyo na sisi wananchi tumeerevuka kwa sasa, kama unabisha twende Tunduma, Biharamulo, Kahama na wilaya zingine uhakikishe maneno yangu.
 
Kwa kauli kama hizi, CDM ni chama cha ki-NAZI kinachoongozwa na madikteta wasioamini katika demokrasia, ni hatari kwa nchi hii kuongozwa na chama kinachoamini kuwa chenyewe tu ndio kina haki au kinastihili na wote wenye kupinga/kutofautiana na mawazo yao ni wasaliti..kwa ustawi wa taifa hili, demokrasia na amani hata kama CDM wakishinda uchaguzi kwa kura iwapo bado kitakuwa na misimamo hii ni heri nchi iongozwe na jeshi hadi hapo wananchi watakapo amua vinginevyo.

Jibu hoja yake usitoe upupu ni kweli kuwa CHADEMA ndio kimeonyesha upinzani kwa sasa wengine wote ni mamluki.
 
, CCM itashindwa na chama kimoja chenye nguvu na sio muungano wa vyama vingi visivyo na nguvu badala yake vina wanasiasa (sio viongozi) wanaotafuta ulaji na kuganga njaa kwa kisingizio cha upinzani. Vyama hivyo pia vina wanasiasa ambao uelewa wao ni mdogo au umefunikwa na maslahi zaidi.

Kuganga njaa na kutafuta ulaji ni tabia ya wanadamu wote haijalishi ni mwalimu, mwanasheria au mwanasiasa wa chama tawala au upinzani, kwa kuwa tabia hii ipo kila mahali kuna taratibu ya kudhibiti hawa watu. Hata ingekuwa ni kanisa bado kuna watu wangejiingiza kwa maslahi yao binafsi lakini watu hao hawafanyi kanisa lote kuonekana halina maana, Msando na wenzako mnaotaka kutuaminisha kuwa zaidi ya CDM hakuna chama cha siasa mngeacha kufanya hivyo kwani kwa kufanya hivyo mnakipa chama chenu jina baya na kwa wapenda demokrasia wanaanza kuona ubabe na uonevu wa CCM si kitu kwa ubaguzi na kashfa za CDM. Binafsi sikubaliani na wazo la kuunganisha vyama lakini sababu yangu ni moja tu, kufanya hivyo utaua demokrasia na si vinginevyo. Nakubaliana na wewe kuwa safari ya upinzani itakuwa imefikia mwisho iwapo vyama vikuu vitaungana lakini sikubaliani abadani kuwa eti kila kiongozi wa upinzani anajifikiria yeye(japo wapo wabinafsi). Mwisho nakupa rai wewe kama kiongozi wa CDM, lazima ujue unawajibu wa kujenga taswira ya chama chako, hata kama unatoa maoni yako binafsi lazima uwe makini kwani mara zote watu watayahusisha na imani/misimamo ya chama chako, sasa si vyema ukatufanya tuamini kuwa viongozi wa CDM wanaamini kuwa wao tu ndio wana haki miliki ya kuwa chama cha siasa hapa nchini.
 
Kwa kauli kama hizi, CDM ni chama cha ki-NAZI kinachoongozwa na madikteta wasioamini katika demokrasia, ni hatari kwa nchi hii kuongozwa na chama kinachoamini kuwa chenyewe tu ndio kina haki au kinastihili na wote wenye kupinga/kutofautiana na mawazo yao ni wasaliti..kwa ustawi wa taifa hili, demokrasia na amani hata kama CDM wakishinda uchaguzi kwa kura iwapo bado kitakuwa na misimamo hii ni heri nchi iongozwe na jeshi hadi hapo wananchi watakapo amua vinginevyo.

nasikitika kwamba umenielewa vibaya! Mimi sio kiongozi wala sina nafasi yoyote kwenye chama. Haya ni nawazo na maoni yangu. Ndio ninavyoamini! Naamini vyama vingine vya "upinzani" vimepoteza mwelekeo na chadema ndio chama pekee kinacho practice upinzani wa kweli. Kama kuna kingine unayonafasi ya kunishawishi!
 
Kwa taarifa tu ni kwamba hakuna mtu atakaa awe kiongozi wa CHADEMA kama msimano wake haueleweki kwa wanachama na wananchi kwa ujumla. .

Vipi Mh Zitto Zuber Kabwe, Naibu katibu Mkuu msimamo wake unaeleweka na wanachama?
 
nasikitika kwamba umenielewa vibaya! Mimi sio kiongozi wala sina nafasi yoyote kwenye chama. Haya ni nawazo na maoni yangu. Ndio ninavyoamini! Naamini vyama vingine vya "upinzani" vimepoteza mwelekeo na chadema ndio chama pekee kinacho practice upinzani wa kweli. Kama kuna kingine unayonafasi ya kunishawishi!

Sina haja ya kukushawishi mkuu ila ninaombi moja tu, toka nje ya box
 
Ninapoona Wanachadema wanasisitiza msimamo wa Chama chao kwa maneno yao wenyewe katika namna ya ushawishi wa hali ya juu namna hii, napata faraja kwa kweli.
 
Wabongo wanakiamini CDM,kuungana na vibaraka ni kuusaliti uma. So,CDM isimame yenyewe kama mwanzo,mbona 2naweza.
 
Nduka,

Sikumbuki kusema kwamba CDM pekee ndio chama cha upinzani. Hoja yangu ni kwamba vyama vya siasa kuungana ni makosa. Nimeuliza viongozi wa vyama vya upinzani wamesema nini toka tarehe 31/10/2011. Sikumbagua Mwenyekiti wa CDM, Freeman Mbowe. Kama kuna alichosema kiwekwe kama hakuna isemwe.

Jambo ambalo liko wazi ni kwamba CDM ni chama ambacho kimeendelea kujijenga na kuwa karibu na wananchi. Ni kweli demokrasia inahitaji kuwa na vyama vingi lakini haihitaji vyama hovyo.

Si sahihi kusema kwamba ni lazima niishi nikireflect chadema. Nitakuwa mdumavu wa mawazo. Ninachotakiwa kufanya ni kuwa na mawazo ambayo yatasaidia CDM kuendelea kukua kama chama. Katika hilo natakiwa kuhakikisha mawazo yangu hayapingani na Katiba ya chama na miongozo mingine. Naweza kupingana na mawazo ya mwanaCDM mwingine. Sio kosa na hali hiyo inasaidia chama kukua.
 
Jambo ambalo liko wazi ni kwamba CDM ni chama ambacho kimeendelea kujijenga na kuwa karibu na wananchi. Ni kweli demokrasia inahitaji kuwa na vyama vingi lakini haihitaji vyama hovyo..

Advocate, ugomvi wangu ni hapo kwenye red, tunatumia kipimo gani kuamua kuwa hiki ni chama hovyo? au tunakuwa tumesimamia wapi tunapoamua hivyo? Bado naona ni hatari kwa kiongozi wa chama ku lebell chama kingine kilicha sajiliwa kihalali kwa kufuata katiba na sheria za nchi cha hovyo, vipi kiongozi huyu akipewa nafasi ya kusajili/kufuta vyama kesho atavifanya nini vyama hivi? Na si lazima uandike mahala kuwa chama pekee ni CDM bali unaweza tu ku imply kwenye maandishi yako. Ni kweli kwa ushahidi wa kura CDM ndio chama kinachojijenga kwa sasa, lakini hii inavifanya vilivyobaki kuwa ni vya hovyo? kwani CDM imeshiriki uchaguzi mara ngapi? kabla ya matokeo haya tuliwahi kusikia vyama vingine vikii label CDM kama hivi? CDM wana hoja ya msingi kukataa kuungana na vya vingine lakini kuendelea kuhubiri kuwa vyama hivi ni mapandikizi, vimenunuliwa na wasaliti ni kujiongezea maadui wasi wa lazima. Kwani ugomvi upo wapi kama CDM wangesema kwa ustawi wa demokrasia hatuwezi kuunganisha vyama kwa kuwa kufanya hivyo kuharibu maana nzima ya vyama vingi. Lakini viongozi wa CDM(wewe ukiwa mmoja wao) mmeendelea kuvitukana vya vingine na kuviita majina kitu kinachotupa wasiwasi kama ni kweli CDM inaamini ktk demokrasia.
 

Nimesoma na kukusoma mimi naomba wana JF wasome msemo huo. wakuweza kutafsiri atakuwa ametenda wema.


"I offer my opponents a bargain: if they will stop telling lies about us, I will stop telling the truth about them." ~Adlai Stevenson, campaign speech, 1952
 
Nduka,

Chama hovyo si tusi. Kwani mtu akisema fulani ni hovyo anatumia kigezo gani? Matendo ya chama cha siasa ndiyo yanaweza kutumika kama kigezo cha uhovyo. Inawezekana vilivyopo sio hovyo lakini haizuii sisi kusema kwamba demokrasia haihitaji vyama hovyo.

Inawezekana kutokana na mada ilipoanzia na nafasi yangu ikawa vigumu kueleweka kwamba sina lengo la kuvitukana au kuvidharau vyama vingine bali kuelezea hali halisi ya siasa zetu.
 
Back
Top Bottom