Muundo wa Muungano: Tanganyika tunataka 'Serikali moja, nchi moja, taifa moja'!

Mimi nikokinyume na wadau wengi ambao wanashadadia serikali mbili kwa tatu. Mimi ninasema kama nchi ni moja basi hata serikali iwe moja tu ya jamhuri ya muungano wa Tanzania. Rais awe mmoja na pasiwe na cheo cha makamu wa rais badala yake waziri mkuu atoke upande wa pili wa muungano ambao haukutoa rais. Rais atawale miaka 8 kwa mhula wa 4 by 2, kisha upande wa pili wa muungano ndio uwe na haki ya kutoa rais. Baraza la mawaziri liwe 2/3 kwa 1/3 Tanganyika wawe 2/3 na Zenji wawe 1/3 ya mawaziri wote. Bunge liwe moja tu la muungano. Mikoa iwe majimbo na Zenji iwe na majimbo pia. Jeshi liwe moja na pasiwe na mambo ya muungano na yasiyo ya muungano yote yawe ya muungano maana nchi ni moja yenye serikali moja. Ni mtazamo wangu japo unaweza kubezwa na watu kadhaa.

Hii ndiyo ingekuwa suluhisho la kero za muungano lakini si rahisi kukubalika kwa sasa. Mimi ningeshauri serikali moja iwe moja ya ajenda ya kitaifa kwa miaka ijayo! Lakini kwa sasa serikali 3 hazikwepeki!

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Serikali 3 au 2 zinapigiwa chepuo na makundi mawili tofauti. Hoja ni nyingi lakini lililo kuu hapa kwa maoni yangu si uzalendo bali ubinafsi na uroho wa madaraka. Muungano wa kweli ni serikali moja ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mambo mengine yabaki kwenye historia na makumbusho. Tofauti ya hapo siioni Tanzania miaka 50 ijayo
 
Hilo wazo kukubalika ni ngumu sana la seikali moja. Zenji ni kichwa ngumu hawatakubali na tanganyika wanawaogopa lakini pia wana maslahi na serikali mbili ndo maana hawana jeuri ya ku adapt moja... wazo langu mmi nathani haliko tofauti sana na la watanzania walio wengina ni serikali tatu kamatume ilivyo pendekeza kutoka kwa maoni ya watanzania. La siivyo kwa hizo erikali mbili ccm walizo zikomalia mbaka mishipa imewavimba tutapata katiba ya ccm
 
Tatizo la serekali tatu bado Tanganyika italazimika kuchangia zaidi. Kitu ambacho nashindwa kuelewa ni kwanini Mtanganyika atake muungano na Zanzibar. Sijui faida yoyote ya muungano kwa Mtanganyika. Kinachotakiwa ni kila mtu aende kivyake. Ikishindikana basi angalau kuwe na serekali ya Tanganyika kwanza.
 
Hii nchi imejaa viongozi waoga ambao hawawezi kusimamia maamuzi yenye manufaa kwa wananchi hasa kama maamuzi hayo yanahatarisha maslahi yao. Serikali moja ndiyo inaweza kuwa suluhisho la nchi hii kinyume cha hapo tuuvunje muungano!!
 
Hakuna ubishi kuwa serikali moja is the best kwa wananchi wote kutoka pande zote za muungano lakini ni viongozi hawapendi kwa ubinafsi wao kama ilivyodhihirika miaka 50 ya katiba ya muungano wa serikali mbili ambao kwa vurugu yake huko tutokako ni unafiki kuzungumzia serikali moja na hata serikali mbili nchi moja. Muungano wa kweli ukubalike na wananchi husika na kwa nguvu ya dola. Tuwe na Muungano kwa ajili ya wananchi na siyo kwa ajili ya viongizi au wananchi kwa ajili ya muungano kwa nguvu ya sola au Kundi fulani.
 
Idadi ya serikali inakuzwa na wanasiasa kulinda masilahi yao lakini hazitusaidii kutatua kero zetu RAIA was kawaida.
 
Umenisoma bila ya hivo, ukivunjika muungano Zanzibar tunajipanga miaka mitano then tunai Dar es salam, mtwara, tanga, bagamoyo, mombasa kuwa ni maeneo halali ya Zanzibar kabla ya kuja mjerumani Tanganyika, uaije ukashanga wa zenji watakapo kuja na full document

Mtakuwa mmetoa sababu ya kuwa subjugated na watanganyika! Mtahamishwa na kusambazwa Tanganyika yote tangu Kagera to Ruvuma, Dar to Kigoma mpotelee humo. Then Znzbr watapelekwa wabara tofauti wakaifanyie reform ya kila kitu!

NI SERIKALI MOJA au "LET THEM GO"! CHADEMA NDIO ADUI MKUBWA WA SERIKALI MOJA. CCM ni adui namba 2.
Ni upuuzi na ulimbukeni kila kona.
 
Mimi naafiki serikali moja na tena Raisi awe Kutoka ZANZIBAR MAwaziri wote watoke Zanzibar Mkuu waMajeshi atoke Zanzibar MaBalozi wote watoke Zanzibar Mkuu wa Usalama Atoke Zanzibar Mkuu Wa Polisi atoke Zanzibar Na Nyazifa zote KUbwa Kubwa zishikwe na Watu Kutoka Zanzibar hapo ndipo tutakapo endeleza Umoja wetu na Amani tupinge serikali TAtu ni kuvunja Umoja wetu na kuongeza Gharama za bure wananchi tusikubali kamwe kama kuna pesa za ziada Basi Zipelekwe ZAnzibar zikandeleze muundo mbinu.
 
Mimi naafiki serikali moja na tena Raisi awe Kutoka ZANZIBAR MAwaziri wote watoke Zanzibar Mkuu waMajeshi atoke Zanzibar MaBalozi wote watoke Zanzibar Mkuu wa Usalama Atoke Zanzibar Mkuu Wa Polisi atoke Zanzibar Na Nyazifa zote KUbwa Kubwa zishikwe na Watu Kutoka Zanzibar hapo ndipo tutakapo endeleza Umoja wetu na Amani tupinge serikali TAtu ni kuvunja Umoja wetu na kuongeza Gharama za bure wananchi tusikubali kamwe kama kuna pesa za ziada Basi Zipelekwe ZAnzibar zikandeleze muundo mbinu.

wakubali wapi manyang'au hao.

wafanya makao makuu ya serikali miaka hii 50 ijayo zanizbar na mambo yote ya nchi yapangwe zanziba kama sasa ilivyo kwa watanganyika
 
Back
Top Bottom