ThinkPad
JF-Expert Member
- Apr 11, 2008
- 1,844
- 232
Allah (s.w.) ameumba ulimwengu pasipo chochote
Kutokana na ushahidi mwingi kutoka kwa wanasayansi, maelezo ya tasnifu (Thesis) juu ya ulimwengu usio na mwisho yakatupwa kwenye kapu la historia ya mawazo ya kisayansi. Hata hivyo swali muhimu lililojitokeza ni kuwa ni kitu gani kilichokuwepo kabla ya Big Bang? Nguvu gani iliyosababisha mlipuko huo mkubwa ambao ulitengeneza ulimwengu ambao haukuwapo?
Kuna jibu moja tu kwa swali hilo, kilichokuwepo kabla ya mlipuko wa Big Bang. Ni yule Mwenye Nguvu, Mwenye uwezo, aliyeumba dunia na vilivyomo katika mpangilio mahsusi, Allah (s.w). Wanasayansi wengi, wawe waumini au vinginevyo, wanalazimika kukubali ukweli huu. Mwanafalsafa mmoja katika wanaokana uumbaji Anthony Flew alisema:
Ni vizuri kukiri rohoni ingawa ni kuchungu. Kwa hivyo naanza kukiri kuwa wanaomkana Mungu wanadhalilishwa na makubaliano haya ya muda ya nadharia ya anga. Kwani inaonekana wanaanga wanatoa ushahidi wa kisayansi ambao Mtakatifu Thomas alikubali kuwa hauwezi kupatiwa ushahidi wa kifalsafa, kwa kuwa ulimwengu ulikuwa na mwanzo. Iwapo ulimwengu unaweza ukafikiriwa kuwa siyo tu hauna mwisho bali hauna mwanzo, inabaki wazi kuwa kuwapo kwake na vilivyomo ndiyo maelezo halisi. Ijapokuwa inaonekana ukweli lakini si rahisi kukubaliana moja kwa moja kwa sura ya hadith za Big Bang.
Kuna watu kama mwanafizikia Mwingereza H.P. Lipson wanaokiri kuwa wanalazimika kukubaliana na nadharia ya Big Bang watake, wasitake:
Kama maada hai husababishwa na migongano ya atomu, nguvu za asili, jinsi gani itakavyokuwa? Nafikiri, lazima tukubali kuwa maelezo ya kukubalika ni kuwa kuna Muumba.
Najua haipendezi kusema hivyo kwa wanafizikia, na hivyo hivyo kwangu mwenyewe lakini tusikatae kusema hivyo iwapo majaribio ya kisayansi yanaonesha hivyo.
Kwa kujumuisha, sayansi imeonesha hivyo watake wasitake wasiomkubali Mungu itawalazimu kukubali. Maada na muda umeumbwa na Muumba Mwenye Nguvu ambaye ameumba ardhi, mbingu na vilivyomo kati yake: Allah (s.w) muweza.
Ni Allah (s.w.) aliyeumba mbingu sana na dunia katika idadi sawa, akaiamrisha zote, ili mfahamu kuwa Allah (s.w) ana nguvu kwa kila kitu na ni Allah (s.w.) ameishikilia vyote kwa elimu yake.
Surat at-Talaq: 12
Una hakika kuwa allah ndio aliye umba Dunia?
Manaa naona unachanganya elimu na Dini hapa hata sikuelewi kama unaleta elimu uichanganue ila usichanganye elimu na dini.
uniambie kama una hakika kuwa allah ndio aliye umba dunia.