Muswada Katiba Mpya, Hoja ya Muungano moto Zanzibar!

mzalendo_abdallah-waziri-564x272.jpg

Salma Said,
Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Othman Masoud Othman alisema …marekebisho ya kumi yamegusa katiba ya muungano. Zanzibar kurekebisha makosa imekuwa ni kosa? Bunge halina uwezo kutunga ya sheria ya kuweza kutunga katiba nyengine. Articles of the union ndio iliyozaa katiba hii ya muungano. Turudi katika mapatano ya muungano, tushauriane na tukubalinae. Madaraka hayo yametoka wapi ndani ya katiba hii?
Bunge la jamhuri halina uwezo wa kutunga sheria ya katiba hili ni jambo la msingi si dhani Zanziba na watu wake kama watakubali kuvunja katiba.
Wakitoa maoni yao wazanzibari leo wameukataa mswaada wa kuundwa kwa kamisheni ya kukusanya maoni kuhusu kutungwa katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Visiwani Zanzibar kwa madai kwamba serikali ya Mapinduzi Zanzibar haijashirikishwa katika uandaaji.
Wazanzibari hao wamesema suala la kutengenezwa mswaada wa kuundwa katiba mpya ya Tanzania limefayika bila ya kuzingatia upande wa Zanzibar ambao ni mshirika wake muhimu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania.
Wananchi hao wamesema utaratibu uliiotumika katika mswaada wa katiba mpya haukuwashirikisha wanzibari na badala yake umefanyika kwa upande mmoja wa jamhuri ya muungano wa Tanzania jambo ambalo sio sahihi kwa kuwa bila ya kuwepo Zanzibar kusingekuwepo na Tanzania.
Maoni hayo yametolewa jana na wananchi mbali mbali wakiwemo mawaziri, makatibu wakuu, viongozi wa dini na wananchi mbali mbali katika mdahalo wa wazi wa kukusanya maoni katika ukumbi wa Hoteli ya Bwawani Mjini Zanzibar juu ya utoaji wa maoni ya kuhusu mswaada wa kuundwa kwa kamisheni ya kukusanya maoni kuhusu kutungwa kwa katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Zanzibar.
Akichangia mjdala huo Mwakilishi wa Jimbo la kwamtipura Hamza Hassan Juma amesema mswada wa marekebisho ya katiba ya Muungano una mapungufu mengi yakiwemo kutoshirikishwa kwa serikali ya Zanzibar.
Hamza alifahamisha kuwa Serikali ya Zanzibar haikushirikishwa kikamilifu ili kutoa maoni yake na wala haukupelekwa katika baraza la wawakilishi kupata maoni ya baraza hivyo haukustahiki kupelekwa Bungeni kujadiliwa kwani umekosa ridhaa za pande mbili.
“Mswada huo ni vyema kurudi Serikalini na ukafanyiwe marekebisho na badala yake upelekwe katika Baraza la Wawakilsihi ili kujadiliwa ili upate ridhaa ya nchi mbili zilizoungana”alisema Mwakilishi Hamza.
Kwa upande wake mjumbe kutoka chama cha mapinduzi (CCM) Ali Mwinyi Msuko alisema wanasheria wa Zanzibar wakae na wanasheria wa Tanzania bara kuupitia upya mswada huo na hakuna sababu ya kuharakisha muswada huo kwenda bungeni rais Nyerere na Karume walikubaliana katika Muungao huo na kwa sasa nchi mbili hizi zikubaliane.
Alishauri kwamba mswada huo urudi tena Bungeni na ufuate taratibu kwa kisheria na kwa sasa hakuna sababu yeyote ya kujadiliwa huku akitoa mfano kwamba kujadili mswada huo ni sawa na kutwanga maji kinuni. Na mswaada huo haukuzingatia hali halisi ya Zanzibar…vipi ifanyike ijumaa wakati 98% ni Waislamu wanataka kusali? Hauna haja ya kurakishwa kupelekwa June.


Mjadala wa katiba – Zanzibar | MZALENDO.NET




Sauti za wachangiaji:
Ali Omar Juma:

Awadh Ali Said:

#gallery-1 { MARGIN: auto}#gallery-1 .gallery-item { TEXT-ALIGN: center; MARGIN-TOP: 10px; WIDTH: 33%; FLOAT: left}#gallery-1 IMG { BORDER-BOTTOM: #cfcfcf 2px solid; BORDER-LEFT: #cfcfcf 2px solid; BORDER-TOP: #cfcfcf 2px solid; BORDER-RIGHT: #cfcfcf 2px solid}#gallery-1 .gallery-caption { MARGIN-LEFT: 0px}
Mwanasheria Mkuu wa serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Othman Masoud Othman alisema ni kweli marekebisho ya 10 ya katiba ya Zanzibar yamegusa Muungano ingawa katika katiba hiyo kifungu cha 17 kimempa uwezo rais wa Zanzibar kuwa na uhuru wa kuteuwa wakuu wa mikoa na kukata mipaka ya mikoa bila ya kushauriana na rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jambo ambalo Zanzibar wamerekebisha huku akihoji jee kufnaya hivyo kurekebisha makosa ni ni vibaya au ni kosa hata wengine hawamaki?.



 
ALI YUSSUF in Zanzibar,
A PUBLIC forum on the union constitutional draft Bill was on Friday rejected by majority Zanzibaris including senior ministers pushing for a fresh start because “legal procedures concerning union bills have not been followed as par the current Zanzibar and union constitutions.”
Participants including ministers and other executives, leaders from political parties, and ordinary civilians gathered at the Salama Hall, Bwawani Hotel in the Stone Town to give their views on the constitution, but many said:
“The bill has been rushed, and the required procedures on issues concerning bills to be applied in Zanzibar have been violated.”
Zanzibar’s Attorney General (AG) Mr Othman Masoud told the forum, “Our intention is not to undermine the process, but it is obvious, legal procedures have been violated. We ask for our suggestion to be considered.”
The Minister of Constitution and Legal affairs, Mr Abubakari Khamis Bakari, said that it was unacceptable, not considering Zanzibar interest in the draft bill and also not involving Zanzibar.
According to lawyers in Zanzibar, both Zanzibar and union constitutions say that any bill that is intended to be extended to Zanzibar, should get the consent of the Zanzibar House of Representatives. It emerged at the forum that Zanzibar authorities and members of the House were not consulted prior to preparation of the Bill.”
Mr Hamza Hassan Juma (CCM- Kwamtipura) complained against the use of English, while the majority Zanzibaris could not understand the foreign language.
Mr Salum Bimani, CUF party’s director for information, threatened that should Zanzibar’s interests be ignored, he would mobilize Zanzibaris to reject the proposed constitution at the time of referendum.
Mr Mansour Yussuf Himid, Zanzibar Minister of Agriculture and Natural Resources, said: “This is the right time to press for our (Zanzibar) interest.
We may not have other time. Let us join forces with one voice to make sure Zanzibar’s interests including resolving problems in the Union are considered in the new constitution.”
Prior to the forum chaired by Ms Samia Suluhu Hassan, the State Minister (Union affairs), Mr Samuel Sitta made a presentation on the Union Constitution draft bill, emphasizing that the bill was a process to write the bill. “It is not yet the constitution bill.”
 
Najuwa huu ni mwiba kwa wengi humu who are torn between dharau zao na ukweli wa jambo hili. umefika wakati wote waelewe kuwa Wazanzibari sio kama mnavyowafikiria.
Big Up zanzibaris!
 
Kwani baraza la mawaziri la Tanzania haliwahusu Wazanzibari? Haya ndiyo matatizo yanayotakiwa kuwekwa sawa katika katiba mpya.Huwezi kuwa na serikali ya Jamhuri ya Muungano yenye mawaziri kutoka pande zote, baraza la mawaziri lipitishe jambo halafu useme upande mmoja haujashirikishwa.
Hao mwaziri na wabunge wa JMT kutoka zanzibar wanafanya nini kama siyo kuwawakilisha?


Unazungumzia kuwakilisha wakati wa bara wanahudhuria kwa nafasi zao. Hivyo kuwakilisha na kuhudhuria mwenyewe ni sawa kwako?
Hebu jiulize Katiba iwapo inazungumzia vipengele vyote vya maisha ya wananchi kwanini Zanzibar iwakilishwe kwenye mambo baadhi ( kwa kuchukulia nafasi walizonazo kwenye hiyo serikali ya Tanzania)huku Tanganyika mawaziri wa wizara zote wahudhurie? Kwako huko ndiko unakooona kunafaa? Kama ni hivyo basi waachieni CCM wawe wawakilishi wenu huko Tanganyika!
 
Nafikiri si kweli kwamba ilivyo sasa muungano ni vigumu kuanguka, hapana tungekuwa na serikali moja hapo sawa lakini mbiliii. Kwa muundo ulivyo leo Zanzibar wanaweza tangaza kujiondoa na kusema tangu leo muungano kwishaaa.

Mie kweli nawashangaa wazanzibar wanalalamika wakati uwezo uko ndani yao, Kwa waTanganyika ndo kugumu ku declare kuvunja muungano maana serikali yao ni virtual.
Angalia, makamu wa Rais wa serikali ya Muungano akiwa mzanzibari , waziri wa ulinzi mzanzibari, waziri wa mambo ya ndani mzanzibari nk, unafikiri hawa watadeclare kuvunja muungano wakale wapi?? Hata maalim self akiwa rais wa muungano hatokubali kuvunja muungano akale wapi?

Serikali ya mapinduzi iliyo na wazanzibari kwa asilimia 100% ndo yakuvunja muungano, utawashangaa nao wanajumuika kulalamika wakati guts zimo kitandani mwao zakufanya watakalo.


Kwani ndugu yangu vuguvugu hili lilianza lini? Wazanzibari si watu wa fujo lakini ukifuatilia utaona kuwa ni watu makini wanaotaka wamalize njia zote za kawaida kabla ya kufikia hatua unazotaka wewe> Hao mawaziri ni wawili tu na huyo mmoja ni kizazi cha pande mbili anaweza kuamuwa kumojawapo, lakini hao si kiwazo kwa mapambano ya haki.
 
Siungi mkono zanzibar kuondoka kwenye muungano ila nasema kuwa kama hawa jamaa wana kero zinazowasumbua kitu ambacho naju kipo basi ni vizuri sana zijadiliwe mapema sana. Zanzibar ni sehemu muhimu sana kwetu..
Mkuu.
Tufungue macho na sisi hapo nilipo-highlight nyekundu.
Kivipi?
Sisi tunaiona kuwa ni toto tundu tu.
Tunawabeba na hawana shukrani. wanatutia hasara tu.
Na hatuna serikali ya Tanganyika ndani ya Muungano kama wao.

Mkuu..vipi Zanzibar inakuwa ni sehemu muhimu sana kwetu?
Zanzibar yenyewe hata haina ukubwa wa jimbo la Ubungo la Mnyika!!!

Tueleweshe umuhimu wa Zanzibar kwa Tanganyika, Mkuu.
Natanguliza shukrani zangu kwako.
 
Mkuu.
Tufungue macho na sisi hapo nilipo-highlight nyekundu.
Kivipi?
Sisi tunaiona kuwa ni toto tundu tu.
Tunawabeba na hawana shukrani. wanatutia hasara tu.
Na hatuna serikali ya Tanganyika ndani ya Muungano kama wao.

Mkuu..vipi Zanzibar inakuwa ni sehemu muhimu sana kwetu?
Zanzibar yenyewe hata haina ukubwa wa jimbo la Ubungo la Mnyika!!!

Tueleweshe umuhimu wa Zanzibar kwa Tanganyika, Mkuu.
Natanguliza shukrani zangu kwako.

Kama mtoto mchanga aliyezaliwa leo anakuwa muhimu kwa wazazi wake atakosaje kuwa muhimu sana mtoto wa std one!
 
KONGAMANO la wazi lililoitishwa ili kujadili rasimu ya Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kufanyika mjini hapa Ijumaa, lilimazika kwa wadau wengi wakiwemo Mawaziri wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa, wakitaka rasimu hiyo kuandaliwa upya. Wadau hao walipinga vipengele vya rasimu hiyo kwa kile walichoeleza kuwa ni kutaka kuandaliwa upya kwa vipengele vya kisheria vinavyohusu masuala ya kimuungano havijafuatwa kama inavyotakiwa kama ilivyo katika Katiba ya sasa iliyounda Muungano.

Washiriki wa kongamano hilo wakiwemo mawaziri, maofisa waandamizi wa serikali, viongozi wa vyama vya siasa na wananchi wa kawaida waliokusanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Bwawani iliyopo katika eneo la Stone Town walipata nafasi ya kutoa maoni yao huku wengi wakisema rasimu hiyo imeandaliwa kwa kukurupuka na kwamba masuala ya msingi yanayoihusu Zanzibar hayajazingatiwa.

Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar (AG) Othman Masoud aliwaambia washiriki wa kongamano hilo, “Si lengo letu kutaka kubeza mchakato mzima wa maandalizi ya Katiba mpya, lakini ni ukweli ulio wazi kwamba vipengele vya kisheria vingi vimekiukwa, ombi letu ni kutaka kuona mapendekezo yetu yanafanyiwa kazi.”

Waziri wa Katiba na Mambo ya Sheria, Abubakar Khamis Bakari alisema mapendekezo hayo ya rasimu ya Katiba mpya hayakubaliki kwa vile hayajazingatia haki na maslahi ya kimsingi ya Zanzibar na pia hayaijumuisha Zanzibar kwa upana unaotakiwa.

Kwa mujibu wa wanasheria wa Zanzibar, Katiba ya Zanzibar na ile ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zinaeleza kwamba mswaada wowote ambao unalenga kuandaliwa na kutekelezwa Zanzibar ni lazima upate baraka za Baraza la Wawakilishi. Wanasema rasimu hiyo haiojawashiriki Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na mamlaka nyingine zinazohusika.

Mwakilishi wa Kwamtipura, Hamza Hassan Juma (CCM) alilalamikia matumizi ya lugha ya Kiingereza katika uandaaji wa rasimu hiyo wakati wananchi wengi wa Zanzibar hawajui lugha hiyo. Waziri wa Kilimo na Maliasili, Mansour Yussuf Himid, alisema ni wakati muafaka sasa kwa Wazanzibar kupigania maslahi yao. “Ni wakati muafaka sasa kwa wazanzibar wote kuunganisha nguvu zetu kwa pamoja na kushikamana ili kuhakikisha kuwa tunalinda maslahi na haki za wananchi wa Zanzibar.”

Kongamano hilo lilikuwa chini ya uenyekiti wa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano, Samia Suluhu Hassan, na Waziri wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, aliwasilisha mada kuhusu maandalizi ya uundwaji wa Katiba mpya ambapo alisisitiza kwamba yaliyopo ni mapendekezo na si Muswada kamili wa Katiba mpya.

Source: Habari Leo
 
Kama mtoto mchanga aliyezaliwa leo anakuwa muhimu kwa wazazi wake atakosaje kuwa muhimu sana mtoto wa std one!
Chamajani.

Hapa ndio umetusaidia kuelewa umuhimu wa Zanzibar kwa Tanganyika au umetuzidishia utata?
Kama una ufafanuzi wa kina utandaze hapa mkuu.
Kama una maelezo ya kauli, "Zanzibar ni muhimu sana kwetu" basi tuekee hapa.

Au ndio unataka kuturushia changa la macho, mkuu? Ili tusifahamu kitu?
 
Mswada ulivyotoa tahadhari ya kutogusia mambo ya Muungano hilo laweza leta high temberature kwa wazenji, wao masuala ya kitaifa wanashikana sana.
 
Ndugu zetu wa Visiwani, muda wa sisi wananchi kutetea haki ya kuunda katiba mpya na kuweka sawa zaidi masuala yooote ya muungano bila kugilibiwa na watawala wala kuzuiliwa na tofauti ndogo ndogo za kiitikadi ni huu hapa na tukiupoteza basi vijana tujilaumu wenyewe miaka mingi ijayo.

Tuhakikishe tumeutumia vema sasa hivi kwa kila mmoja wetu kuelimisha wengine walau 3 kila siku juu ya haki yetu kikatiba jukumu letu kujiundia katiba bila udalali wala bughudha za watawala.
 
Huwezi kujuwa wanataka nini kwasababu wakati wewe mwenyewe hujuwi kitu gani kilichopo!


si kikubwa asilani sisi tunachokitaka

tukitakacho ni justice, hicho ndio tukitakacho. na kwa muda mrefu ndugu zetu hicho hawataki kututendea, wao wanapenda mambo ya ujanja ujanja na uonevu

wazanzibari walivumilia muda mrefu na wamechoka, na kwa muda mrefu pia wamejipanga na kwa hakika wanastahiki pongezi maana wameweza kuwaunganisha wazanzibari wote juu ya haki zao

leo mzanzibari popote alipo wa rangi yoyote, ukimuuliza juu ya muungano mawazo yao hayapishani


na kwa ukweli hapa sasa ndio patamu, maana bubu akiamua kusema watastaaajabu wanenao
 
  • Wasema imeegemea upande mmoja wa Muungano
  • Wahoji kutoshirikishwa SMZ katika maandalizi yake
  • Wasema haiwahusu kwa kuzuiwa kujadili Muungano
  • Wajipanga kuunda Kamati yao kukusanya maoni hayo
  • Walazimisha Mkataba wa Muungano kuwa msingi

WANANCHI wa Zanzibar wameipinga rasimu ya uandaaji wa Tume itayoandaa Katiba mpya ya Muungano, wakidai haiko kihalali na pindipo serikali ya Muungano ikiifisha Bungeni itakuwa imekiuka Katiba ya Muungano. Maoni hayo waliyatoa jana mbele ya Kamati ya Katiba na Sheria ya Bunge la Jamhuri ya Muungano, inayoratibu maoni ya kuweza kupatikana mswaada wa sheria wa kuweza kukusanya maoni ya wananchi juu ya mabadiliko ya Katiba ya Tanzania, mjadala ambao umefanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Bwawani Mjini Zanzibar. Mjadala huo ambao uliwashirikisha viongozi wa serikali ya SMZ, vyama vya siasa na Jumuiya binafsi, wameipinga rasimu hiyo huku wakionekana kuchukizwa nayo kutokana na sehemu kubwa ya mjadala huo ukichangiwa kwa jazba na maoni makali.

Kila kiongozi aliyepata fursa ya kutoa maoni alitamka wazi wazi kuikataa rasimu hiyo na kutaka irudishwe ilipotoka kutokana na kushindwa kuishirikisha Zanzibar kikamilifu katika maandalizi yake kiasi ambacho haina matakwa ya yanayohusu Zanzibar na Rais wa Zanzibar hakuwekwa kama ni mtu muhimu katika uundaji wa Tume hiyo.

Othman Masoud Othman (Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar)

Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Othman Masoud, akitoa mchango wake alisema kuwa Bunge liliopo halina uwezo wa kuunda Bunge la katiba, huku akitaka aonyeshwe madaraka hayo yako ibara gani. Alisema sheria ziliopo zinaelekeza ni namna vilivyotowa uwezo katika kifungu cha 68 ambacho kinatoa mamlaka ya kufanyika kwa marekebisho ya Katiba na sio kazi kuunda sheria. Alisema jambo ambalo walitakiwa kulifanya kama serikali katika kuunda sheria hiyo walitakiwa kuwepo mapatano kati ya serikali mbili na kinyume cha hivyo watakuwa wanavunja Katiba ya Muungano.


Hassan Nassor Moyo

Akitoa mchango wake alisema wakati umefika hivi sasa wa serikali ya Muungano kukubali kuwapo kwa mabadiliko katika mambo ya Muungano na kuacha kung’anag’ania mambo waliyozoweya. Alisema mambo waliyofanya miaka iliopita wakati wa kina Lusinde, Hassan Moyo na Sitta, hivi sasa hayapo tena na wasizuie kuwapo kwa mabadiliko kwani kazi yao imekwisha na watafanya makosa kuzuia mambo ya Muungano Wazanzibari waasiyajadili katika katika mpya.

“Haiwezekani hata kidogo wapewe nafasi waseme kwani hili nalisema ndani ya moyo wangu Nyerere alikuja Zanzibar na karatasi ina mambo 11, mimi nilikuwa Waziri wa Sheria alinipa faili na hakuna hata sentesi moja iliotolewa leo tunaambiwa kuna mambo 22 na Jumbe alipotaka kuengeza alifukuzwa kazi, sasa mnaposema tusizungumze mambo ya Muungano maana yake nini mnawaambia nini Wazanzibari”,alisema Mzee Moyo. Alisema amesikitishwa kuona Mwanasheria wa Zanzibar kueleza kuwa hana taarifa ya mswada huo jambo ambalo ni la maajabu kwa serikali kwani kinachotengenezwa ni katiba mpya na sio kutia viraka na ni vyema kamati hiyo ikapeleka ujumbe wa Wazanzibari nini wanachotaka. “Mnasema tusiseme mnataka tuzungumze utumbo, lazima mabadiliko yafanywe kwani hivi sasa vijana wamesoma na hawakubali kuamuliwa, Nyerere alikuwa anakubaliana na mzee Karume hakua anatoa maamuzi, Wewe sita umefanya kazi na Nyerere, Jumbe na Karume msifanye mambo ya wakati ule ‘is over’ ”, alisema Mzee Moyo.

Ali Mwinyi Msuko

Kada huyo wa CCM, alisema wanasheria wa Zanzibar wakae na wanasheria wa Tanzania bara kuupitia upya mswada huo na hakuna sababu ya kuharakisha kupelekwa Bungeni, rais Nyerere na Karume walikubaliana katika Muungao huo na kwa sasa nchi mbili hizi zikubaliane. Alishauri kwamba mswada huo urudi tena Bungeni na ufuate taratibu kwa kisheria na kwa sasa hakuna sababu yeyote ya kujadiliwa huku akitoa mfano kwamba kujadili mswada huo ni sawa na kutwanga maji kinuni.

Salum Bimani

Mkereketwa huyo wa CUF, alisema anashangazwa na Waziri Sitta kutokana na kujipa maadaraka ya kuandaa taratibu za kuingiza Zanzibar katika Jumuiya ya Afrika Mashariki jukumu ambalo halikupata ridhaa ya wazanzibari,

Ali Omar NCCR Mageuzi

Alisema kinachoonekana ni muendelezo wa serikali ya Muungano kuiburuza Zanzibar kwa kuona kuwa haiwashikishi katika mamaunzi makubwa.

Hamad Mussa Yussuf (CHADEMA)

Alisema madaraka ya wananchi yapo mikononi mwao na inashangaza kuona bado serikali ya Muungano imekuwa ikiamua bila ya kuishirikisha Zanzibari.

Awadh Ali Said

Alisema baada ya miaka 50, Wazanzibari wanataka kujua Muungano umewaletea tija gani na una kasoro gani. Alisema licha ya kuwa hakuna uwiano lakini yeye hakubaliani na hilo kwa kuwa lazima maslahi ya pande mbili yazingatiwe huku akilaumu kwamba mswada huo unaonekana ni wa upande mmoja wa Muungano wakati kuna nchi mbili zilizoungana.


Mohammed Ahmed Mugheiry

Alimtatahadharisha Waziri Sita kutokana na kumuona kuwa anacho kifanya kitamharibia sifa yake kwani wanapaswa kutambua kuwa serikali iliopo imechaguliwa na wananchi na hivi sasa Zanzibar kuna serikali ya umoja ya kitaifa ambayo tayari imekaa vizuri.

Samuel Sitta CCM

Akiwasilisha madhumuni na sababu za mswaada huo Samwel Sitta alisema mswada huo umependekeza kutungwa kwa sheria ya mabadiliko ya katiba ya nchi ya mwaka 2011 ambapo mswada unakusudia kuanzishwa kuweka masharti uanzishaji wa tume pamoja na sekretari kwa madhumuni ya kuendesha na kusimamia mchakato wa mabadiliko ya katiba ya jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mchakato wa mabadiliko ya katiba pamoja na muswada pamoja na masuala mengine utaangalia chimbuko na mahusiano ya katiba iliyopo kwa kuzingatia uhuru wa wananchi mfumo wa siasa ambao unatarajiwa kukamilika Aprili 1014. Alisema pindi mswada huo utakapopitishwa na kuwa sheria utakuwa na utaratibu wa kisheria utakaomwezesha rais kuunda tume ya kukusanya maoni kuhusu katiba na kuunda bunge la katiba kwa madhumuni ya kutunga katiba mpya.

Sitta aliwataka Wajumbe hao kushirikiana na Kamati hiyo kuwashawishi wananchi kukubaliana nayo na itapofikia wakati watoe maoni yao kwani wamelazimika kufanya hivyo kutokana na hivi sasa wanataratajia kuwasilisha kupata bajeti inayokadiriwa kufikia bilioni 30 na mwezi huu wa nne itakuwa ni wa matayarisho ya Bajeti hiyo. Hata hivyo Sitta aliahidi kuyafikisha maoni ya Wazanzibari kama yalivyotolewa katika mkutano huo. Wakati watu wakichangia hamasa na jazba zilitanda huku wakipiga makofi ya kukataliwa mswada huo na kuimba nyimbo ya ‘sisi sote tumegomboka kwa ndugu’
 
Safi sana kwani muswada mbovu huzaa sheria na kanuni mbovu, sheria na kanuni mbovu huzaa katiba mbovu na mwisho wa yote ni machafuko kwahiyo ni vizuri sana kuukataa muswada mbovu ambao unaweza kuzaa sheria na tarataibu mbovu... Hongereni zenji!!!
 
Ni ajabu sana kuona watanganyika hatujajali kabisa kwanza kupigania katiba ya nchi yetu ndio baadae tuongee mambo ya katiba ya muungano. Zanzibar wamekataa kwa sababu muswada unakinzana na katiba yao, sisi tunataka nini? Mwaka jana Zanzibar wamebadili katiba yao na kuitambulisha Zanzibar kama nchi sisi kwa nini tunaogopa kuuvunja muungano ili tuunde upya kulingana na mahitaji ya sasa?
Je huu Muungano una faida yeyote kwetu? Inakuwaje nchi kubwa na watu zaidi ya Milion 43 tunaendeshwa na nchi ndogo kuliko hata jimbo la uchaguzi la Ubungo? Ni kwa nini Viongozi wetu kutoka bara wanaogopa kuongelea suala la kuuvunja muungano ili tuweze kukubaliana upya? ni nini tutapoteza tukivunja muungano?
 
hata bara hatuutak huu mswaada maana hauna maslahi kwa taifa.............na jmosi ijayo tumeandaa kunji nchi nzima......
 
naam kumekucha

sasa tuwatake serikali ya jamhuri kufuata utaratibu ulioelekezwa na katiba yetu ili tuelekeee kwenye bara bara sahihi ya kutafuta katiba mpya

tuache kuogopa, watanzania wa leo ni waelewa wa nn wakitakacho, na huu si wakati tena wa baadhi ya watu kuwaburuta wengine, tena kwa kutumia ujanja ujanja
 
Inashangaza kwa nini tusipiganie katiba ya Tanganyika kwanza halafu ndio na sisi tuingie kwenye majadiliano na Zanzibar? Haiingii akilini kwa nini bado tunaumbatia huu Muungano badala ya kuuvunja halafu tutengeneza mpya kama kuna haja.
 
Back
Top Bottom