Sasa naweza kutamka kwa uhakika kuwa Musoma Mjini itakwenda kwa Nyerere wa CHADEMA. Kila nilikopita kati ya watu 10 ni 2 au 3 ndo CCM, waliobaki wote CHADEMA.
Wamejiandikisha. CCM walijaribu kununua baadhi ya shahada kama elfu 3 maeneo ya Nyakato, CHADEMA kama kawaida yao wakainasa issue kama ilivyo na kuwaanika jukwaani. Kwa hakika nimetoka Musoma leo jioni CCM wamepoteana kabisa. Nyerere ana sera zinazotekerezeka kwa watu wa chini na ana data mpaka za vikao vya ndani kabisa vya siri wanazopanga CCM. Na kama kawa ya CHADEMA data zote huwa wanazimwaga jukwaani na huwa zina kuwa za kweli kwa kuthibitishwa na watu hao hao wa CCM walioichoka.Asante kwa taarifa nzuri sana hiyo. Je uliwauliza pia kama wamejiandisha kupiga kura??
Wakinunua wewe unayeunga mkono upinzan unashindwa kupiga kura. Then ile kura uliyoshindwa kupiga wewe inapigiwa m2 wa ccm na kuingizwa kinyemela kwene kituo ulichojiandikishaKazi kweli kweli kwa CCM. Na hizo shahada wakizinunua, zinawasaidiaje kushinda? Ebu nijuze