MUSEVENI: Wapinzani Afrika hawajaiva kisiasa kama wale wa Ulaya

Mwabhleja

JF-Expert Member
Jan 27, 2016
1,351
2,058
Hiyo ni kauli ya Rais Mteule wa Uganda, Yoweri Kaguta Meseveni alipokuwa akihojiana na mtangazaji wa BBC Swahili Zuhura Yunisi. Rais Museveni amedai kuwa wapinzani Afrika wanapenda kuendesha siasa kwa kuchanganya na uvurugaji wa amani jambo ambalo halipendezi na ndiyo maana Besigye anawekwa kizuizini.
Pamoja na hayo Rais Museveni ameulizwa ikiwa ana mpango wowote wa kufanya mabadiliko ya kikatiba kusudi kiti cha urais kiwe katika msimu wa kipindi fulani cha uongozi aidha miaka mitano au minne lakini Rais Museveni amegoma kuzungumzia jambo hilo akidai kuwa halina umuhimu kwa sasa.
Ushindi wa Rais Museveni umetiliwa shaka na baadhi ya waangalizi wa kimataifa akiwemo Rais Mstaafu wa Nigeria, Olusegun Obasanjo aliyesema uchaguzi wa Uganda ulitawaliwa na usiri,ubabe na siasa chafu jambo linalotatiza uhalali wa uchaguzi huo.
Lakini pia katika anga za kimataifa, mgombea urais kupitia tiketi ya chama cha Republican anayeongoza katika kura za awali za maoni ameweka wazi msimamo wake dhidi ya wahafidhina barani Afrika hususani Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe na Yoweri Museveni wa Uganda.
Naam, mwana JF nini maoni yako katika hili. Je, ni kweli kwamba wapinzani tu ndiyo hawajaiva kisiasa kwa kuwafananisha na wapinzania wa Ulaya au Marekani ama hata watawala wa Afrika hawajaiva kisiasa na kauli ya Museveni ni kuwapooza wafadhili wa Ulaya?
 
Hahahaa.....kwa nini wanapoteza hela kufanya hayo maigizo yaitwayo 'uchaguzi' huko Uganda?
 
Museveni ni moja ya watu ambao wako kwenye kamati ya kumwomba Nkurunzinza aachie madaraka.
 
sadijumamarwa: Licha ya Dr.Besigye kuwekwa kizuizini taarifa zaidi zinatanabaisha kwamba mgombea mwingine Amama Mbabazi amezingilwa na maofisa wa polisi nyumbani kwake. Je, yaweza kuwepo matumaini ya kuheshimu katiba ndani ya muda mfupi kwa mtu aliyeikanyaga katiba hiyo kwa kipindi kirefu. Pasi na shaka Afrika bado ina safari ndefu kuelekea kwenye demokrasia ya kweli inayoheshimu misingi ya utu.
 
Wapinzani wa kiafrika hawajaiva kisiasa kama wale wa ulaya ila viongozi waliopo madarakani wameiva kisiasa kama wale wa ulaya. Hizi ni zile kauli zinazotoka kwa wale wasiojua kama hawajui.. I mean wajinga... Kauli za kijinga.
 
sadijumamarwa: Licha ya Dr.Besigye kuwekwa kizuizini taarifa zaidi zinatanabaisha kwamba mgombea mwingine Amama Mbabazi amezingilwa na maofisa wa polisi nyumbani kwake. Je, yaweza kuwepo matumaini ya kuheshimu katiba ndani ya muda mfupi kwa mtu aliyeikanyaga katiba hiyo kwa kipindi kirefu. Pasi na shaka Afrika bado ina safari ndefu kuelekea kwenye demokrasia ya kweli inayoheshimu misingi ya utu.
Nchi za jumuia ya Afrika Mashariki zipo kimya !Kenya Rais wao kampongeza M7! Hii jumuia Naona haina maana yoyote.Wanaogopana kuambiana ukweli na hakuna demokrasia ya kweli.
 
M7 kaingia madarakani nikiwa bado ninasukuma ringi na kuchezea makopo na kubeba vijiti vya mathe ktk begi langu la darasa la pili.Sasa hivi nina watoto na kukaribia kupata wajukuu yeye bado rais tu.Inamaana anatoa gamba kama chatu hazeeki?Jamani angewaachia wengine hicho kiti.Ni aibu kwa Afrika.Nchi ya Uganda nazani ina watu wengi sana tena wasomi hasa.
 
Why Africans' reasoning is so poor?Is it true that we are unintelligent creatures? When you hear such African leaders as Mugabe and Museven speak you will wish to switch off your TV, they're very embarrassing.
 
Back
Top Bottom