MURO TRANS, laacha barabara na kupinduka mara tatu

hilo ni princess muro .. na si muro trans

nadhani limeacha njia ... poleni majeruhi
 
Poleni majeruhi wote mliopatwa na mkasa!

MUNGU kawape nguvu majeruhi na wapone mapema.
 
Namshukuru Mungu sijasikia habari za vifo, hope majeruhi hawatapata ulemavu wa maisha. Poleni jamani!!!!
 
Madereva hawana huruma na abiria. Ingepitishwa kanuni kuwa kila gari la abiria liwe na nambari za simu za polisi wa
usalama barabarani ili inapotokea basi linaenda mwendo kasi kiasi cha kuhatarisha usalama wao waiarifu polisi.
 
Ni kweli kabisa ajali hiyo imetokea, na limepinduka mara 3.
Eneo la Mkolani-Buhongwa ni baya sana kwa hapa Mwanza, magari hukimbia sana na kuna kona 3, hakuna matuta na kuna mteremko mkali. Eneo lilipopindukia gari ni Darajani (kati ya Mkolani na Buhongwa). Ila kwa taarifa za uhakika, hakuna mauti katika ajali hii, ila walikuwemo wanafunzi wengi wa SAUT. Ni basi la princess Muro-YUTONG.
 
Huyu Bwana Kazi Yake ni Kusafirisha watu Kutoka Mwanza Hadi Dar!! Siku Zote na ni kazi anayoipenda, Sasa Haraka yake ni kukimbilia Wapi? Kwani akifika dar Kesho yake atarudi tena Mwanza!! Naona ni muda muafaka wa kuwaandaa hawa Madereva Kisaikologia Zaidi Kwani Hawatakiwi kuwa na Haraka kwani maisha yao ya kazi na furaha kwa familia yake inategemea yeye kuwa Salama na Mzima wa Afya!! Hivyo Hana budi Kuendesha Gari kwa Tahadhari na usalama ili familia yake imkute salama leo kesho na mtondogoo!! Enye Madereva acheni Haraka!! Ila maeneo Hayo ya Ajali kuna Askari wameweka Mapipa na ujenzi wa Kuziba Viraka unaendelea Inaweza Ikawa ndio Chanzo Cha Ajali kwani Tahadhari Zenyewe Zimewekwa Kiholela sana!! Naomba Mamlaka Husika zifanye Uchunguzi wa Kina na sio Kuwalaumu Madereva siku Zote!!
 
Ni kweli kabisa ajali hiyo imetokea, na limepinduka mara 3.
Eneo la Mkolani-Buhongwa ni baya sana kwa hapa Mwanza, magari hukimbia sana na kuna kona 3, hakuna matuta na kuna mteremko mkali. Eneo lilipopindukia gari ni Darajani (kati ya Mkolani na Buhongwa). Ila kwa taarifa za uhakika, hakuna mauti katika ajali hii, ila walikuwemo wanafunzi wengi wa SAUT. Ni basi la princess Muro-YUTONG.

mkuu inabidi ufanye kazi ya kuwashawishi wakubali, mie wamenigomea nimeamua kukubaliana nao
 
madereva hawana huruma na abiria. Ingepitishwa kanuni kuwa kila gari la abiria liwe na nambari za simu za polisi wa
usalama barabarani ili inapotokea basi linaenda mwendo kasi kiasi cha kuhatarisha usalama wao waiarifu polisi.

ukiona dereva anakiuka sheria za usalama barabarani, halafu ukamkemea abiria wenzako watakutukana. Namba za maafisa wa polisi kila mtu mwenye nia njema na taifa lake anatakiwa kuwa nazo, huwezi jua ipo siku zitaokoa maisha na mali. Sema kuna changamoto wengi wana mgogoro na jeshi
 
Mi huwan awashangaa sana hawa madreva, pale mkolani na Buhongwa kuna kona kali za ajabu ajabu, sasa wenyewe wakishafika hapo ndio wanaongeza mwendo, sijui ni sifa au ujinga. Poleni sana mliokumbwa na ajali hii.
 
hizi picha siyo kweli kwani hayo mabati hayawezi kuhimili mzigo wa tani 10. fikiria basi kama yale ya mohjamed trans, shabiby yaliyopata ajali kama hiyo yalikuwaje? labda kama liliacha njia lakini halikupinduka nitamwelewa mleta maada
 
halafu MUNGU huwa anaweza kuokoa awezavyo pamoja na ajali kuonekana mbaya kuliko. 25 wamejeruhiwa, lakini 6 kati yao hali zao si nzuri.
Sasa kama anaweza kwa nini hakuepusha ajali in the first place, ili asije tena kuhangaika kuwaponya? Huyo Mungu mnavyomuelezea utadhani power Mabula!

Anyhow, mwendokasi mara nyingi ni mchango wa abiria. Last year nimepanda Shabiby likawa linaenda mwendo wa wastani sana, halafu Shabiby lina tabia ya kusimama simama njiani kupandisha wanafunzi basi abiria wakaanza kulalamika kwamba hawafiki. Nikawashanga sana nikawaanzishia full timbwili, nikawaambia, kwani tiketi imeandikwa mnafika saa ngapi? Hakuna mwenye jibu, ila nilikuwa outnumbered nikaonekana mimi ndio kichaa na nina muda wa kupoteza barabarani. Yani hakuna mwenye concept ya road safety. Nadhani hata safety records zake ni nzuri hili basi, bahati mbaya linaishia Dodoma tu from Dar nadhani.
 
hizi picha siyo kweli kwani hayo mabati hayawezi kuhimili mzigo wa tani 10. fikiria basi kama yale ya mohjamed trans, shabiby yaliyopata ajali kama hiyo yalikuwaje? labda kama liliacha njia lakini halikupinduka nitamwelewa mleta maada

hivi kuwa great thinker ni mzigo kwa baadhi ya watu? tafuta mtu aliyeko mwanza, mpigie simu, mwulize kama ana taarifa za ajali hiyo, kama hana mpe kazi ya kutafuta ukweli halafu ndo uonekane umefanya utafiti. sio kila kitu kubisha tu
 
Sasa kama anaweza kwa nini hakuepusha ajali in the first place, ili asije tena kuhangaika kuwaponya? Huyo Mungu mnavyomuelezea utadhani power Mabula!

Anyhow, mwendokasi mara nyingi ni mchango wa abiria. Last year nimepanda Shabiby likawa linaenda mwendo wa wastani sana, halafu Shabiby lina tabia ya kusimama simama njiani kupandisha wanafunzi basi abiria wakaanza kulalamika kwamba hawafiki. Nikawashanga sana nikawaanzishia full timbwili, nikawaambia, kwani tiketi imeandikwa mnafika saa ngapi? Hakuna mwenye jibu, ila nilikuwa outnumbered nikaonekana mimi ndio kichaa na nina muda wa kupoteza barabarani. Yani hakuna mwenye concept ya road safety. Nadhani hata safety records zake ni nzuri hili basi, bahati mbaya linaishia Dodoma tu from Dar nadhani.

umenikumbusha mbali sana.

ukweli ni kwamba limepinduka/rolling mara tatu, wengi wamekataa kuwa halijapinduka mara tatu, lakini ndo ukweli. hakuna aliyepoteza maisha, 25 walijeruhiwa na bado gari linaonekana liko kwenye hali nzuri, ndo maana wengi wanakataa lilipinduka mara tatu.

we unadhani nani kaepusha
 
umenikumbusha mbali sana.

.... we unadhani nani kaepusha
Zamani eeh? Kwa hiyo unanambia ndugu yangu nikisema power Mabula inawezekana kuna a whole generation humu hawajui what I'm talking about? Duu, kumbe kweli nimezeeka aisee! Alikuwa analetwa shuleni kwetu kufanya miujiza, mara kachomwa bisu la tumbo hafi, mara kala moto haungui, mara kazuia landlover kwa jino la mbele! Nilivyokuwa mkubwa na kuelewa ule usaii nikagundua kwamba usanii wa Mungu ndio worse zaidi kwa sababu angalau power Mabula unamuona na kumgusa!

Anyhow, wasema sasa nani ameepusha. Ameepusha nini, watu wasife? Sasa kama ana nguvu ya kuepusha mtu asife na ana upendo kweli kweli, kwa nini asiepushe the whole big mishap in the first place? Alibiringishe gari mara tatu, watu wauumie vibaya lakni wasife, kwani nini anatuchezea kama midoli? Au alitaka tu ku create a big scene eneo la ajali? Hahahaha.....

Haya, mpe sifa yake kwamba kaepusha, lakini haitamaliza wiki hii tutasikia watu wamekufa barabarani, nikisema Mungu kaua mtasema Mungu katwaa! Mungu amempenda zaidi. Japo hapo atakuwa kashindwa kuepusha. Amewapenda zaidi ndio awaue kwa kuwapasua vichwa na vyuma vya malori? Ndo u power Mabula huu!

Ajali hazihusiani na 'Mungu.' Tujenge mifumo ya kuboresha usalama barabarani, na mara nyingi inaanzia na abiria wenyewe kudai mazingira salama zaidi ya usafiri, na ku stanch mfumo rushwa.
 
Back
Top Bottom