MAMMAMIA
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 3,811
- 1,603
Mwanamume mmoja alimuomba Mungu amjalie ageuke kuwa mwanamke kwa sababu alihisi mke wake anafaidi kubaki nyumbani wakati yeye anapiga mzigo masaa kumi mfululizo.
Mungu hakuwa hiyana, asubuhi alipoamka, akajikuta tayari amekuwa mwanamke. Harakaharaka akamtayarishia "mumewe" chai, ili ahawahi mzigoni, akakogesha watoto, akawapa chai na kuwatayarisha kuwapeleka shule. Wakati anarudi, akapitia sokoni kununua mahitaji ya siku. Kufika nyumbani, akaanza kusafisha nyumba na kufua nguo. Wakati anataka kutayarisha chakula, akagundua kuwa umeme umekatwa kwa sababu ya deni, ikabidi atoke mbio kwenda kulipia bili ya umeme. Alipotoka kule, wakati wa kwenda kuwachukua watoto ulishafika, ikabidi apitie shule. Kufika nyumbani, akaanza kutayarisha chakula huku watoto wanamlilia njaa.
Kwa ufupi, hadi kufika wakati wa kulala, bado hakuwa hajamaliza kazi zote, ikambidi aingie kitandani hivyo hivyo. Kitadani nako hakukuwa na kupumzika. "Mume" alitaka apewe kidogo, hakumkatalia. Lakini baada ya kumaliza tu akamwomba Mungu:
"Mungu wangu, nimefanya makosa, kwani kazi anazofanya mke wangu ni kumbwa kuliko nilivykuwa nikifikiria. Naomba unirejeshe katika hali yangu ya zamani".
"Hakuna tabu kiumbe wangu", Mungu alimjibu na kuendelea "ombi lako nimelikubali, lakini itabidi usubirie miezi tisa kwani jana ulipofanya mapenzi na mume wako, ulishika ujauzito"
Mungu hakuwa hiyana, asubuhi alipoamka, akajikuta tayari amekuwa mwanamke. Harakaharaka akamtayarishia "mumewe" chai, ili ahawahi mzigoni, akakogesha watoto, akawapa chai na kuwatayarisha kuwapeleka shule. Wakati anarudi, akapitia sokoni kununua mahitaji ya siku. Kufika nyumbani, akaanza kusafisha nyumba na kufua nguo. Wakati anataka kutayarisha chakula, akagundua kuwa umeme umekatwa kwa sababu ya deni, ikabidi atoke mbio kwenda kulipia bili ya umeme. Alipotoka kule, wakati wa kwenda kuwachukua watoto ulishafika, ikabidi apitie shule. Kufika nyumbani, akaanza kutayarisha chakula huku watoto wanamlilia njaa.
Kwa ufupi, hadi kufika wakati wa kulala, bado hakuwa hajamaliza kazi zote, ikambidi aingie kitandani hivyo hivyo. Kitadani nako hakukuwa na kupumzika. "Mume" alitaka apewe kidogo, hakumkatalia. Lakini baada ya kumaliza tu akamwomba Mungu:
"Mungu wangu, nimefanya makosa, kwani kazi anazofanya mke wangu ni kumbwa kuliko nilivykuwa nikifikiria. Naomba unirejeshe katika hali yangu ya zamani".
"Hakuna tabu kiumbe wangu", Mungu alimjibu na kuendelea "ombi lako nimelikubali, lakini itabidi usubirie miezi tisa kwani jana ulipofanya mapenzi na mume wako, ulishika ujauzito"