Bara la Afrika lazidi kupasuka vipande

JAMII-ASM

JF-Expert Member
Jul 30, 2015
1,305
524
in-africa-born-ocean-afar-triangle-photo_1.jpg

Kwa wale tunaoishi karibu na bonde la ufa -Rift valley, hili halitushangazi,kwani haipiti mwezi bila tetemeko la ardhi kutokea.Lakini ni dalili kwamba bara la Afrika linameguka ,tena kwa kasi.
Kwa mujibu wa utafiti unaofanywa na Dr James Hammond katika eneo lililopewa jina la Afar Triangle ambako ardhi imeanza kuzama na kuanza kutengeneza umbo linaloonekana kama maandalizi ya kuibuka kwa bahari itakayolitenganisha na kulipasua bara la Afrika katika mapande mawili. ni dhahiri kuwa muumba wa mbingu na ardhi bado hajamaliza uumbaji.
ESS_PasteBitmap05145.png

600x600

Kwa mujibu wa utafiti huu pande moja (plate) litazibeba nchi za Afrika mashariki..Tanzania,Kenya,Ethiopia,Somalia ,Uganda ,Rwanda ,Burundi na sehemu ya Msumbiji. Mpasuko huu utapita na kufuata maziwa makuu ya Tanganyika,Nyasa,Kivu,Edward na Albert.
300px-Albertine_Rift%2C_East_African_Rift_%28artificial_rendering%29.jpg

Ingawaje mpasuko huu ni wa milimita chache kwa mwaka lakini mtafiti huyu anasema kasi hii ya kupasuka ni kubwa kuliko sehemu yoyote duniani.
upload_2016-2-8_0-33-47.jpeg

Ila kawatoa hofu waafrika ..kwani mipasuko kama hii huchukua mamilioni ya miaka mpaka kukamlika. Lakini mwenyezi mungu huwa hana ahadi na yeyote. Akitaka litimie basi litatimia hata sasa.. hakuna wa kuzuia.

Giant crack in Africa formed in just days

Scientists are sounding the alarm: the mysterious cracks appear across the planet
 
Mkuu bora tusepe tu, ila sa sijajua kama tutondoka na kile chama ama tutakiacha huku!
 
asavali limeguke haraka tu maana tumechanganyikana na wajinga wengi
 
Ni kweli kabisa mungu hajamaliza kuumba tuwe kisiwani na ni bora sasa tuanze kuaandaa rais wetu sijui hili bara tuliitaje?
 
Back
Top Bottom