Mumewangu ndio chanzo cha mimi kuwa na uhusiano nnje ya ndoa!

kama anakusumbua sana tafadhali tuma private msg kwenye profile yangu ili nikupe mbinu mwanana za kukabiliana na hali hiyo
 
kama anakusumbua sana tafadhali tuma private msg kwenye profile yangu ili nikupe mbinu mwanana za kukabiliana na hali hiyo
mwaga ladhi hapa kwani hili tatizo ni la walio wengi!
 
tatizo wanawake hamna maamuzi kwenye kutumia zana za kujilinda wakati wa mapenzi na especially mkitoka nje ya ndoa, how come mwanamke uliyeko kwenye ndoa unafanya mapenzi nje ya ndoa bila kutumia kondom, ndio maana tunawalaumu sana nyie, waachieni wanaume tu waendelee kwani wanajua principles za kutoka nje ya ndoa,
Ndivyo unavyofikiaria mama...kaangalie kibeti ya mama watoto kule pembeni kama hutakutana na hizo condom. Kwani wao ndo hawajui kifo!ama?
 
hata wanawake wanajua prinsipo za kufanya hivyo nnje ya ndoa! acheni nao wajipe raha huko...mkuki kwa nguruwe eeeh?
Baeleze wajiju...maana wanajifanya kama wao ndo the experts! Kila mtu anajua hiyo prinsipo tena wanawake ndo makini kwa kuwavalisha hao wadudu mbilimbili.
 
Dear sio kuvunda tuu kitaoza kabisa na kupoteza lile tobo.

Kumbe Hatari beye!, Unajua siku zote anayekwenda kwa kisasi ndie aumiaye?.


  • Siku zote tatizo huwa halitatuliwi kwa tatizo (yaani piga nikupige).
  • Ikiwa mwanandoa hali inazidi kuwa mbaya ikifikia hivi.
  • Hakuna uamuzi wowote wa kukomoana ambao una matokeo mazuri ni lazima itaishia kumuumiza mmoja kama sio familia (watoto) ambao hawahusika kwenye hicho kinyang'anyiro.
  • Kama wewe una heshima zako, kutoka nje ya ndoa kwa kisa mwenzako ametoka haileti kinga pale jamiii itakapo baini huo upuuzi na pengine heshima yako ikishuka, huwezi kujitetea kwa kusema nilimfuatisha mume au mke wangu na ikitokea siku umefumaniwa, aibu au maumivu utakayopata huwezi kumshirikisha mwenzio.
  • Ikiwa pia utaambukizwa huko nje, usumbufu wa kujiuguza na maumivu yake ni yako pekee, huwezi kusema mwenzio akusaidie kwa kuwa alichangia kwa wewe kutoka nje ya ndoa.(utakufa peke yako, na kama ni dhambi itakuwa yako peke yako, kila mmoja wenu atapimwa kwa kipima chake cha dhambi!).
  • Kama upo timamu, na hukuwahi kuruhusu mwili wako au sehemu ya viungo vyake "kuchafuka" kwa kutoa utumike na kila mwanaume/ mwanamke uliyemwona mzuri kabla hata ya kuingia kwenye ndoa, huwezi kusema unapata furaha kwa tendo la ndoa ambalo umeamua kulifanya kwa kulazimishwa na mazingira eti kwa kuwa mwenzio ana toka nje ya ndoa (furaha ya ndoa ni zaidi ya hayo, inawezekana tu ukawa unatumika na huyo unayedhani anakupa furaha kumbe furahi inatokana na saikolojia yako kichwani. Kuhisi unapata furaha kwa tendo la "wizi" wa muda na mtu ambaye huna "future nae", ni kujipa matumaini ambayo mwishowe ni mbaya zaidi kuliko ungekaa kimya ili kutafuta mwafaka wa kutatua tatizo la mwenzio kutoka nje.
Kumbuka, Japo haimaanishi kuhalalisha huo upuuzi:

wanawake wanaotoka nje ya ndoa zao wapo katika hatari zaidi kuliko wanaume ukiacha maambuzi kwa kutokuwa na maamuzi ya kutumia au kutotumia kinga, pia ni vigumu kwao kuolewa na huyo wanayetoka naye wakati ndoa ikiendelea tofauti na wanaume ambao wanaweza kuoa hata mke wa pili au kuishi nae kama Kimada (nyumba ndogo) na jamii ikaelewa.
 
Hakuna suruhu ya matatizo ambayo hufanywa kulipiza kisasi, huo ni ujinga. Ni sawa kwenye footbal aliyefanya kosa la kwanza anaweza akawa mwema kuliko aliyefanya kosa kwa kulipiza kisasi.
 
FL1, kila jambo huwa lina chanzo chake. Hata mbuyu ulianza kama mchicha baadaye likawa jimti kubwa ajabu! Kuna mahali fulani kwa pande zote mbili nati zilianza kulegea hadi chombo yalianza kwenda mrama! The "first love" grew colder and colder until it went off!
Mimi naamini kwamba "two wrongs can not make a right!" Kwa hiyo siamini kwamba jino kwa jino ndio suluhisho, umeongeza tatizo juu ya tatizo! Watu wengi wanapenda kutatua matatizo ya muda mfupi (eg nyumba ndogo, etc) na kujifanya hawaoni matatizo yanayozunguka hilo "suluhisho" la muda!
Kama unamwamini Mungu, timiza sehemu yako katika ndoa, without any qualification or excuse, mwache mwenzako atimize sehemu yake!
Mwisho: Furaha ya kweli inatokana na kufuata Mapenzi ya Mungu, sio kwa kuwa na fedha na mali nyingi, kwani "Wamejaa amani nyingi waishikao Sheria ya BWANA!"
Pape, acha kwenda nje ya ndoa, eti kwa sababu unatimiziwa haja yako ya muda! Unalea bomu, likija kulipuka utakuja kujuta, it will be too late for sure! Tafuta njia ya kutengeneza ndoa yako badala ya kuchangia katika kuivunja. "Alichokiunganisha Mungu, Mwanadamu asikitenganishe!"


Well said buddy
 
Ndoa na iheshimiwe na watu wote!

Ukitoka kwakuwa mwezio alitoka umeshindwa kuiheshimu na kujiheshimu wewe mwenyewe pia!
 
Ndoa na iheshimiwe na watu wote!

Ukitoka kwakuwa mwezio alitoka umeshindwa kuiheshimu na kujiheshimu wewe mwenyewe pia!
Well said ndugu, leo nimeamka na wazo jengine, nikweli usilipize baya kwa baya. Ni heri mwenzio akianza hako kamchezo mtahadharishe na atakapo kuja kwako kukuomba unyumba mwambie avae condom kwa ajili ya afya yako. Then kama ikitokea akapotelea huko jumla mwache aende maana hakuwa njiwa wako. Cha msingi mtu aendelelee na maisha yake kama kawaida Mungu hamtupi mja wake ipo siku utapata wa kwako tuu. Kwa njia hiyo hata yeye atakapo kinai huko na kugeuza majeshi anakuta tuu harufu yako...ndipo atakapo tia akili. Nivizuri sana kwa kweli na sisi wanawake tujifunze ku weigh mizani yetu ya maisha(kwa kujielimisha na kujitegemea) na kujipa nafasi ya mambo kama haya yatokeapo we will be in which position to handle them. Nadhani hawa wadudu wangetia adabu sana na wasinge tubabaisha kwa kweli.
 
Kwa kawaida maisha ya ndoa ni kuvumiliana lakini mnapofikia mwisho wa uvumilivu, inakuwa mwenye msumari atajua mahali pa kutoboa kwa kutumia msumari wake huo na mwenye kapu atajua atie nini humo ndani ya kapu!!
 
Wangekuwa Sudan wote yeye na mumewe walitakiwa kupigwa mawe mpaka wafe!!!! Solution ya matatizo sio ujinga.. ulichokifanya wewe mama sijui bibi ni ujinga..Kama uliona ka cheat si ungefuata taratibu zinazotakiwa na fungua file la divorce kwani ata dini zinaruhusu divorce kwenye situation kama hizi..

Mtaambukizana maukimwi.........Wewe na mumeo wote UZUNI MTU!!!. sio story za kutoa wala kuomba ushauri ni upuuzi huu...

Nenda angaza kapime!
 
Wangekuwa Sudan wote yeye na mumewe walitakiwa kupigwa mawe mpaka wafe!!!! Solution ya matatizo sio ujinga.. ulichokifanya wewe mama sijui bibi ni ujinga..Kama uliona ka cheat si ungefuata taratibu zinazotakiwa na fungua file la divorce kwani ata dini zinaruhusu divorce kwenye situation kama hizi..

Mtaambukizana maukimwi.........Wewe na mumeo wote UZUNI MTU!!!. sio story za kutoa wala kuomba ushauri ni upuuzi huu...

Nenda angaza kapime!
je wewe umeshapima?
 
Back
Top Bottom