Ndivyo unavyofikiaria mama...kaangalie kibeti ya mama watoto kule pembeni kama hutakutana na hizo condom. Kwani wao ndo hawajui kifo!ama?tatizo wanawake hamna maamuzi kwenye kutumia zana za kujilinda wakati wa mapenzi na especially mkitoka nje ya ndoa, how come mwanamke uliyeko kwenye ndoa unafanya mapenzi nje ya ndoa bila kutumia kondom, ndio maana tunawalaumu sana nyie, waachieni wanaume tu waendelee kwani wanajua principles za kutoka nje ya ndoa,
Baeleze wajiju...maana wanajifanya kama wao ndo the experts! Kila mtu anajua hiyo prinsipo tena wanawake ndo makini kwa kuwavalisha hao wadudu mbilimbili.hata wanawake wanajua prinsipo za kufanya hivyo nnje ya ndoa! acheni nao wajipe raha huko...mkuki kwa nguruwe eeeh?
Mwe shosti ndo hivyo mwaya...na hiyo ni Nguruwe shosti sio ngulube au kama ulivyo state hapo juu.Penny siku zote mkuki kwa nguluwe ...
Dear sio kuvunda tuu kitaoza kabisa na kupoteza lile tobo.Hivi akina dada kwa nn mnalipiza ubaya kwa uovu? Ukitulia kwani kitumbua kitavunda?
Dear sio kuvunda tuu kitaoza kabisa na kupoteza lile tobo.
FL1, kila jambo huwa lina chanzo chake. Hata mbuyu ulianza kama mchicha baadaye likawa jimti kubwa ajabu! Kuna mahali fulani kwa pande zote mbili nati zilianza kulegea hadi chombo yalianza kwenda mrama! The "first love" grew colder and colder until it went off!
Mimi naamini kwamba "two wrongs can not make a right!" Kwa hiyo siamini kwamba jino kwa jino ndio suluhisho, umeongeza tatizo juu ya tatizo! Watu wengi wanapenda kutatua matatizo ya muda mfupi (eg nyumba ndogo, etc) na kujifanya hawaoni matatizo yanayozunguka hilo "suluhisho" la muda!
Kama unamwamini Mungu, timiza sehemu yako katika ndoa, without any qualification or excuse, mwache mwenzako atimize sehemu yake!
Mwisho: Furaha ya kweli inatokana na kufuata Mapenzi ya Mungu, sio kwa kuwa na fedha na mali nyingi, kwani "Wamejaa amani nyingi waishikao Sheria ya BWANA!"
Pape, acha kwenda nje ya ndoa, eti kwa sababu unatimiziwa haja yako ya muda! Unalea bomu, likija kulipuka utakuja kujuta, it will be too late for sure! Tafuta njia ya kutengeneza ndoa yako badala ya kuchangia katika kuivunja. "Alichokiunganisha Mungu, Mwanadamu asikitenganishe!"
Na asiporudi?
Well said ndugu, leo nimeamka na wazo jengine, nikweli usilipize baya kwa baya. Ni heri mwenzio akianza hako kamchezo mtahadharishe na atakapo kuja kwako kukuomba unyumba mwambie avae condom kwa ajili ya afya yako. Then kama ikitokea akapotelea huko jumla mwache aende maana hakuwa njiwa wako. Cha msingi mtu aendelelee na maisha yake kama kawaida Mungu hamtupi mja wake ipo siku utapata wa kwako tuu. Kwa njia hiyo hata yeye atakapo kinai huko na kugeuza majeshi anakuta tuu harufu yako...ndipo atakapo tia akili. Nivizuri sana kwa kweli na sisi wanawake tujifunze ku weigh mizani yetu ya maisha(kwa kujielimisha na kujitegemea) na kujipa nafasi ya mambo kama haya yatokeapo we will be in which position to handle them. Nadhani hawa wadudu wangetia adabu sana na wasinge tubabaisha kwa kweli.Ndoa na iheshimiwe na watu wote!
Ukitoka kwakuwa mwezio alitoka umeshindwa kuiheshimu na kujiheshimu wewe mwenyewe pia!
je wewe umeshapima?Wangekuwa Sudan wote yeye na mumewe walitakiwa kupigwa mawe mpaka wafe!!!! Solution ya matatizo sio ujinga.. ulichokifanya wewe mama sijui bibi ni ujinga..Kama uliona ka cheat si ungefuata taratibu zinazotakiwa na fungua file la divorce kwani ata dini zinaruhusu divorce kwenye situation kama hizi..
Mtaambukizana maukimwi.........Wewe na mumeo wote UZUNI MTU!!!. sio story za kutoa wala kuomba ushauri ni upuuzi huu...
Nenda angaza kapime!