Kima mdogo
JF-Expert Member
- Sep 17, 2011
- 303
- 46
Alikua mume mwema sana,Mwenye upendo wa hali ya juu sana na mimi na mwanae,Alianza kubadilia baada ya mimi kubeba mimba,Alikua mkatili sana kwangu na hakunijali kabisa kwa kipindi chote cha ujauzito,Niliumia lakini nilijipa moyo kw huenda ni kutokana na ujauzito,...nilishtuka sana baada ya kujifungua mtoto wa kiume anayefanana naye sana akanitamkia kwa mdomo wake kuwa hamtaki huyo mtoto na ni bora ningekufa na mimba,Kwakweli iliniuma sana nikafatilia na kugundua kuwa anamwanamke anayedaiwa kazaa naye japo haina hakika km mtoto ni wake,Na inasadikika kuwa mwanamke huyo anauhusiano wa kimapenzi wa muda mrefu na mfanyakazi wa mume wangu ambaye yeye ndo alifanikisha kumtegea mume wangu dawa ili awe na uhusiano na mwanamke huyo (mwenye watoto 3) na wanashirikiana kumwendea kwa mganga ili amjengee huyo mwanamke nyumba. Nisaidieni nifanyaje jamani