Mume wa rafiki yangu

mimi sijaelewa tatizo bado; kama yote anayokuambia tena hadharani, bila kuuma maneno na mbele ya mke wake akimaanisha kuwa ni kweli kwamba:

a. Kaka una miguu ya CCM
b. Macho ya chama
c. Umbo la kibalozi
d. Ngozi laini ya kifisadi fisadi

Mpe hizo sifa mbele ya mke wake halafu tuone mtaishia wapi, inawezekana ndio mtakuwa mnaheshimiana zaidi. DON'T take it too serious...

On the other hand.. itakuwaje kama hizo ni preview ya kukupigia mahesabu?


MMJ asante nimecheka sana, hapo kwenye macho naweza kusema ana macho ya uzinzi ...sijui ndio hayo ya chama?


Annina
 
Nadhani unamuendekeza, posibly kwa sababu zako binafsi!
- Wewe ni single, married, divorced, widowed?
- Wewe unapomuona unahisi vipi? I mean kuna hisia yoyote uliyonayo juu yake?
- Umeshaongea na mke wake kuhusu kutopendezwa na tabia ya mumewe?
- Kwani njia yao ya kwenda kazini inapitia barazani kwako?

Obuntu asante kwa kuchangia.
  • Nipo kwenye serious mahusiano na huyu mume wa rafiki yangu anafahamu hilo,
  • Sijazungumza nae, sababu mume wake huwa anasema mbele yake - niliamini katika hali ya kawaida angechukua hatua,
  • Sina hisia zozote kwake
  • Ni majirani zangu, tunashare parking.
Natumai nimejibu maswali yako, asante sana.

Annina
 
Hapo kwenye red.....Natamani kukuona ili niongeze exposure:bounce:!

Kwa vile bado hujamfahamu vizuri huyo bwana, inawezekana ni mapema mno kufanya conclusion yoyote hasa ukizingatia mambo hayo anafanya mbvele ya mekewe (hayafanyi mafichoni). Kwa mfano suala la ku'hug' kwa baadhi ya watu sio ishu kihivyo. Na hilo la kusifia, kuna watu wana tabia ya mzaha sana hata kwa watu wageni.

Lakini kama walivyosema wengine kama ukaribu huo unakukera ni vema ukamueleza wazi huyo bwana bila kuuma maneno na hasa body language yako ioneshe kweli hupendi/hutaki!

Kuna vidume havina aibu na vinaweza ku flirt kiutani na mke akachukulia utani kumbe ndio vinafanya kweli! No sio mapema tena amechelewa sana! Amani yako moyo ni muhimu na hao mke na mtoto wala hawana habari na kinachokusibu; TAKE ACTION mamii
 
Kuna vidume havina aibu na vinaweza ku flirt kiutani na mke akachukulia utani kumbe ndio vinafanya kweli! No sio mapema tena amechelewa sana! Amani yako moyo ni muhimu na hao mke na mtoto wala hawana habari na kinachokusibu; TAKE ACTION mamii
hhehehehe!hapa nilijua tu hommie langu lazima lichangie tu!
ai miin YUU HAS TU SEI SAMSINGI HIA BANA!
 
hhehehehe!hapa nilijua tu hommie langu lazima lichangie tu!
ai miin YUU HAS TU SEI SAMSINGI HIA BANA!


Hommie wea av yu been?

teh teh teh

Nakuja mjini probably this weekend .............vikage uvaso! :becky::becky:
 
JF kuna watu vichaa...
Duh, nimeianza siku kwa kucheka mna...asanteni na pole dada Annania, ushauri ushapewa kazi kwako!
 
oh pole sana dada yangu

Unajua nikupe siri
  • Kitendo cha kwamba anakusifia na akaona positive response hiyo ikampa green light
  • pili kitendo cha huo ufundi/sanaa za maneno huenda inakufurahisha na ushaidi ni jinsi ulivyo yanukuu hayo maneno nadhani yanajionyesha eg umbo la kampeni, huyu jamaa inaelekea ni mtunzi mzuri ila hajajua tu kipaji chake
  • tatu ameona akikupatia ufundi wa maneno kuna positive response japo unajidai kupinga kwa mbali (kwa mwanaume huwa anajipa matumaini ya kuwa hapa mwanzo ni mgumu nikiongeza bidii kidogo tu nampata maneno mengine huwa wanaume tunasema (she mean try hard stupid)
  • nne baada ya kuona mission pre-accomplished ndio maana akaamua ku take extra step kuku hug na kuongeza chumvi kidogo ka sanaa yake kama ada i.e una ngozi laini
  • Tano kwa mimi ninavyoona ni kwamba unamfurahia ila tu unajiuliza kuhusu mkewe ambaye ni rafiki yako
Ushauri
  • Usifuge ugonjwa kama kweli hutaki maana mapenzi ni kama majani huota popote hata juu ya nyumba utani utani mwishowe utampenda huyo bwana as i know ladies
  • Tatu kama kwa dhati unachukia hiyo tabia ni bora useme ukweli hata kama utagombana na rafikiyo kuliko kuzua balaa kwani huenda huyo dada sio rafiki bali ni jamaa wa karibu
  • Mwisho waswahili wanasema akimwaga ugali wewe mwaga mboga potelea mbali mwambie ukweli na usimuonee haya wala kumuogopa kwani yeye mbona hakuonei haya kuku harassssssssss
kila la heri
 
Furahaeliud asante sana kwa ushauri, unaonekana kuwafahamu vyema wanaume hasa wenye vipaji kama cha huyu mume wa rafiki yangu. Nashukuru kwa mawazo yako.


Annina
 
wewe annina nawe uko very welcoming....sikulaumu wanawake wengi mko hivi. ....U pple u need 2 change....U can use ur face, anything to show or xpress hufurahishwi na anavofanywa.....Lakini wewe ndo kwanza tabasam kwa sana na unaendelea kumpa point jamaa....
 
Asante Tripo9, itabidi nikionana nae nilambe ndimu ili niwe na sura ya ugwadu lol!


Annina
 
Mh, unajua inawezekana yumo humu!! Kama si mume basi mke!!

Tena mi namhisi kakangu Xpin, haswa kwa vile jibu lake la mwanzo lilikuwa ' Nitarudi kukujibu'!!

Pole sana Annina, kuna watu wengine wako hivyo tu. Nakuelewa kabisa unavyokosa raha. Na inaonekana umetokea kuuthamini urafiki wa huyu dada.....kila la kheri
 
Wapendwa nina rafiki ambae pia ni jirani yangu. Urafiki ulianzia kwa mtoto wao wa miaka 4, tukafahamiana na mama wa mtoto na tukawa marafiki na hatimae nikatambulishwa kwa baba wa mtoto ambae pia ni mume wa huyu rafiki yangu. Tulipoonana mara ya kwanza akadai nafanana sana na dada mmoja na haamini kama hatuna undugu na huyo dada - mke wake hamfahamu huyo mdada ninaefananishwa nae nami simfahamu pia.

Toka siku hiyo kila tunapoonana amekuwa hakosi cha kusema juu yangu, mara nina macho ya uhamasishaji, lips sijui za kufanyaje.... umbo la kampeni... nk nk. Amekuwa akiyasema hayo mbele ya mke wake na rafiki zake. Sijamzoea wala sina utani nae, na nimeweka wazi kwamba sifurahii anachokifanya lakini ni kama hanielewi. Leo asubuhi tumekutana akiwa na mke wake wanaelekea kazini, mke wake akaja kunisalimia na kunihug, mume nae akaja akafanya kama mke wake hii ni mara ya kwanza kwa yeye kunihug, akashtuka kama kapigwa shoti na akasema nina ngozi laini hajapata kuona! Nilijisikia vibaya na niliona mke wake pia amekosa amani. Sijui kilichoendelea baada ya kuachana nao. Nimebaki na maswali mengi na sijui ana maana gani kwa anayoyafanya lakini naona anavuka mipaka. Nilikuwa na imani mke wake atachukua hatua na kumkanya, sijui kama amefanya hivyo.

Wapendwa mnalionaje hili?


Annina

Annina, huyu jamaa ni kama unampa ruhusa ya kusema anayoyasema mbele ya mkewe na wewe kunyamaza kimya na pia kukukumbatia mbele ya mkewe na wewe usitie neno. Mwambie mbele ya mkewe kwamba hupendelei kabisa sifa anazokupa kuhusu uzuri wako na pia anapotaka kukumbatia basi usimruhusu akukumbatie hapo utakuwa umefikisha ujumbe...watoto wa mjini wanasema mkoromee...LOL!
 
...........mhhhhhhhhhhh!!Njia nzuri hapo ni kuwaepuka wote huyo rafiki yako na mume wake usiwe close nao. Bila hivyo mtakuja kukorofishana na huyo rafiki yako kwa ajili ya mume wake. Ninavyosema hivi mimi mwenyewe yalishanikuta kama hayo, hivyo hivyo mume wa rafiki kutwa kunisifia hadi mkewe ambaye ni rafiki yangu wivu ukamwingia na kuhisi namchukulia mumewe kumbe mumewe alikuwa limbukeni tu.Halafu mbaya zaidi anakusifia vitu ambavyo mkewe hana hapo ndio kasheshe kweli kweli.
 
Nipo kwenye serious mahusiano na huyu mume wa rafiki yangu anafahamu hilo, Sijazungumza nae, sababu mume wake huwa anasema mbele yake - niliamini katika hali ya kawaida angechukua hatua, Sina hisia zozote kwake

Sasa hapa ndo kwenye suluhisho, kama yeye anaweza kukufanyia yote haya Annina tena akiwa mbele ya mkewe.
Wewe na wewe mwambie huyo ambaye uko kwenye mahusiano naye serious, hapa yote uliyosema haya (kwanini hujamwambia mpaka leo kama kweli inakuudhi).
Naamini ukifanya hivi huku unakoita kunyanyaswa kutaisha maana jamaa yako atamaliza kila kitu sio kama huyo dada rafiki yako ambaye amekaa kimya.

Waswahili husema '' akimwaga mboga wewe mwaga ugali '' kama kweli hujali..
 
Hakuna hata haja ya kumwambia mkewe wala kusubiri wakati mkikutana pekeyenu, wewe mkikutana tena mpe live kwamba shemeji sipendi the way unavoongea juu yangu, na vyote anavyofanya. wish you all the best.
 
...........mhhhhhhhhhhh!!Njia nzuri hapo ni kuwaepuka wote huyo rafiki yako na mume wake usiwe close nao. Bila hivyo mtakuja kukorofishana na huyo rafiki yako kwa ajili ya mume wake. Ninavyosema hivi mimi mwenyewe yalishanikuta kama hayo, hivyo hivyo mume wa rafiki kutwa kunisifia hadi mkewe ambaye ni rafiki yangu wivu ukamwingia na kuhisi namchukulia mumewe kumbe mumewe alikuwa limbukeni tu.Halafu mbaya zaidi anakusifia vitu ambavyo mkewe hana hapo ndio kasheshe kweli kweli.

Asante sana Pretty, nitawaepuka.Naona afadhali wewe rafiki yako aliingiwa na wivu - kwangu ingekuwa dalili nzuri na maswali ninayojiuliza yangepungua. Lakini huyu rafiki yangu hakuwa akionyesha dalili za wivu wala kukerwa na anachofanya mume wake, ni leo asubuhi tu ndio ameonyesha kukosa amani.

Pole na wewe kama yalikukuta hayo.


Annina
 
Back
Top Bottom