Annina
JF-Expert Member
- Nov 15, 2009
- 437
- 57
Wapendwa nina rafiki ambae pia ni jirani yangu. Urafiki ulianzia kwa mtoto wao wa miaka 4, tukafahamiana na mama wa mtoto na tukawa marafiki na hatimae nikatambulishwa kwa baba wa mtoto ambae pia ni mume wa huyu rafiki yangu. Tulipoonana mara ya kwanza akadai nafanana sana na dada mmoja na haamini kama hatuna undugu na huyo dada - mke wake hamfahamu huyo mdada ninaefananishwa nae nami simfahamu pia.
Toka siku hiyo kila tunapoonana amekuwa hakosi cha kusema juu yangu, mara nina macho ya uhamasishaji, lips sijui za kufanyaje.... umbo la kampeni... nk nk. Amekuwa akiyasema hayo mbele ya mke wake na rafiki zake. Sijamzoea wala sina utani nae, na nimeweka wazi kwamba sifurahii anachokifanya lakini ni kama hanielewi. Leo asubuhi tumekutana akiwa na mke wake wanaelekea kazini, mke wake akaja kunisalimia na kunihug, mume nae akaja akafanya kama mke wake hii ni mara ya kwanza kwa yeye kunihug, akashtuka kama kapigwa shoti na akasema nina ngozi laini hajapata kuona! Nilijisikia vibaya na niliona mke wake pia amekosa amani. Sijui kilichoendelea baada ya kuachana nao. Nimebaki na maswali mengi na sijui ana maana gani kwa anayoyafanya lakini naona anavuka mipaka. Nilikuwa na imani mke wake atachukua hatua na kumkanya, sijui kama amefanya hivyo.
Wapendwa mnalionaje hili?
Annina
Toka siku hiyo kila tunapoonana amekuwa hakosi cha kusema juu yangu, mara nina macho ya uhamasishaji, lips sijui za kufanyaje.... umbo la kampeni... nk nk. Amekuwa akiyasema hayo mbele ya mke wake na rafiki zake. Sijamzoea wala sina utani nae, na nimeweka wazi kwamba sifurahii anachokifanya lakini ni kama hanielewi. Leo asubuhi tumekutana akiwa na mke wake wanaelekea kazini, mke wake akaja kunisalimia na kunihug, mume nae akaja akafanya kama mke wake hii ni mara ya kwanza kwa yeye kunihug, akashtuka kama kapigwa shoti na akasema nina ngozi laini hajapata kuona! Nilijisikia vibaya na niliona mke wake pia amekosa amani. Sijui kilichoendelea baada ya kuachana nao. Nimebaki na maswali mengi na sijui ana maana gani kwa anayoyafanya lakini naona anavuka mipaka. Nilikuwa na imani mke wake atachukua hatua na kumkanya, sijui kama amefanya hivyo.
Wapendwa mnalionaje hili?
Annina