..habari wanajf,,kuna mume wa mtu mwenye watoto wawili amening'ang'ania kama ruba anataka nimzalie mtoto japo mmoja kwa madai ya kua mkewe kamjibu hana muda wa kuzaa anamuda na biashara zake maana wanaishi nyumba moja lakn kila mtu na chumba chake kwa miaka 5 sasa na hawez kumpa talaka mana wao niwakristo kanisa halina talaka na mimi ni muslim na anadai yupo tayar yeye kubadili dini mana haoni raha ya ndoa yake na mkewe,na mtoto wake wa kwanza ni best yangu kupita kiasi na mkewe ni kama dada yangu namheshmu sana..huyu mwanaume ananisumbua mpaka imefka kpnd nataka nimwambie mkewe lakni sijui nianzie wapi na mtoto wake kumwambia kama baba yake ananikera naogopa kupita kias yani hata kwao kwenda siendi tena nmebadili laini ya simu mara tatu lakn kila nikibadili ananambia labda nife ndo atashndwa kunifatilia...na akinipgia anataka kuniona ofisini kwake nsipoenda siku hiyohyo lazma aje mpaka getin kwetu kuniulizia kwetu nimekwenda wapi mana nimkubwa kazni kwao anauwezo wa kutoka muda wowote....plz nsaidieni nimwanzaje mkewe kumueleza mana sms zake zote ninazo anazonitumia na mimi simpendi hata kumuona yani ananinyima amani..,,
Mie sijakuelewa vizuri ebu nijibu maswali yangu,
1. unamuona kama anakusumbua kwa kuwa ana mke na watoto?
2.au Unamuona anakusumbua kwa kuwa kakupenda?
3.au Unamuona anakusumbua kwa kuwa tayari unamchumba?
4.au Unamuona anakusumbua kwa kuwa humpendi tu?
5.Aliposema anataka kusilimu ulimuuliza anasilimu kwa sababu yako au anasilimu kwa kukubali kuwa "Anashahidilia kuwa hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki ila Allah, anashahidilia kuwa Muhammad ni mtume wake"?
Tanbihi: kama utaamua kuolewa naye na msimamo wake ukawa ni kusilimu kwa sababu ya matamanio yake basi huyo hakufai jiepushe nae kwani atakutia mitihani. Akisha zaa na wewe atakuwa kisha timiza malengo yake ya kukuzini na atakuacha kama anavyomuacha huyo mwingine.