Mume wa jinsi hii........kama mke utavumilia kweli?

tendo la ndoa ni muhimu na kama kuna tatizo inabidi wasaidiane kutafuta solution (jamaa anaweza kuwa bize sana au nature ya kazi ni so demanding; mazoea yametawala na hakuna tena hamasa kwenye tendo; mama hana initiative anasubiri 'kuombwa' tu kila siku; mazingira na nafasi ya nyumbani etc); mengine yaliyobaki siyo big deal, mama ajitahidi kumsomesha jamaa taratibu, akielewa well and good but ikishindikana asimshinikize coz kimsingi watu tumeumbwa tofauti na haiwezekani wote tu-behave the same way

hii inakera MNO!namna hii naweza 'NISIOMBE' hata MIEZI MITATU au hata nikiomba ujue iatakuwa KWAAJILI YANGU TU!(ila ubinafsi kwenye eneo hili pia sio tabia yangu,so mtu(mjue tunatofautian sana) wa namna hii mke wa hivyo atamtesa sana!!
 
Huyo shogako ameshazowea dhiki, amuache hivyo alivyolala basi asimuamshe,akimuamsha atalala yeye as long as unapata kila kitu anataka mume a chichi nae bao ngapi 100? au anataka ajichanganye haoni wenzie waume zao wanaojichanganya wanavyo lia?
mwambia kama anachezea shilingi chooni asijekulia..
 
Dah!nimesoma post zote na nimeondoka na desa la kutosha,

Mwambie shosti atulize mpira huyo jamaa wala hana matatizo ana tatizo moja tu,
Anatakiwa kuwa karibu na mmewe na kwa pamoja watatue tatizo la kufanya tendo la ndoa,

Hilo ndio naliona ni tatizo hayo mengine ni ziada tu ndani ya ndoa na wengi wetu tunaiga tu hasa huku mijin,
Wenzio wanalia kutelekezwa,mume kashikwa na nyumba ndogo yy analilia outing!!!!!!

Anatakiwa ajipange upya kurudisha hamu ya tendo kwa mumewe kwan hiyo ndio ndoa,wengine hapa tunapowafanyia interview kigezo muhimu ni game tu hayo mengine yanatengenezeka.
 
maybe umejiachia na hujiweki vizuri ndo maana hana mvuto wa kukutana kimwili na anaona aibu kutoka nawe
 
Kuna aina ya wanawake mie hunisikitisha
Wanaishi maisha ya fasheni shoo

Utaskia baba nanihii hebu tuwahamishe watoto shule
Tuwapeleke Marimbe Academy
Akiulizwa kwa nini
Anajibu, Mama fulani kapeleka wa kwake hapo, ada mil4 kwa mwaka, sie watoto wetu wanasoma shule ya mil 2 kwa mwaka:A S-confused1:

Na ukisharyhusu hayo, mtaishi kwa kukimbizana na majirani maisha yote
Ndo huyu, mwanamme anakupeleka out na watoto? anakusubiri kwenye gari?
Umeshindwa tumia maneno ya kumtoa garini, hata ikibidi ku-act a bit of a bad girl?
Definetely tatizo ni la mwanamke

Huyu analinganisha mme wake na waume wa wengine.....anafanya kama kuna standard ya mme, na kimsingi anaweza kuwa hajui mahitaji yake ya mwanaume (anaiga na kulinganisha tu).......nadhani akifanya vyote alisema bado atataka vingine! (Kongosho kamaliza).

Japo hatujapata maelezo ya mme, ila huyu mke ana tabu kweli!
 
Huyo baba ana tatizo la low self esteem. Inawezekana hata hana confidence na mwili wake (si ajabu hata hizo mechi chache anangojea giza liingie na tanesco wam-support). Inawezekana malezi aliyopata na mazingira aliyopitia yamechangia. Dada ana kazi moja tu, vile wameshaoana, amjengee high self esteem. Amsifie mumewe mbele za watu na yeye akishuhudia kwenye mazuri yake, wakiwa alone amsifie ama na watoto wao amsifie pia.
Kuna vitu vidogo tu, kama kumshukuru mwenza kwa kujali familia, kununua chakula, na hata sex; vitu vinavyochukuliwa kama wajibu lakini ukishukuru kwa kukubali kufanya wajibu wake itamsaidia kubadilika na kutaka kufanya ya ziada.

Wewe umejua kumchambua mwanaume as if wewe ni mwanamke (sina hakika anyway), ila kwa mtazamo wangu msisimko huletwa na kilicho mbele yako. Una hakika gani huyo dada ni msafi, anavutia na ana staha mbele za watu kiasi huyo mumewe awe na hamu ya kukutana naye kutoka naye na kuwa naye mbele za watu?

Kamwe siwezi kumjaji mtu kwa hilo bila kujua mkewe ana matatizo gani. Nina rafiki yangu aliwahi kunilalamikia kuwa demu wake anapenda sana deep kissing, lkn huyo dada ni namba moja kwa kunuka mdomo: hili umelifikiria?
 
hii inakera MNO!namna hii naweza 'NISIOMBE' hata MIEZI MITATU au hata nikiomba ujue iatakuwa KWAAJILI YANGU TU!(ila ubinafsi kwenye eneo hili pia sio tabia yangu,so mtu(mjue tunatofautian sana) wa namna hii mke wa hivyo atamtesa sana!!

Nyinyi wanawake mna matatizo sana, hivi ni nani aliwaambia wanaume ni kama mashine na ile kitu ni kipande cha mti kwa hiyo kimekakamaa saa zote? Mumeo karudi kachoka hata hamu ya kula kande ulizopika vibaya hana ndio atakuwa na hamu ya huo mwili ambao haujaogeshwa tangu asubuhi?

Hebu kuwa msafi wa mwili na kinywa, andaa chai na karanga au korosho, mpatie mzee akirudi halafu apate maji ya kuoga. Weka mazingira safi hapo chumbani na chagua maneno ya kuongea naye halafu uone kama hatokuwa na hamu na wewe.

Nguo za kumvalia mwanaume wako ndani ndio mnavaa kwenda sokoni za kuvaa ofisini ndio mnavaa ndani. Na wapo ambao wameona kukaa uchi muda wote ndio kivutio bila kujua macho ya mumeo yakiuzoea mwili wako napo pia ni tatizo. Vaa nguo fupi inama hovyo hovyo unapokuwa umekusudia kumsedyuzi sio mpk kanisani, ebo!

Na sitaacha kuwaambia ujinga wenu mwingine: Vyakula mnavyotulisha ni sahihi?
Nani aliwaambia wanaume wanakula nafaka zilizokobolewa? Mboga za majani zimepikwa mpk zimekuwa mrenda na chumvi kibao kama unakausha samaki. Kwenye nyama umejaza mafuta kibao, na bado unategemea huyo mumeo awe na nguvu kama mimi!

Tambueni tofauti yenu na wanaume. Mwili wa mwanaume unahitaji nguvu na blood circulation nzuri kufanikisha haya mnayoyataka. Hapa ukiulizwa ni vyakula gani unamlisha mumeo utaleta vichekesho. Kwa akili zenu mnadhani kumpikia mume wali kuku mara 4 kwa wiki ndio kumpenda wkt unamharibu. Kazi kukariri mitindo ya ngono pasina kujishughulisha na nutrition.

Kwendeni zenu kule na mambo yenu ya kuiga. Mimi wife wangu anapika chakula changu special na yeye na mwanawe wanakula mikuku yao ya kwenye friji na wala simuulizi. Mkioneshwa hela mnaona kula hovyo ndio maisha, nyoo! Mbona wauza madafu wanakamua 24hrs? Badilikeni, jifunzeni mambo yenye kuleta faida: kupika na lishe ni mojawapo
 
Kupigwa na mkeo mchezo?

Bishanga mwenzio hata mama aniuzi vipi, hata nikasirike vipi, lakini tukishakuwa faragha na mama akiianza mautundu!, basi kwishnei.
Lakini akiuchuna hata anigusi wala nini! nazidi kukasirika, nazidi kuwa mnyonge, nazidi kukosa raha, Usingizi hauji kabisaa.
Hii nataka kuonyesha ni jinsi gani, kama mmoja anakuwa na msongo wa mawazo, au mmetofautiana kwa njia yoyote au mmegombana na mwingine akalitambua, muafaka wa yote upatikana mkiwa faragha, yote hupotea.
 
As long as there is love, trust, honesty, respect and loyaly tell her to hang on there shosty!!
 
Hawa hata kwetu wapo, ni experience niliyoishuhudia katika familia yetu kabisa, shemeji yangu mmoja hivi, haendi kanisani, haendi kwenye sherehe, yaan hana muda na familia kabisa, kituko ambacho sitakisahau hadi leo ni siku mtoto wake anabatizwa, ndo kwanza alisafiri kabisa

.......jamaa kabadilika baada ya kuoana, enzi za uchumba walikuwa wanatoka wote out. Inawezekana alikuwa anajitahidi kufanya hivyo ili ampate mwanamke.
 
Yaani Kongosho umenena. Hizi mbona c tatizo! Mwambie mdada ajiadjust kwa kumpokea na kumchukulia mumewe kama alivyo. Pengine malezi yake yalikuwa hivyo atambadilishaje sasa hivi?!

Tatizo lipo kwenye tendo la ndoa. Hebu kwanza kabla ya kuchukua hatua aongee naye, ajichungue na yeye asijekuwa yeye ndo hasisimshi!


Huyu analinganisha mme wake na waume wa wengine.....anafanya kama kuna standard ya mme, na kimsingi anaweza kuwa hajui mahitaji yake ya mwanaume (anaiga na kulinganisha tu).......nadhani akifanya vyote alisema bado atataka vingine! (Kongosho kamaliza).

Japo hatujapata maelezo ya mme, ila huyu mke ana tabu kweli!
Nyie wawili hebu twendeni bungeni kule tukajadili masuala ya Afya na Mustakabali wa taifa letu.....

Mj1.... Kumbe mnapenda sana dudu eh?
 
........Wana MMU mambo zenu!! Haya leo kuna hili, wewe mdada umeolewa na mwanaume ambaye anakujali. I mean anakupa huduma zote kama chakula, malazi na mavazi. Yaani chochote unachotaka kama ana uwezo nacho anakupa.

.......Ila sasa huyu mwanaume ana matatizo yake, nayo kama hivi:

  • Mvivu kukutana kimwili na mkewe, sio kwamba ana matatizo hapana. Yaani tendo la ndoa halipi kipaumbele sana.
  • Hapendi kutoka out, anaweza kumpeleka mkewe sehemu yoyote anayotaka kwenda, akifika huko yeye anabaki kwenye gari na kumuacha mkewe aende na watoto.
  • Wakialikwa sehemu, kama kwa marafiki kupata dinner au mkusanyiko wowote wa watu haendi, lazima atoe udhuru.
Hana maneno laini, kama mjuavyo wanawake tunapenda kusifiwa. Hata mkewe ajitahidi kufanya kitu kizuri kama kupika, kuvaa vizuri hajui hata kumsifia mkewe. Watu wa nje watamsifia mkewe lakini si mumewe.
Mkewe ameshamwambia muda mrefu kwamba hapendi hiyo tabia yake, na je watoto watajifunza nini kwa baba wa jinsi hii?

Huyu mdada ameniambia mengi kuhusu mumewe, ila mimi nimeshindwa kumwambia achukue uamuzi gani.......nimebaki tu nimezubaa kwa hizi tabia za mumewe.

Kuna mengi yakuandika kuhusu huyo mume wa mtu......sasa jamani mume wa hivi kweli anavumilika? Kama wewe mdada umeolewa na mume wa jinsi hii utafanyaje?

Toba..!!!:A S 13:...... Sasa ameoa mke wa nini? Alikuwa anatafuta mpishi?
 
Rafiki nakusalimu....

Afu sijakuelewa vizuri ujue......... we ushawaona wangapi kitandani ili kuthibitisha hoja yako?

Kuna wanaume na migumegume rafiki.....
rafiki hofu kwako,
halafu kweli hujanielewa..... nimesema sijawahi kusikia, siyo kuona. huyo wangu tu ananitoa jasho...........ndo maana sipati picha uvivu wa mwanaume, lol!
 
Back
Top Bottom