Mume na mtoto wa nje!!!

miss linga

Member
Apr 4, 2012
17
1
Habari ya kazi wa JF?mimi ni mwanamke wa miaka 28 nimeolewa na nina watoto wawili wa kike wa kwanza ana miaka 6 na anaemfuta ana miaka 4,juzi nimegundua mume angu kazaa mtoto mwingine na mwanamke mwingine mtoto ni mdogo kuliko wangu,nimechanganyikiwa jamani sijui ata la kufanya,ni bora ata huyo mtoto ningemkuta,nimechoka kuanzia akili mpaka mwili nyumba naiona chungu,naombeni ushauri wenu jamani nifanyeje mwenzenu
 
Vumilia, songa mbele......hamna lingine lolote utakaloweza kulifanya huyo mtoto hana makosa. Jaribu kuongea na mumeo ujue sababu iliyomfanya akamzalishe mwanamke mwingine(maana kuwa na mahusiano ni kawaida yao,ila mpaka ampe na mimba mmhh!) labda majibu atakayokupa yanaweza kukufungua zaidi. Piga goti muombe Mungu akupe muongozo. POLEEE
 
vumilia tu my dear
kama mumeo anakupenda
na anaishi kama baba hapo nyumbani
anatambua wajibu wake vizuri kama mwanaume vumilia
ndivo wanaume walivo..
huna hati miliki ya mwili wake kumbuka.....
 
nikupe pole sana kweli inauma japo wanaume ndio sisi huyo jamaa simuaminifu kwako hata kidogo ila sikushauri umuache wala usikatae kumpokea huyo mtoto na kumpenda wakati atakapoletwa umlee au kutambulishwa kwako najua inauma na pia najua uamuzi unaoweza kuupata au ushauri kwandugu au marafiki nikuondoka na kumuacha.ila mimi nakushauri uwe mvumilivu umuombe mungu ili uweze kulea hao wanao tabia haina dawa ila ongea nae taratibu nakumbusha hali ya magonjwa ilivyo sasa huenda akarudi nyuma mkumbushe pia kua endapo akiukwaa watoto nani atawalea na ingali bado wagogo?usitumie jazba kuongea nae pia onyesha utayari wa kumsamehe kwa kosa hili la kwanza na kumpokea huyo mtoto ila kwashart la yeye kuvunja uhusiano wa kimapenzi na huyo mwanamke ubaki uhusiano juu ya mtoto na sivinginevyo.baada ya hapo tafuta ukaribu na huyo mwanamke muwe marafiki hii itakusaidia pale patakapokua na mchezo mchafu utaugundua kirahsi zaidi
 
nikupe pole sana kweli inauma japo wanaume ndio sisi huyo jamaa simuaminifu kwako hata kidogo ila sikushauri umuache wala usikatae kumpokea huyo mtoto na kumpenda wakati atakapoletwa umlee au kutambulishwa kwako najua inauma na pia najua uamuzi unaoweza kuupata au ushauri kwandugu au marafiki nikuondoka na kumuacha.ila mimi nakushauri uwe mvumilivu umuombe mungu ili uweze kulea hao wanao tabia haina dawa ila ongea nae taratibu nakumbusha hali ya magonjwa ilivyo sasa huenda akarudi nyuma mkumbushe pia kua endapo akiukwaa watoto nani atawalea na ingali bado wagogo?usitumie jazba kuongea nae pia onyesha utayari wa kumsamehe kwa kosa hili la kwanza na kumpokea huyo mtoto ila kwashart la yeye kuvunja uhusiano wa kimapenzi na huyo mwanamke ubaki uhusiano juu ya mtoto na sivinginevyo.baada ya hapo tafuta ukaribu na huyo mwanamke muwe marafiki hii itakusaidia pale patakapokua na mchezo mchafu utaugundua kirahsi zaidi

sawa nitafanya asante sana.
 
Mmh cjui wanaume wakoje,i had the same problem,akili yangu yote apa inanituma kuondoka,ila mshirikishe mungu zaid
 
Aisee ndoa zina kazi!..
Anaonyesha kujutia aliyofanya au anaona sawa tu??
Anatimiza majukumu yake kama mwanzo au amebadilika??
Kama anajutia makosa yake na anatimiza majukumu yake msamehe,vumilia na maisha yaendelee..ila muonyeshe msimamo wako kama mwanamke anayejitambua,ukimchekea chekea sana utashangaa ameongeza na wa pili..mpige mkwara kidogo lol..
Pole ndo maisha ya ndoa hayo..
 
pole sana,yachukulie hayo ni ya kawaida ili upate amani mdada,hivi unadhani wanaume wenye ndoa na ambao hawana watoto nje wapo siku hizi?ni wachache mno!kama anakupenda,anakujali na anakuthamini vumilia tu,maana umri huo ulio nao na watoto wawili utaenda wapi?kote kumejaa,sanasana utajikuta unakuwa nyumba ndogo kwa mtu,sasa ipi bora uwe mwizi wa mume wa mtu au mmiliki halali?
 
kumbuka kuwa yawezekana unamtimizia yote mumeo,halafu bado kaenda nje,niamini maneno yangu,mwanaume kwenda nje si kwamba umridhishi,ni hulka tu!ila wewe usimnunie hata kidogo ongeze mapenzi zaidi na zaidi,pia muombe sana mungu wako,atakusimamia.
 
Inauma, huyo si mwaminifu kaa mzungumze hayo matatizo kama bado ana mahusiano na mama wa huyo mtoto ama sivyo, usiondoke kwa kuwa una watoto wadogo. Ikiwa ataamua kukuletea huyo mtoto umlee, sikushauri hata kidogo.
 
Kazi kweli! Kama unadhani unahitaji mtoto wa 3 na wewe mchakachulie. Formula ni kuwa mna open marriage, na wewe uta-apologise tu yeshe. (Tahadhari, uwe tayari kuachwa. Kama ni tegemezi sana chakachua kwa siri)
 
Pole sana shost, samahani lakini kwani huyo mumeo dini gani na huyo mwanamke kazaa nae tuu au kamuoa? isitoshe usitoke kwenye ndoa yako ukampisha yeye banana nae mpaka kieleweke,najua kama sio rahisi unahisi kama kuchanganyikiwa lakini jikaze wewe mwanamke na usikubali mwanamke mwenzio akakuzidi kete,kama mume mumeo wewe na unajua nini anapenda zaidi analadha gani na wapi mtamu funga mbeleko umrudishe mumeo nyumbani mlee watoto wenu na kumbuka hakuna ndoa
isiyo kua na misukosuko inshallah mwenyezi mungu atakupa moyo wa subra na ushindi.
 
Habari ya kazi wa JF?mimi ni mwanamke wa miaka 28 nimeolewa na nina watoto wawili wa kike wa kwanza ana miaka 6 na anaemfuta ana miaka 4,juzi nimegundua mume angu kazaa mtoto mwingine na mwanamke mwingine mtoto ni mdogo kuliko wangu,nimechanganyikiwa jamani sijui ata la kufanya,ni bora ata huyo mtoto ningemkuta,nimechoka kuanzia akili mpaka mwili nyumba naiona chungu,naombeni ushauri wenu jamani nifanyeje mwenzenu

Pole sana mamito, Japo sipo kwenye ndoa ila haka kaushauri kanaweza ku-work out.
je mumeo amepunguza mapenzi kwako, je anaonesha dharau kwako na je ameshakutambulisha rasmi ama umegundua tu, unamfahamu huyo mama wa huyo mtoto na je huyo mama anakuonesha dharau?? kama mumeo hajabadilika chochte vumilia shost make hakuna ndoa isiyokuwa na majaribu, ukisema ndoa ni chungu it means unafikiria kuondoka na je huko utakakokwenda kutakuwa tambarale??? au una mpango wa kuwa single milele.. kama walivosmea wadau utaishia kuwa nyumba ndogo ya mwingine bora uwe tu nyumba kubwa mama! kuna ndoa zina misuosuko asikwambie mtu. kuna wengine wanadharauliwa kama vile walituma maombi ya kuolewa na huyo mwanaume. VUMILIA NA PIA MUOMBE MUNU AKUSIMAMIE KATIKA HILO SUALA NA AKUPE UJASIRI..... Pamoja na kugundua umeshamuuliza mumeo na kama bado jipange kwanza, usiende kwa pupa ama hasira unaweza kukutana na talaka bibie, tafuta siku ambayo utakuwa na furaha na mumeo akiwa na furaha then umuulize kwa upole na hekima sana. Simama kama mwanamke jasiri ukionesha kukerwa na hiko kitendo ila co kwa jazba.... ni hayo tu!
 
Back
Top Bottom