Mume ana wivu

Labda amchukulie ticket aje huko wakae kwa mda hata wiki mbili then arudi,kwa kifupi ajiwekee utaratibu wa kutembeleana!
 
Kuna dada tunafanya nae kazi huku nje ya Tanzania, kaolewa mumewe yupo Dar ndoa yako ina miaka mitano, toka tumekuja huku jamaa anagombana na mkewe kila kukicha tangu mwezi wa 5 tuko huku huyu dada hana raha kabisa mumewe kila akipiga simu akisikia tu sauti hata ya gari ataanza kuuliza hapo uko wapi hujafika nyumbani na amesahau kuwa huku tunatumia usafiri wa public. Mbaya zaidi amemkasirikia toka ijumaa hajaongea na yeye huyu dada hata kazi inamshinda analia tu kila mara. Amefikia kusema kuwa anataka kurudi maana hali imefika pabaya. Na mkataba tulipewa three years? Je? Aache kazi arudi Dar ama afanyeje mie nimeshindwa kumshauri maana ukiongea nae tu analia nikaona niilete hapa tumshauri. Tafadhali nisaidieni najua humu nitapata jibu

...mwambie awe ngangari bana, analia lia kitu gani?
Ajifunze tu kumweleza ukweli mumewe. Wanawake wa aina hiyo ndio wale
tangia mwanzo walikuwa "hewala bwana, ....!" kila analofanya alitangulia kumfurahisha mumewe matokeo yake ndio hayo sasa,
eti arudi...khaaaa!? atakuja jutia nafasi hii...

'Akunyimae kunde kakupunguzia mashuzi!', kama jamaa kanuna kupiga simu si ndio kero zimepungua?
Mpelekeni 'viwanja', na winter hii aaaahhh...soon atasahau machungu.
 
nakushauri usiache kazi yako binadamu vigeugeu sana usije ukarudi hapa mambo yakigeuka kidogo ukaanza kumtupia lawama mume naamini ataelewa siku moja unayofanya ni kwa faida ya familia simamia yale unayoamini (tija)ikizingatiwa yatakulinda siku zote hasira nyingi ni sababu ya kupenda kuridhishwa kuliko kuridhisha nikimaanisha UBINAFSI
 
That explains everything... Mwanaume anajisikia inferior... na hilo tatizo ni kubwa sana, sijui atasaidiwaje... ila kwa ufupi ni kwamba, dada aache kazi arudi TZ akae na mume wake...
whattttt!!!!!!! yaani kweli katika halil hii ya maisha magumu watu wanatafuta kujikomboa kiuchumi eti mke aache kazi kisa mume???? we unadhani mume angekua ameenda huko nje angekumbuka hata kupiga cm sikwambii kuacha kazi kuja kumkumbatia mkewe, hivi hamjui ukiwa na mawazo ya kukosa pesa hata mapenzi hayafanyiki??? na usikute huyo mwanamume alioa mke 'ready made' kasomeshwa na wazazi halafu eti kwa ajili ya 'kukaa' na mume aache kazi! mmh ckujua kama dunia ya leo bado watu wanawaza kama enzi ya 2 ya mawe!!!!!!!!!!!!:disapointed: ooh Lord have mercy!!!!!!!!!
 
Hivi mwanaume harusiwi kuwa na wivu au si kawaida mwanaume kuwa na wivu?

Anaruhusiwa kuwa na wivu wenye kuleta maarifa ktk familia yake. Sasa huo mpango wake wa kumfikiria vibaya mkewe wakati walikubaliana kuwa aende kutafuta pesa mi naona ni zaidi ya wivu.
Huenda anachukulia mapenzi kama silaha ya yeye kusema lolote kwa mkewe. Kama anaona hawezi kukaa bila mkewe na washauriane kufanya taratibu zitakazomfanya aende akaishi naye ktk nchi husika.

Watu wengine wanakera sana kwa kukatisha tamaa watafutaji ktk familia.

Bahati mbaya mimi si mwema ki hivo....kama vipi nitaachia moja lenye maslahi duni!
 
Jamani jamani, siku zote mawasiliano na uwazi ni kitu muhimu. Mke ampe ukweli kwamba mme atulie wakati mama anatafuta riziki. Ila kama walishafanyia ukwale hapo mwanzo lazima uaminifu utakuwa down. Hata akiwa naye bongo kama ni kudinywa atadinywa tu.

mama apige kazi kwa manufaa ya family. ila wapeane mambo.........
 
Back
Top Bottom