Mwita Maranya
JF-Expert Member
- Jul 1, 2008
- 10,564
- 7,973
Wadau wa MMU, habari zenyu bana.
Juzi kati nilikuwa nimekaa kwenye kiti kirefu mahali fulani katikati ya jiji, pembeni yangu kulikuwa na meza wamekaa mashostito wawili wanapiga stori huku wakilamba vimiminika na mdudu.
Mwanzoni walikuwa wanazungumza kwa kunong'ona, lakini baadae kadri stori ilivyonoga na kinywaji kukolea, ndipo mmoja wao aliyekuwa anaonekana kutoa masimulizi muda mrefu akafyatuka kwamba;
"Siku mume wangu akifa, kesho yake naolewa. Tafadhali sana msije kuniuliza huyo mchumba nilimpata lini na wapi". "Tena natamani life hata leo hii ili nipate furaha, kwanini niendelee kuteseka kwa sababu ya limmbwa lisilojua thamani ya mke?" Life is nothing if i'm not happy (akaweka msisitizo kwa kidhungu)!!
Baada ya kusikia hivyo, sikutaka kuwa shahidi katika kesi inayoweza kumpa mtu life ban ama kitanzi, nikapiga funda la mwisho nikajiondokea zangu huku nikijiuliza huyo bwana kamkosea nini mkewe hadi amuombee kifo?
MYTAKE:
Akina dada na akina mama wa hapa JF naomba kufahamu kupitia kwenu, ni kosa gani huyu mume kamtenda mwenzenu hadi anamuombea kifo? Je tayari ameshapata mchumba/mume mwingine anasubiri tu kifo cha mumewe ili atimize ndoto zake?:scared::thinking:
Juzi kati nilikuwa nimekaa kwenye kiti kirefu mahali fulani katikati ya jiji, pembeni yangu kulikuwa na meza wamekaa mashostito wawili wanapiga stori huku wakilamba vimiminika na mdudu.
Mwanzoni walikuwa wanazungumza kwa kunong'ona, lakini baadae kadri stori ilivyonoga na kinywaji kukolea, ndipo mmoja wao aliyekuwa anaonekana kutoa masimulizi muda mrefu akafyatuka kwamba;
"Siku mume wangu akifa, kesho yake naolewa. Tafadhali sana msije kuniuliza huyo mchumba nilimpata lini na wapi". "Tena natamani life hata leo hii ili nipate furaha, kwanini niendelee kuteseka kwa sababu ya limmbwa lisilojua thamani ya mke?" Life is nothing if i'm not happy (akaweka msisitizo kwa kidhungu)!!
Baada ya kusikia hivyo, sikutaka kuwa shahidi katika kesi inayoweza kumpa mtu life ban ama kitanzi, nikapiga funda la mwisho nikajiondokea zangu huku nikijiuliza huyo bwana kamkosea nini mkewe hadi amuombee kifo?
MYTAKE:
Akina dada na akina mama wa hapa JF naomba kufahamu kupitia kwenu, ni kosa gani huyu mume kamtenda mwenzenu hadi anamuombea kifo? Je tayari ameshapata mchumba/mume mwingine anasubiri tu kifo cha mumewe ili atimize ndoto zake?:scared::thinking: