Mukama na mbinu za kitoto Igunga

Molemo

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
14,534
13,225
Mwandishi Kulwa Karedia wa gazeti la Mtanzania leo jumapili amemuelezea Katibu mkuu wa ccm Wilson Mukama kama mtu aliyepoteza sifa za kuwa kiongozi wa CCM. Mukama ameshutumiwa kwa kutunga uongo ulio wazi kuhusu kwamba CHADEMA imeleta makomandoo kutoka nchi za kiislam na kuwaingiza Igunga. Mwandishi amesema Mukama amekosa mbinu za kisasa za kupambana na chadema na badala yake anatapatapa.

Mwandishi anaeleza vitendo vya ovyo na mbinu za kizamani za Mukama vitaiangamiza CCM mapema kuliko ilivyotarajiwa.Mwandishi anachambua inavyoelekea uchaguzi wa Igunga huenda ikawa kiama cha Mukama.

SOURCE MTANZANIA UK. 11
 
Aliyelala usimwamshe, ukimwamsha unaweza kulala wewe!! Waaache waendeleee kulala kwa kulewa kodi zetu, ipo siku moja watakumbuka wakati muda nao utakuwa umeshaisha.
 
Aliyelala usimwamshe, ukimwamsha unaweza kulala wewe!! Waaache waendeleee kulala kwa kulewa kodi zetu, ipo siku moja watakumbuka wakati muda nao utakuwa umeshaisha.

Kweli, mwacheni alale usingizi, hizo ofisi za CCM zitageuzwa kuwa baa muda si mrefu!
 
Back
Top Bottom