Mukama: Katibu Mkuu wa CCM atia aibu kwenye Msiba wa Bob pale Karimjee

salisalum

JF-Expert Member
Oct 27, 2010
418
136
Tuko hapa kwenye kutoa heshima za mwisho kwa Kiongozi aliyetukuka mwanamaendeleo Bob Nyanga Mohammed Makani. MC alitoa nafasi kwa mwakilishi wa CCM kutoa rambirambi. Akainuka Mkama akazoza kama kawaida yake. Anasema Marehemu makani alikuwa mtu safi na mwenye hekima, kama Chadema wangefuata mfano wake ingekuwa vizuri sana. Halafu akasema umakini na umahiri wake unathibitishwa na ukweli kwamba Makani aliweza kufanikiwa kuwa Katibu Mkuu miongoni mwa watu tisa waliotoka kanda moja ya nchi hii. Yaani kwamba pamoja na ukanda bado Makani aliweza kuchaguliwa kuwa katibu mkuu. Mkama alitaka wana msiba tuingie kwenye mambo ya kisiasa na kutuaminisha kuwa Chadema ni chama cha ukanda na ukabila.

Mwenyekiti Mbowe kwa utulivu na hekima ya hali ya juu, wakati wa zamu yake alitoa ufafanuzi wa kurekebisha kauli hiyo akisema, ''Mdomo huumba, si vema kauli hiyo iachwe hivi hivi bila kurekebishwa''. Mbowe alianza kutaja mtu mmoja mmoja kwa wale waanzilishi wa Chadema waliokuwepo siku ile ya kumpata katibu mkuu. Ilikuwa orodha ndefu kwa kweli, katika orodha hiyo walioonekana kutoka kanda ya kaskazini walikuwa ni Mzee Mtei, Mzee Kimesera na yeye Mbowe wakati huo akiongoza vijana.

Mkama ametia aibu sana kwanza kugeuza mahali pa msiba pawe pa malumbano ya kisiasa, pili alikuwa amevaa kofia ya kihuni kwenye hafla ya heshima na ibada kama hii, tatu kusema uongo, Nne kamdhalilisha Rais Kikwete ambaye zamu yake ilipofika yeye hakutaka kujiingiza kwenye ujinga wa katibu wake. Yeye amesema, ''Hapa ni mahali pa msiba, tumekuja kuwapa pole wafiwa na kuwaombea subira''.

Ninashauri CCM katika uchaguzi wao mkuu wafikirie kupata mtu mwenye hekima atakayeweza kubeba dhamana ya chama badala ya kubeba aibu ya chama. Vinginevyo tutaamini kuwa Chama chetu hakiwezi tena kuaminika kupewa dhamana ya kuongoza nchi. IMEKUWA AIBU SANA.
 
Mkama hana talent ya uongozi kwenye siasa, kwanza ni mtu wa jazba na pili anaonekana siasa alijifunzia ukubwani sema tu ana bahati! Sishangai kusikia hivyo!
 
Ndio maana Mukama haingei sana, bora hata angeongea Nape. Maana Mukama inaonekana hana busara ya kutosha..
 
Huyu jamaa alitakiwa awe nyumbani kwake analisha ng'ombe! sijui kwa nini walimteua kuwa katibu mkuu! jamaa hafai hata ukatibu kata!! Vapour zote za CCM kumbe yeye ndiyo huwa anamtuma katibu wa itikadi na uenezi.
 
mkama mvi nyingi kichwani lakini hamna kitu enzi zetu tulikua tunaambiwa "AKILI YAKO HAINA AKILI" ccm kama itaendela kujisifia hazina ya wazee na wazee wenyewe ni kama MKAMA, MAKAMBA na KINA MKAPA kazi wanayo
 
Mkama hana talent ya uongozi kwenye siasa, kwanza ni mtu wa jazba na pili anaonekana siasa alijifunzia ukubwani sema tu ana bahati! Sishangai kusikia hivyo!

Mkama hana tofauti na Nape wote wanatia kichefuchefu kabisa wakiongea. Asubuhi Nape kaanzisha uzi asubuhi na kuweka katikati maneno ya chuki, fitna na uchongonganishi.

CCM wasiwawaangalia kwa jicho la makini watajikuta pabaya zaidi.
 
Tuko hapa kwenye kutoa heshima za mwisho kwa Kiongozi aliyetukuka mwanamaendeleo Bob Nyanga Mohammed Makani. MC alitoa nafasi kwa mwakilishi wa CCM kutoa rambirambi. Akainuka Mkama akazoza kama kawaida yake. Anasema Marehemu makani alikuwa mtu safi na mwenye hekima, kama Chadema wangefuata mfano wake ingekuwa vizuri sana. Halafu akasema umakini na umahiri wake unathibitishwa na ukweli kwamba Makani aliweza kufanikiwa kuwa Katibu Mkuu miongoni mwa watu tisa waliotoka kanda moja ya nchi hii. Yaani kwamba pamoja na ukanda bado Makani aliweza kuchaguliwa kuwa katibu mkuu. Mkama alitaka wana msiba tuingie kwenye mambo ya kisiasa na kutuaminisha kuwa Chadema ni chama cha ukanda na ukabila.

Mwenyekiti Mbowe kwa utulivu na hekima ya hali ya juu, wakati wa zamu yake alitoa ufafanuzi wa kurekebisha kauli hiyo akisema, ''Mdomo huumba, si vema kauli hiyo iachwe hivi hivi bila kurekebishwa''. Mbowe alianza kutaja mtu mmoja mmoja kwa wale waanzilishi wa Chadema waliokuwepo siku ile ya kumpata katibu mkuu. Ilikuwa orodha ndefu kwa kweli, katika orodha hiyo walioonekana kutoka kanda ya kaskazini walikuwa ni Mzee Mtei, Mzee Kimesera na yeye Mbowe wakati huo akiongoza vijana.

Mkama ametia aibu sana kwanza kugeuza mahali pa msiba pawe pa malumbano ya kisiasa, pili alikuwa amevaa kofia ya kihuni kwenye hafla ya heshima na ibada kama hii, tatu kusema uongo, Nne kamdhalilisha Rais Kikwete ambaye zamu yake ilipofika yeye hakutaka kujiingiza kwenye ujinga wa katibu wake. Yeye amesema, ''Hapa ni mahali pa msiba, tumekuja kuwapa pole wafiwa na kuwaombea subira''.

Ninashauri CCM katika uchaguzi wao mkuu wafikirie kupata mtu mwenye hekima atakayeweza kubeba dhamana ya chama badala ya kubeba aibu ya chama. Vinginevyo tutaamini kuwa Chama chetu hakiwezi tena kuaminika kupewa dhamana ya kuongoza nchi. IMEKUWA AIBU SANA.

Amekosea nn sasa kusema ukweli ? hakuna kitu hapo kwenye thread yako aiseee
 
Mkama hana talent ya
uongozi kwenye siasa, kwanza ni mtu wa jazba na pili anaonekana siasa
alijifunzia ukubwani sema tu ana bahati! Sishangai kusikia
hivyo!

Huyu mustach wake tu unaonyesha jinsi alivyo mjinga!
Tabia zake za hovyo ikiwemo kutembea na wake za watu nidiyo ilikuwa sifa yake kuu alipokuwa jiji.

Magamba hawana watu, kiongozi gani huyu mpuuzi hivi!
 
Watanzania sasa tumepata confirmation juu nani muasisi wa siasa za kugawa wananchi kwa ukanda. Nilidhani yalikuwa maneno ya Nape lakini kwa kauli ya Mukama basi ni wazi propaganda hizi zimesukwa toka ngazi ya juu. Ni jambo la kusikitisha sana kuona Mukama anahubiri siasa za kibaguzi, siasa za kugawa watanzania na mbaya zaidi anahubiri huu upuuzi kwenye msiba - mbele ya mwili wa marehemu! Huu ni utamaduni mbaya sana na kila mtanzania anayeitakia mema hii nchi ni vema akalaani kauli ya Mukama.

NB: Ni Mukama huyu huyu aliwatangazia watazania wakati wa uchaguzi mdogo Igunda kuwa CHADEMA wameleta makomandoo toka Libya na Pakistan ili waje kuchafua nchi! Sijui kwa nini CCM wanaona huyu mzee bado anafaa kuongoza chama!
 
Mi nadhani Kauli yake ndio imemuumbua kuwa kumbe CDM haina ukabili muda mrefu... look here Mkani ndio alikuwa Katibu mkuu wa kwanza wa CHADEMA, ambaye ni MSUKUMA, akawa mwenyekiti MSUKUMA sasa hapo inakuwaje kuitwa ni chama cha kikabila?
 
Anawakilisha kundi kubwa la viongozi wa CCM, uwezo wao wa kufikiri ndio umefikia hapo
 
Huu ni uthibitisho dhahiri kwamba CHADEMA imewashika pabaya hawa magamba. Endapo kiongozi wa chama tawala anaamua kuacha decency na ustaarabu wetu wa kiafrika na kuanza kutoa mashambulizi ya kisiasa kwenye kadamnasi ya wafiwa, ujue mambo yanazidi kuwa magumu kwa CCM. Same stupidity has been written by Nape Nnauye kwenye post yake moja humu JF. CCM = Chama Mfu.
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Tuko hapa kwenye kutoa heshima za mwisho kwa Kiongozi aliyetukuka mwanamaendeleo Bob Nyanga Mohammed Makani. MC alitoa nafasi kwa mwakilishi wa CCM kutoa rambirambi. Akainuka Mkama akazoza kama kawaida yake. Anasema Marehemu makani alikuwa mtu safi na mwenye hekima, kama Chadema wangefuata mfano wake ingekuwa vizuri sana. Halafu akasema umakini na umahiri wake unathibitishwa na ukweli kwamba Makani aliweza kufanikiwa kuwa Katibu Mkuu miongoni mwa watu tisa waliotoka kanda moja ya nchi hii. Yaani kwamba pamoja na ukanda bado Makani aliweza kuchaguliwa kuwa katibu mkuu. Mkama alitaka wana msiba tuingie kwenye mambo ya kisiasa na kutuaminisha kuwa Chadema ni chama cha ukanda na ukabila.

Mwenyekiti Mbowe kwa utulivu na hekima ya hali ya juu, wakati wa zamu yake alitoa ufafanuzi wa kurekebisha kauli hiyo akisema, ''Mdomo huumba, si vema kauli hiyo iachwe hivi hivi bila kurekebishwa''. Mbowe alianza kutaja mtu mmoja mmoja kwa wale waanzilishi wa Chadema waliokuwepo siku ile ya kumpata katibu mkuu. Ilikuwa orodha ndefu kwa kweli, katika orodha hiyo walioonekana kutoka kanda ya kaskazini walikuwa ni Mzee Mtei, Mzee Kimesera na yeye Mbowe wakati huo akiongoza vijana.

Mkama ametia aibu sana kwanza kugeuza mahali pa msiba pawe pa malumbano ya kisiasa, pili alikuwa amevaa kofia ya kihuni kwenye hafla ya heshima na ibada kama hii, tatu kusema uongo, Nne kamdhalilisha Rais Kikwete ambaye zamu yake ilipofika yeye hakutaka kujiingiza kwenye ujinga wa katibu wake. Yeye amesema, ''Hapa ni mahali pa msiba, tumekuja kuwapa pole wafiwa na kuwaombea subira''.

Ninashauri CCM katika uchaguzi wao mkuu wafikirie kupata mtu mwenye hekima atakayeweza kubeba dhamana ya chama badala ya kubeba aibu ya chama. Vinginevyo tutaamini kuwa Chama chetu hakiwezi tena kuaminika kupewa dhamana ya kuongoza nchi. IMEKUWA AIBU SANA.

No wonder chama chenyewe kinaporomoka kwa kasi ya ajabu; yatakuwa maajabu ya Musa kutegemea mtu kama huyu mkama kukisaidia chama kuimarika. anyway the rule the game is "ONE MISTAKE ONE GOAL" acha waendeleee kufanya makosa ndio mtaji wa CDM.
 
Ndio maana Mukama haingei sana, bora hata angeongea Nape. Maana Mukama inaonekana hana busara ya kutosha..
Mkuu, Nape naye amekuja na ujinga huo huo!Som hapa!

Nakulilia Bob Nyanga Makani! Kuna wanasiasa wengi lakini Mzee Makani ni wa aina ya pekee! Kuna wanasheria wengi lakini si wa aina ya Bob Makani! Umepambana kuhakikisha siasa za Tanzania hasa za ndani ya Chama chako zinakuwa za kweli na zisizo na uongo, chuki na ubabaishaji! Bahati mbaya umeondoka wakati siasa hizo zilizokukera zikishika kasi kubwa kwenye Chama chako! Naamini Mungu atainua mwingine wa aina yako au zaidi yako, akiokoe Chama chako, ili kwa pamoja tujenge Demokrasia ya kweli nchini! TANZANIA KWANZA, UZELENDO KWANZA!

Nape Moses Nnauye
Chama Cha Mapinduzi
Katibu wa Itikadi & Uenezi Taifa
 
Back
Top Bottom