nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
* Huyu Mukama ni mgonjwa anasema Wananchi wajifunze ya Misri Eti Kuandamana kwao kama Chadema kumeashiria Nchi kuongozwa Kijeshi
Wednesday, 11 May 2011 11:11 newsroom
NA WAANDISHI WETU - GAZETI LA UHURU
KATIBU Mkuu wa CCM, Wilson Mukama, amemponda Dk. Wilbroad Slaa na kusema ni mwanasiasa anayejifunza. Amemfananisha Dk. Slaa ambaye ni Katibu Mkuu wa CHADEMA na mtu anayebadilisha dini na kujifanya mjuaji kuliko aliowakuta na matokeo yake anaropoka kila kukicha na kutoa matamshi ya vitisho kwa wananchi. Mukama alisema CCM inajadili mambo
yake kwa uwazi na kilichofanyika ni mabadiliko ya kukijenga upya Chama na si vinginevyo, na kwamba kwa kutoa maneno ya uzushi Dk. Slaa ni sawa na mtoto anayelilia wembe, siku moja utamkata. Pia, amesisitiza kwamba hakuna waraka wa siri.
Aliyasema hayo jana, wakati akifafanua kauli ya iliyotolewa na Dk. Slaa kupitia gazeti moja la kila siku lenye kichwa cha habari Dk. Slaa: Nchi haitatawalika, Anasa waraka wa siri wa CCM.
Katika gazeti hilo, Dk. Slaa alikaririwa akizungumza katika mkutano wa hadhara katika viwanja vya shule ya msingi Msakila mjini Sumbawanga ambapo alisema amebaini waraka wa siri wa CCM uliokuwa na muhuri wa SIRI ambao amedai CCM imekiri kuwa haikubaliki.
Mukama alisema Dk. Slaa, haelewi nini maana ya nchi kutotawalika kwani Tanzania ni nchi inayoendeshwa kwa misingi ya demokrasia, inawekezeka kiuchumi na wananchi wanaishi kwa amani na utulivu.
Dk. Slaa hana karama ya kutawala, kiongozi makini hupima hata matamshi yake, anazangumza mambo yenye mwelekeo wa kuwakosesha amani, lakiniwakati wao wakiendelea na maandamano, Serikali ya CCM inajenga miundombinu ya kusafirisha mazao, alisema.
Aliwataka wananchi wajifunze yanayotokea Misri, ambako wameandamana na sasa wanaongozwa na jeshi la nchi hiyo, kila siku watu 50,000 wanakamatwa na kuhukumiwa.
Alisema CHADEMA ni hodari wa kusema uongo, kwa kutumia haki yao ya kujieleza kusambaza uzushi na kwamba CCM haiwezi kushindana nao kwa kuzua mambo.
Mukama alisema wamekuwa wakiwapatia vijana sh. 500 kuwavuta kwenye maandamano na kuwadanganya kwamba watawaondolea umasikini kupitia maandamano hayo.
Akizungumzia kuhusu kupanda kwa bei za bidhaa, alisema chanzo ni matatizo ya kisiasa yaliyozikumba nchi za Magharibi ikiwemo Libya ambao ndio wenye visima vya mafuta, nishati hiyo imepanda bei katika soko la dunia, na viwanda vyote nchini vinaendeshwa kwa kutegemea mafuta.
Hakuna siri yoyote CCM, imejipanga kuboresha utendaji wa Chama kwa kuangalia vigezo vya msingi, na kila kimoja kimepitia kwenye vikao halali vya kikatiba, alisema.
Akifafanua Mukama alisema CCM si kundi la watu ama ukoo fulani kama ilivyo CHADEMA, bali ni Chama kinachoendeshwa kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake tangu enzi za TANU na ASP.
Alisema katika mkakati wa kufanya mageuzi CCM ilipanga kuboresha mambo muhimu, ikiwemo fikra na itikadi, muundo wake, viongozi wa Chama, watendaji, usalama na maadili, wanachama na kujiimarisha kiuchumi na fedha.
Mukama alisema vigezo hivyo vyote havina usiri bali ni mikakati ambayo imewekewa mipango ya utekelezaji kwa maana ya kuunda CCM yenye mwelekeo tofauti.
Alitoa mfano wa mambo yaliyobadilishwa ni kufanya uchaguzi wa Chama na jumuia kwa mwaka mmoja ili kupunguza muda wa kushughulikia uchaguzi kutoka miaka mitatu kwenda minne.
ÒMiaka mitano ya utawala, ni mwaka mmoja tu ndo hatufanyi uchaguzi, mwakani tuna uchaguzi wa Chama , tumeona tufanye pamoja na jumuia, ili tupumzike 2013, 2014 tubaki na uchaguzi wa serikali za mitaa na 2015 uchaguzi mkuu, alisema.
Alisema pia katika usalama na maadili, iliangaliwa viongozi na wanachama wanaotuhumiwa kwa rushwa na vitendo vingine viovu, ilionekana hawawezi kusimamia vitendo vya kimapinduzi ambavyo Chama kinavitekeleza.
Ni jambo la kawaida kufanya marekebisho hususan katika kipindi ambacho CCM inakubalika kwa wananchi, bado tuna nafasi kubwa hata katika uchaguzi wa 2010 imedhihirisha tumepata majimbo 187 mara tisa zaidi ya majimbo 22 ya CHADEMA, alisema.
Alisema matokeo ya uchaguzi huo yamebainisha kwamba CCM bado inakubalika kwani hata wabunge wa viti maalumu ambao hupatikana kutokana na wingi wa kura , CCM ina wabunge 67 na vyama vingine vina wabunge 35.
Hivi karibuni CCM ilifanya mabadiliko makubwa kwa kujivua gamba kwa baadhi ya viongozi waandamizi, walijizulu na kujipanga upya, ambapo nafasi ya Katibu Mkuu iliyoachwa wazi na Yussuf Makamba ilichukuliwa na Mukama.
Siku chache baada ya mabadiliko hayo, baadhi ya watuhumiwa wa ufisadi ndani ya CCM, walianza njama za kuwachafua viongozi waandamizi akiwemo Mwenyekiti wa Taifa, Rais Jakaya Kikwete.
Wednesday, 11 May 2011 11:11 newsroom
NA WAANDISHI WETU - GAZETI LA UHURU
KATIBU Mkuu wa CCM, Wilson Mukama, amemponda Dk. Wilbroad Slaa na kusema ni mwanasiasa anayejifunza. Amemfananisha Dk. Slaa ambaye ni Katibu Mkuu wa CHADEMA na mtu anayebadilisha dini na kujifanya mjuaji kuliko aliowakuta na matokeo yake anaropoka kila kukicha na kutoa matamshi ya vitisho kwa wananchi. Mukama alisema CCM inajadili mambo
yake kwa uwazi na kilichofanyika ni mabadiliko ya kukijenga upya Chama na si vinginevyo, na kwamba kwa kutoa maneno ya uzushi Dk. Slaa ni sawa na mtoto anayelilia wembe, siku moja utamkata. Pia, amesisitiza kwamba hakuna waraka wa siri.
Aliyasema hayo jana, wakati akifafanua kauli ya iliyotolewa na Dk. Slaa kupitia gazeti moja la kila siku lenye kichwa cha habari Dk. Slaa: Nchi haitatawalika, Anasa waraka wa siri wa CCM.
Katika gazeti hilo, Dk. Slaa alikaririwa akizungumza katika mkutano wa hadhara katika viwanja vya shule ya msingi Msakila mjini Sumbawanga ambapo alisema amebaini waraka wa siri wa CCM uliokuwa na muhuri wa SIRI ambao amedai CCM imekiri kuwa haikubaliki.
Mukama alisema Dk. Slaa, haelewi nini maana ya nchi kutotawalika kwani Tanzania ni nchi inayoendeshwa kwa misingi ya demokrasia, inawekezeka kiuchumi na wananchi wanaishi kwa amani na utulivu.
Dk. Slaa hana karama ya kutawala, kiongozi makini hupima hata matamshi yake, anazangumza mambo yenye mwelekeo wa kuwakosesha amani, lakiniwakati wao wakiendelea na maandamano, Serikali ya CCM inajenga miundombinu ya kusafirisha mazao, alisema.
Aliwataka wananchi wajifunze yanayotokea Misri, ambako wameandamana na sasa wanaongozwa na jeshi la nchi hiyo, kila siku watu 50,000 wanakamatwa na kuhukumiwa.
Alisema CHADEMA ni hodari wa kusema uongo, kwa kutumia haki yao ya kujieleza kusambaza uzushi na kwamba CCM haiwezi kushindana nao kwa kuzua mambo.
Mukama alisema wamekuwa wakiwapatia vijana sh. 500 kuwavuta kwenye maandamano na kuwadanganya kwamba watawaondolea umasikini kupitia maandamano hayo.
Akizungumzia kuhusu kupanda kwa bei za bidhaa, alisema chanzo ni matatizo ya kisiasa yaliyozikumba nchi za Magharibi ikiwemo Libya ambao ndio wenye visima vya mafuta, nishati hiyo imepanda bei katika soko la dunia, na viwanda vyote nchini vinaendeshwa kwa kutegemea mafuta.
Hakuna siri yoyote CCM, imejipanga kuboresha utendaji wa Chama kwa kuangalia vigezo vya msingi, na kila kimoja kimepitia kwenye vikao halali vya kikatiba, alisema.
Akifafanua Mukama alisema CCM si kundi la watu ama ukoo fulani kama ilivyo CHADEMA, bali ni Chama kinachoendeshwa kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake tangu enzi za TANU na ASP.
Alisema katika mkakati wa kufanya mageuzi CCM ilipanga kuboresha mambo muhimu, ikiwemo fikra na itikadi, muundo wake, viongozi wa Chama, watendaji, usalama na maadili, wanachama na kujiimarisha kiuchumi na fedha.
Mukama alisema vigezo hivyo vyote havina usiri bali ni mikakati ambayo imewekewa mipango ya utekelezaji kwa maana ya kuunda CCM yenye mwelekeo tofauti.
Alitoa mfano wa mambo yaliyobadilishwa ni kufanya uchaguzi wa Chama na jumuia kwa mwaka mmoja ili kupunguza muda wa kushughulikia uchaguzi kutoka miaka mitatu kwenda minne.
ÒMiaka mitano ya utawala, ni mwaka mmoja tu ndo hatufanyi uchaguzi, mwakani tuna uchaguzi wa Chama , tumeona tufanye pamoja na jumuia, ili tupumzike 2013, 2014 tubaki na uchaguzi wa serikali za mitaa na 2015 uchaguzi mkuu, alisema.
Alisema pia katika usalama na maadili, iliangaliwa viongozi na wanachama wanaotuhumiwa kwa rushwa na vitendo vingine viovu, ilionekana hawawezi kusimamia vitendo vya kimapinduzi ambavyo Chama kinavitekeleza.
Ni jambo la kawaida kufanya marekebisho hususan katika kipindi ambacho CCM inakubalika kwa wananchi, bado tuna nafasi kubwa hata katika uchaguzi wa 2010 imedhihirisha tumepata majimbo 187 mara tisa zaidi ya majimbo 22 ya CHADEMA, alisema.
Alisema matokeo ya uchaguzi huo yamebainisha kwamba CCM bado inakubalika kwani hata wabunge wa viti maalumu ambao hupatikana kutokana na wingi wa kura , CCM ina wabunge 67 na vyama vingine vina wabunge 35.
Hivi karibuni CCM ilifanya mabadiliko makubwa kwa kujivua gamba kwa baadhi ya viongozi waandamizi, walijizulu na kujipanga upya, ambapo nafasi ya Katibu Mkuu iliyoachwa wazi na Yussuf Makamba ilichukuliwa na Mukama.
Siku chache baada ya mabadiliko hayo, baadhi ya watuhumiwa wa ufisadi ndani ya CCM, walianza njama za kuwachafua viongozi waandamizi akiwemo Mwenyekiti wa Taifa, Rais Jakaya Kikwete.