Mukama aanza kwa Ushindi CCM

mkigoma

JF-Expert Member
Jul 26, 2011
1,180
309
Katibu mkuu mpya wa chama tawala CCM ameanza kwa ushindi katika jimbo la igunga toka achaguliwe ndio uchaguzi wa kwanza kwa nafasi ya ubunge toka achaguliwe, Je? hii ni hatua nzuri kwa chama cha Mapinduzi kuelekea uchaguzi mkuu wa 2015.
 
Katibu mkuu mpya wa chama tawala CCM ameanza kwa ushindi katika jimbo la igunga toka achaguliwe ndio uchaguzi wa kwanza kwa nafasi ya ubunge toka achaguliwe, Je? hii ni hatua nzuri kwa chama cha Mapinduzi kuelekea uchaguzi mkuu wa 2015.
Bila kumsahau NAPE pia. Hawa wawili ndio tegemeo la CCM kwa sasa. Mungu awabariki.
 
ccm yashindwa kwa asilimia 53, inaongoza wapinzani hii ni kutokana na kushindwa chini ya asilima 50.
 
Katibu mkuu mpya wa chama tawala CCM ameanza kwa ushindi katika jimbo la igunga toka achaguliwe ndio uchaguzi wa kwanza kwa nafasi ya ubunge toka achaguliwe, Je? hii ni hatua nzuri kwa chama cha Mapinduzi kuelekea uchaguzi mkuu wa 2015.

Mukama ni strategist sana ana tumia akili nyingi na nguvu chache, tofauti na makatibu wakuu wengine wa vyama vya upinzani km slaa nguvu nyingi akili chache.
 
Mukama ni strategist sana ana tumia akili nyingi na nguvu chache, tofauti na makatibu wakuu wengine wa vyama vya upinzani km slaa nguvu nyingi akili chache.

Kwa jinsi unavyomkubali Dr. Slaa umeamua hadi kutumia picha yake... Action speaks louder than words, tumekuelewa kuwa hayo maneno ni porojo ila ukweli unao moyoni.
 
Katibu mkuu mpya wa chama tawala CCM ameanza kwa ushindi katika jimbo la igunga toka achaguliwe ndio uchaguzi wa kwanza kwa nafasi ya ubunge toka achaguliwe, Je? hii ni hatua nzuri kwa chama cha Mapinduzi kuelekea uchaguzi mkuu wa 2015.

Unashindwa kutofautisha ushindi na wizi, we kweli una akili ya mbayuwayu!
 
katibu mkuu mpya wa chama tawala ccm ameanza kwa ushindi katika jimbo la igunga toka achaguliwe ndio uchaguzi wa kwanza kwa nafasi ya ubunge toka achaguliwe, je? Hii ni hatua nzuri kwa chama cha mapinduzi kuelekea uchaguzi mkuu wa 2015.

Ndugu yangu hajafanya uchambuzi wa kutosha.

Kashinda uchaguzi gani? Kwani hilo jimbo lilikuwa la chama gani, sio ccm? Ukilinganisha uchaguzi uliopita na wa sasa hivi ni uchaguzi gani ccm ilipata kura nyingi(asilimia kubwa). Ukilinganisha uchaguzi wa mwaka jana na huu wa juzi ni uchaguzi upi ccm imetumia rasilimali nyingi (watu, pesa , vifaa, vitisho, ulaghai, ghiliba n.k)? Ukijibu haya maswali pamoja na mingine kama haya basi ndio utajua kama kashinda uchaguzi au kashindwa.
 
Kwa jinsi unavyomkubali Dr. Slaa umeamua hadi kutumia picha yake... Action speaks louder than words, tumekuelewa kuwa hayo maneno ni porojo ila ukweli unao moyoni.

Si umeona jezi aliyovaa ni ya timu gani ? hilo ndilo chama la ushindi
 
Ndugu yangu hajafanya uchambuzi wa kutosha.

Kashinda uchaguzi gani? Kwani hilo jimbo lilikuwa la chama gani, sio ccm? Ukilinganisha uchaguzi uliopita na wa sasa hivi ni uchaguzi gani ccm ilipata kura nyingi(asilimia kubwa). Ukilinganisha uchaguzi wa mwaka jana na huu wa juzi ni uchaguzi upi ccm imetumia rasilimali nyingi (watu, pesa , vifaa, vitisho, ulaghai, ghiliba n.k)? Ukijibu haya maswali pamoja na mingine kama haya basi ndio utajua kama kashinda uchaguzi au kashindwa.

Chadema wamebomoa benki kwa uchaguzi wa igunga, kwenye akaunti zao hakuna kitu Tshs 1.345bn zimetumika na hawakupata kitu. Pesa hizi zingetosha kufungua matawi zaidi ya 300. CCM oyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee !
 
Ndugu yangu hajafanya uchambuzi wa kutosha.

Kashinda uchaguzi gani? Kwani hilo jimbo lilikuwa la chama gani, sio ccm? Ukilinganisha uchaguzi uliopita na wa sasa hivi ni uchaguzi gani ccm ilipata kura nyingi(asilimia kubwa). Ukilinganisha uchaguzi wa mwaka jana na huu wa juzi ni uchaguzi upi ccm imetumia rasilimali nyingi (watu, pesa , vifaa, vitisho, ulaghai, ghiliba n.k)? Ukijibu haya maswali pamoja na mingine kama haya basi ndio utajua kama kashinda uchaguzi au kashindwa.

Kama lilikuwa la CCM kwa nini CHADEMA waliweka Mgombea na kutumia fedha nyingi ikiwamo kukodi Helkopta na kutumia nguvu ya viongoziu wake wakuu akiwamo Mwenyekiti Mbowena Katibu Mkuu Slaa?
 
Ni Mukama au Mkapa na Mangula wanasiasa wasio na makundi ndo waliookoa jahazi angeenda Jk na mukama pekee muone kama wanaigunga wasingewaCUF.
 
Katibu mkuu mpya wa chama tawala CCM ameanza kwa ushindi katika jimbo la igunga toka achaguliwe ndio uchaguzi wa kwanza kwa nafasi ya ubunge toka achaguliwe, Je? hii ni hatua nzuri kwa chama cha Mapinduzi kuelekea uchaguzi mkuu wa 2015.

nimesema mahala pengine na ninarudia hapa tena.....wana ccm wenye akili (kama bado wapo) wametiwa hofu sana na matokeo ya igunga...hususani wakifikiria mustakabali wa chama chao 2015!
 
Chadema wamebomoa benki kwa uchaguzi wa igunga, kwenye akaunti zao hakuna kitu Tshs 1.345bn zimetumika na hawakupata kitu. Pesa hizi zingetosha kufungua matawi zaidi ya 300. CCM oyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee !

Nimegundua wewe ni sinker/stimker na wala siyo thinker .KIla mara unaleta ushabiki na hoja kujaza space bure wanao kujibu bora watumie muda wao kuangalia maswala ya maana.Maana unabisha tu sijui umerogwa au sijui kitu gani .CCM hawawezi kujivunia ushindi w Igunga na kwingineko.Ngojeaa kesi iende mahakamani uone moto .
 
Katibu mkuu mpya wa chama tawala CCM ameanza kwa ushindi katika jimbo la igunga toka achaguliwe ndio uchaguzi wa kwanza kwa nafasi ya ubunge toka achaguliwe, Je? hii ni hatua nzuri kwa chama cha Mapinduzi kuelekea uchaguzi mkuu wa 2015.

Unauliza ndevu kwa marehemu Osama?
 
Nimegundua wewe ni sinker/stimker na wala siyo thinker .KIla mara unaleta ushabiki na hoja kujaza space bure wanao kujibu bora watumie muda wao kuangalia maswala ya maana.Maana unabisha tu sijui umerogwa au sijui kitu gani .CCM hawawezi kujivunia ushindi w Igunga na kwingineko.Ngojeaa kesi iende mahakamani uone moto .

Mmechanganyikiwa sana tangia jana , poleni sana yabidi tuwasamehe. Ndivyo mmekuja kujiliwaza na kutamka mahakamani ili wanachama wenu wasiwaone vibonde kwa kupigwa ngwara ? Dah igunga mlikuwa mnaitamani sana na mliwekeza sana ila wananchi ndio wameamua kwenye uchaguzi huru na wa haki
 
Ni Mukama au Mkapa na Mangula wanasiasa wasio na makundi ndo waliookoa jahazi angeenda Jk na mukama pekee muone kama wanaigunga wasingewaCUF.

Hao wote uliowataja ni CCM na ndio miongoni mwa jeshi la ccm
 
WATANZANIA TUNAPIGA SANA KURA ISIPOKUA WALE WAPIGA KURA MARUANI SIKU ZOTE WANATUZIDI IDADI WAPIGA KURA TULIOHAI, NA MTAJI WA CCM KUTISHA WANANCHI

Wa-Tanzania tunnapiga sana kura isipokua wale Wa-Tanzania WAFU WASIOONEKANA ni wengi zaidi kuliko wale wanaoonekana kwa macho na wenye uamuzi kuchagua kukipigia kura chama tofauti na CCM.

Hivi karibuni kumeibuka aina ya demokrasia mpya nchini ya (1) demokrasia ya Bastola kiunoni kwenye kampeni za kisiasa, (2) Matumizi ya maruani kwenye daftari la wapiga kura ambalo ni miliki ya CCM tu, (3) uhuru wa rushwa za mapishi na nafaka kwenye kampeni, na hivi sasa (4) ubunifu mpya kwa CCM kuibuka na fesheni mpya ya
'CCM GREENGUARD MUNGIKI' na utekaji, uchomaji nyumba za watu ubakaji na kadhalika.

Hivyo ni muhimu ikawekwa kwamba
DAFTARI LA WAPIGA KURA liwe likifanyiwa uhakiki na CHOMBO HURU kinachokubalika na vyama vyote vya siasa nchini.

Vile vile ni vema utaratibu ukawepo wa wazi zaidi kwamba uchaguzi wowote unapoitishwa katika jimbo lolote lile basi ni sharti vyama vyote vitakavyoshiriki uchaguzi huo vishiriki moja kwa moja kufanya uhakiki mwingine, hata kama uhakiki wa kile chombo huru kilimalizika tu jana yake, ili kuwepo na uwanja sawa kwa waashiriki wote kwa wakati husika.

Huwezi kumridhisha mtu yeyote aakilini kwamba daftari la wapiga kura aliloliacha Rais Mstaafu Mkapa zaidi ya miaka kumi iliopita ndio bado hutumika kuendeshea uchaguzi mpaka leo kwa kuwa watakaokua wamekufa ni wengi sana hapo kati kati ambo majina yao yafaa kuondolewa kwenye daftari hilo kabla CCM inayohodhi utunzaji wa daftari hajaamua kutumia faida ya WAFU KUTOWEZA KUJIELEZA hivyo kuelekeza kura zao zote kwake jinsi apendavyo.

Na huo ndio demokrasia ya CCM miaka yote huku akiwatisha na wale waapiga kura wachache waalio hai wasijitokeze.

Kwa misingi hii inamaanisha kwamba Tanzania hatujawahi kuwa na kitu
FREE AND FAIR ELECTIONS isipokua geresha tu.

Katibu mkuu mpya wa chama tawala CCM ameanza kwa ushindi katika jimbo la igunga toka achaguliwe ndio uchaguzi wa kwanza kwa nafasi ya ubunge toka achaguliwe, Je? hii ni hatua nzuri kwa chama cha Mapinduzi kuelekea uchaguzi mkuu wa 2015.
 
Katibu mkuu mpya wa chama tawala CCM ameanza kwa ushindi katika jimbo la igunga toka achaguliwe ndio uchaguzi wa kwanza kwa nafasi ya ubunge toka achaguliwe, Je? hii ni hatua nzuri kwa chama cha Mapinduzi kuelekea uchaguzi mkuu wa 2015.

Ameshinda tenda ya kuwanunua CUf
 
chadema wamebomoa benki kwa uchaguzi wa igunga, kwenye akaunti zao hakuna kitu tshs 1.345bn zimetumika na hawakupata kitu. Pesa hizi zingetosha kufungua matawi zaidi ya 300. Ccm oyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee !

usema chadema wametumia bil 1.345 je una ushahidi?
Hata kama unashahidi kwa wametumia shilingi hizo unazosema, je data za kuthibitisha kuwa pesa kwa hizo zinaweza kufungua matawi zaidi ya 300? Unaposema kufungua matawi una maana gani? Kujenga ofisi au kujenga sehemu tu ya kuweka bendera? Ua unamaanisha nini haswa?

Pili, je CCM nayo imetumia shilingi ngapi kwenye huo uchaguzi?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom