Muhimu: Orientation course for non great thinkers here in JF!

Waberoya

Platinum Member
Aug 3, 2008
15,169
10,783
Ndugu wana JF,

Kumezuka kundi la watu Fulani aidha kwa kujua au kutojua wanaliharibu jukwaa la JF ambalo kwa muda mrefu limejizolea heshima sana, si kwa matusi bali kwa hoja na vithibitisho


HIDDEN ID
Unapotukana mtu usiyemjua, usiyemuona, eti kwa sababu ya mmeshindwana hoja ni ulimbukeni na utoto wa hali ya juu sana. Kumshinda mtu aliyekinyume na mwazo yako inahitaji convicing power ambayo inapatikana kwa hoja yenye nguvu tu. Matusi na name calling huwa haviwabadilishi watu popote pale dunia hii!!! Tena kibaya zaidi kwa watu wasioonekana!

KUJUA MSIMAMO WA MTU

Kuna button ya kujua previous posts za mtu husika kama uko interested kujua misimamo yake.Lakini ijulikane kama tunataka uandishi uliotukuka kuna watu umu huwa hawazungumzi au kuandika kwa kumaanisha directly walichoandika. Kwa bahati mbaya kizazi cha sasa hivi hakijuia uandishi huu wa mafumbo, kufikirisha, na MTU ANACHOTAFSIRI NI ile maana isiyo halisia. Kizazi hili ambacho wengi kwa sasa wanaitwa JF-kata wengi wao (sio wote) hawajui na imewapelekea kuleta conclusionza ajabu sio tu kwa kuharibu jukwaa bali kwa kuumiza mioyo na nafsi za watu

OLD-JF HELPS

Ukitaka kujua forums ina maana gani , ilikuwaje mpaka ikapata sifa, kuna thread nyingi sana za miaka iliyopita za members wengi ambao kwa sasa hawapo, zipitieni hizo na unaweza kuji-evaluate kama kweli unayo thinking capacity ya kuitwa great thinkers, if you are not one of them, KINDLY LEAVE! IF YOU THINK YOU CAN FIT THE STATUS please do needful, PEOPLE OUT THERE WILL LOVE TO SEE YOUR KIND VALUABLE AND EDUCATIVE POSTS NA siyo matusi, name calling na conclusion ambazo sio tu zinadhalilisha au kuwaumiza mnaowatukana ila zinaweka questiona mark nyingi za mrusha post kama kweli ni great thinker.

Michango imekuwa mibaya sana kwa ( June 2010-2011 baadhi ya members)

Till then.
 
Nashukuru kwa angalizo Mkuu,, ni matumaini yangu kuwa wengi tutajifunza kitu kwenye hili angalizo..
 
Swahiba ni kweli kabisa...

I think the move is intentional na lengo lake ni ku-dilute every good move inayofanywa na wana JF wa ukweli...

If we stand firm yatakwisha lakini nadhnai kuna haja ya restricted registration to the new members kwakweli...:washing:

United we stand, divided we fall...
 
Ni kweli mkuu baadhi yetu tumekuwa hatuheshimu mawazo ya wenzetu na badala yake conclusion inakuwa matusi. Imeshazungumzwa hapa mara nyingi kwamba ukiona huna cha kuchangia ni bora ukae kimya kulilko kutukana mtu usiyemjua waweza kumtukana hata baba yako bila kujua. Mijadala popote duniani ni kuvumiliana.
 
Aisee hii kozi ni muhimu sana ila kwa uvivu wetu wa kusoma sidhani kama itasaidia.
 
Umesikika mkuu,

Hivi karibuni umejitokeza sana kutoa wito kwa watoa hoja mbali mbali kutumia majukwaa ya JF kufanya uchambuzi makini wenye kuzingatia hoja. Kimsingi hapa nakubaliana kabisa na wewe, hamna shida.

Hoja nzuri sana bado zinakuja na zile ambazo hazina mashiko nazo zipo. Nachelea kusema ubora wa uchambuzi wa hoja bado upo ila mara nyingine inabidi uokoteze koteze kwa vile wapenda mzaha nao wameongezeka. Lakini mimi naona hali hii ni ya kawaida kwa sababu watu wote hatuwezi kuwa sawa. Misingi yetu ni tofauti kimakuzi, kiimani, kielimu na kimapato. Bahati nzuri mtu makini hupati shida kuwatofautisha watu mbali mbali humu ndani ya majukwaa ya JF.

Kitu kimoja kikubwa kuelewa ni kwamba JF imekua na umaarufu wake umekuwa ukiongezeka sana kadri siku zinavyokwenda. Sasa kwa mtazamo wangu hizi ni changamoto ambazo JF itakabiliana nazo sasa na hapo baadaye.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom