Gamba la Chuma
JF-Expert Member
- Feb 11, 2012
- 1,243
- 340
Peeeoples ................ Nianze kwa kusema ID yangu isiwape tabu, nimehamia CDM juzi. Nimeona baadhi ya wana JF wanajaribu kujiuliza kilichoiangusha CCM Arumeru. Ukweli ni kuwa hata hizo kura chache walizopata CCM wamejitahidi sana. Mara nyingi ushindi wa CCM hutokana na hujuma, kununua mawakala, rushwa, kucheza na daftari la kura, vitisho na matumizi makubwa ya nguvu na rasilimali za serilali/umma. Arumeru Chadema wameweza kudhibiti mambo hayo japo sio kwa 100%. Ushindi wa Chadema hautokani na kupiga kura, bali kulinda kura. Ni kwa mantiki hiyo, naweza kusema kuwa Chadema huwa wanashinda siku zote. Walishinda Uraisi, walishinda Ubunge kwa Pinda, walishinda Segerea, walishinda Kibaha kwa Koka, walishinda zaidi ya 70% ya majimbo ya Tanzania na hata Igunga naamini walishinda. Tatizo ni kulinda kura. Ili hili lifanikiwe, sasa tuelekeze nguvu kwenye Katiba mpya, itupe tume huru ya uchaguzi. Hili ni la muhimu sana kwa ukombozi wa taifa letu. Viva CHADEMA.