Muhimbili: Aliyepasuliwa kichwa MOI apooza upande

Zee la shamba

Member
Oct 17, 2007
55
3
Na Jackson Odoyo

MGONJWA Emmanuel Didas aliyefanyiwa upasuaji wa kichwa badala ya mguu Novemba Mosi, mwaka huu katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) amepooza upande mmoja wa mwili wake.


Akizungumza na mwandishi wa Mwananchi ndugu wa mgonjwa huyo ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini kwa kuwa si msemaji wa familia, alisema licha ya kuwa ndugu yake hajaanza kuzungumza, kukaa wala kutembea pia hivi sasa amepooza upande mmoja, suala ambalo pia lilithibitishwa na baadhi ya madaktari bingwa wa upasuaji katika taasisi hiyo.


Alisema baada ya kugundua hali hiyo walimuuliza daktari anayemuhudumia aliyemtaja kwa jina moja la Dk Kinasha ambaye alikiri kwamba hali hiyo haiwezi kutibiwa kwa sasa, badala yake wanajaribu kumfanyia uchunguzi wa kina ili aweze kurudia hali yake ya kawaida.


?Pamoja na matatizo aliyonayo ya kutoweza kuzungumza, kukaa wala kutembea pia amepooza upande mmoja hali hiyo inazidi kutupa wasiwasi kama kweli ataweza kupona, kwa sababu kila kukicha kuna matatizo mapya yanaibuka, na tukiwauliza madaktari hawatupi majibu ya uhakika,? alisema ndugu wa mgonjwa huyo.


Alifafanua kwamba hivi sasa wana mikakati ya kumuona Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Profesa David Mwakyusa kwa mazungumzo ya kina kuhusiana suala hilo, ikiwa ni pamoja na kupata ushauri wa kitaalam.


Aliongeza kwa sasa wanafamilia hawajaamua la kufanya kwasababu uongozi wa taasisi hiyo uliwaomba wasubiri mpaka tume iliyoundwa na Mkurugenzi wa MOI, Profesa Laurent Museru kuchunguza tukio hilo itakapotoa taarifa yake.


Mbali na madai hayo ya ndugu, mwandishi wa habari hizi pia alizungumza na baadhi ya madaktari bingwa wa upasuaji katika taasisi hiyo (majina yamehifadhiwa) ambao walithibitisha kwamba mgonjwa huyo kapooza.


Mbali na mgonjwa huyo pia mwenzake Emmanuel Mgaya ambaye alifanyiwa upasuaji wa mguu badala ya kichwa alitegemewa kufanyiwa upasuaji wa kichwa jana ili kutibu tatizo linalomsumbua.


Kwa mujubu wa ndugu wa karibu wa mgonjwa huyo aliyezungumza na mwandishi wa habari hizi, Mgaya alitakiwa kufanyiwa upasuaji wa kichwa jana.


Taarifa hizo zilizotolewa na baadhi ya madaktari wa taasisi hiyo zinasema kuwa Mkurugenzi wa taasisi hiyo aliwatangazia kwenye kikao chao cha utendeji cha asubuhi kwamba mgonjwa huyo alitakiwa kufanyiwa upasuaji wa kichwa jana.


Alisema kwamba mbali na tangazo hilo pia alitangaza kuwasimamisha kazi watu wawili ambao ni daktari aliyetakiwa kumfanyia Emmanuel Didas upasuaji wa mguu kwasababu mgonjwa huyo hakuwa kwenye orodha ya wagonjwa waliotakiwa kufanyiwa upasuaji siku hiyo.


Mwingine aliyesimamishwa kazi kwa muda usiojulikana ni mwandaaji wa orodha ya wagonjwa wanaotakiwa kufanyiwa upasuaji kwakutoingiza jina la mgonjwa huyo katika orodha.


Upasuaji huo tata, ulilazimisha Bodi ya MOI, kuagiza uongozi kuunda Tume kwa ajili ya kuchunguza tukio hilo. Tayari Tume imeshamaliza kazi na kuwasilisha ripoti yake kwa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii kwa ajili ya hatua zaidi.

Source: mwananchi Newspaper
 
I see it as a system problem, rather than individual health worker problem.
 
Na Jackson Odoyo

MGONJWA Emmanuel Didas aliyefanyiwa upasuaji wa kichwa badala ya mguu Novemba Mosi, mwaka huu katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) amepooza upande mmoja wa mwili wake.


Akizungumza na mwandishi wa Mwananchi ndugu wa mgonjwa huyo ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini kwa kuwa si msemaji wa familia, alisema licha ya kuwa ndugu yake hajaanza kuzungumza, kukaa wala kutembea pia hivi sasa amepooza upande mmoja, suala ambalo pia lilithibitishwa na baadhi ya madaktari bingwa wa upasuaji katika taasisi hiyo.


Alisema baada ya kugundua hali hiyo walimuuliza daktari anayemuhudumia aliyemtaja kwa jina moja la Dk Kinasha ambaye alikiri kwamba hali hiyo haiwezi kutibiwa kwa sasa, badala yake wanajaribu kumfanyia uchunguzi wa kina ili aweze kurudia hali yake ya kawaida.


?Pamoja na matatizo aliyonayo ya kutoweza kuzungumza, kukaa wala kutembea pia amepooza upande mmoja hali hiyo inazidi kutupa wasiwasi kama kweli ataweza kupona, kwa sababu kila kukicha kuna matatizo mapya yanaibuka, na tukiwauliza madaktari hawatupi majibu ya uhakika,? alisema ndugu wa mgonjwa huyo.


Alifafanua kwamba hivi sasa wana mikakati ya kumuona Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Profesa David Mwakyusa kwa mazungumzo ya kina kuhusiana suala hilo, ikiwa ni pamoja na kupata ushauri wa kitaalam.


Aliongeza kwa sasa wanafamilia hawajaamua la kufanya kwasababu uongozi wa taasisi hiyo uliwaomba wasubiri mpaka tume iliyoundwa na Mkurugenzi wa MOI, Profesa Laurent Museru kuchunguza tukio hilo itakapotoa taarifa yake.


Mbali na madai hayo ya ndugu, mwandishi wa habari hizi pia alizungumza na baadhi ya madaktari bingwa wa upasuaji katika taasisi hiyo (majina yamehifadhiwa) ambao walithibitisha kwamba mgonjwa huyo kapooza.


Mbali na mgonjwa huyo pia mwenzake Emmanuel Mgaya ambaye alifanyiwa upasuaji wa mguu badala ya kichwa alitegemewa kufanyiwa upasuaji wa kichwa jana ili kutibu tatizo linalomsumbua.


Kwa mujubu wa ndugu wa karibu wa mgonjwa huyo aliyezungumza na mwandishi wa habari hizi, Mgaya alitakiwa kufanyiwa upasuaji wa kichwa jana.


Taarifa hizo zilizotolewa na baadhi ya madaktari wa taasisi hiyo zinasema kuwa Mkurugenzi wa taasisi hiyo aliwatangazia kwenye kikao chao cha utendeji cha asubuhi kwamba mgonjwa huyo alitakiwa kufanyiwa upasuaji wa kichwa jana.


Alisema kwamba mbali na tangazo hilo pia alitangaza kuwasimamisha kazi watu wawili ambao ni daktari aliyetakiwa kumfanyia Emmanuel Didas upasuaji wa mguu kwasababu mgonjwa huyo hakuwa kwenye orodha ya wagonjwa waliotakiwa kufanyiwa upasuaji siku hiyo.


Mwingine aliyesimamishwa kazi kwa muda usiojulikana ni mwandaaji wa orodha ya wagonjwa wanaotakiwa kufanyiwa upasuaji kwakutoingiza jina la mgonjwa huyo katika orodha.


Upasuaji huo tata, ulilazimisha Bodi ya MOI, kuagiza uongozi kuunda Tume kwa ajili ya kuchunguza tukio hilo. Tayari Tume imeshamaliza kazi na kuwasilisha ripoti yake kwa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii kwa ajili ya hatua zaidi.

Source: mwananchi Newspaper

Simply mind boggling! This tragic case elevates Bantu incompetency and inefficiency to a whole new level!! Even pissy nursery school kids could have come up with a better diagnosis. Never ever put your life under trust of these insane Bantu daktaris.
 
Hii kitu nchi zenye sheria za maana, muda kama huu kunakuwa na law suit kama tano hivi.
Blanda katika udaktari ipo duniani kote, sema law suit inapunguza huu ushenzi. Yaani mnasue kiasi kwamba huyo dk kila cent anayo make mpaka anakufa familia inachukua 70%.
 
mtanganyika umenena,ila bongo ndio imetoka ni sawa na ajali kazini.
nilisoma kwenye md,kuwa ripoti itawekwa adharani leo je kunaaliye pata kunusa au ndio bado siri ya sirikali
 
Katibu tarafa, nani alikwambia Tanzania tunatoaga riport hadharani? labda hii ya madini kwa sababu Zitto yumo! Just thinking loud!!!!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom