MUHAS why Kikwete and not Karume??

Jackbauer

JF-Expert Member
Oct 28, 2010
6,038
2,199
Jana tulishuhudia Muhimbili University of Health and Allied Sciences(MUHAS) Wakimtunukia mh kikwete honorary degree,kwenye fani ya afya ya jamii(public health).kwa ufahamu wangu fani hii ni muhimu sana hasa ukizingatia inavyopambana na magonjwa kwa ujumla wake.inaangalia ni jinsi gani tunavyoweza kupambana na magonjwa kwa kuangalia mazingira na tabia za watu(jamii),haiangalii mgonjwa mmoja bali jamii yote kwa ujumla wake.ni hivi karibuni tumesikia Zanzibar imefanikiwa kueradicate(kuondoa kwa kiwango cha juu) ugonjwa wa malaria.mafanikio haya yameletwa na wadau mbalimbali wa afya,lakini ni ukweli usiopingika mafanikio haya yamekuja kutokana na comitment waliokuwanayo viongozi wa kisiasa kule zanzibar wakiongozwa na mh Abed Karume.nashangaa kwa nini MUHAS wameshindwa kutambua mchango wa Karume katika mafanikio haya.nabaki nikijiuliza WHY KIKWETE NA SIO KARUME?JE HUU NI MUENDELEZO WA UTEKAJI NYARA WA SIASA KATIKA TAASISI ZETU ZA KITAALUMA?binafsi naona ni upuuzi mwingine wa kuwakatisha tamaa watu wenye nia ya kweli ya kuleta maendeleo katika Tanzania.
Nawasilisha...
 
Back
Top Bottom