Mzalendo80
JF-Expert Member
- Oct 30, 2010
- 2,508
- 1,338
Unafiki hauwezi kumsitiri mtu mbele ya aibu anayoitengeneza. Tatizo sioi Bakwata kama chombo. Tatizo ni watu wanaoziongoza taasisi hizi. Njaa kali halafu wanatetea hata makosa ambayo dini zetu zinasema bayana kuwa ni dhambi mbele ya mungu. Ndo hapo sasa unafiki unaposhindwa kutusitiri!!!
Waislamu hapa Tanganyika hatuna umoja, Ramadhani tunafunga tofauti, kusheherekea sikukuu tunashehereka tofauti, sijui kwanini hatukai chini kumaliza tofauti zetu. Kazi kulalamika kuwa tunaonewa, tunakandamizwa hatupewi haki. Tutaishimiwa vipi wakati sisi wenyewe bado tuna migogoro? Misikiti mingi hapa Tanganyika kuna migogoro ya kijinga