Mufti ataka Waislamu waiombee dua Libya

kilimasera

JF-Expert Member
Dec 2, 2009
3,068
268
MUFTI wa Tanzania, Shehe Mkuu Issa bin Shaaban Simba amewataka Waislamu kuwaombea dua wenzao waliouawa katika vita inayoendelea Libya na wengine wanaodhulumiwa haki zao duniani.

Alitoa mwito huo kwenye hotuba yake katika Msikiti wa Gaddafi mjini Dodoma mwishoni mwa wiki.

Alisisitiza waumini wamwombee Kiongozi wa Libya, Kanali Muammar Gaddafi ambaye amekuwa msaada mkubwa kwa Waislamu duniani na wanyonge katika nchi zote bila kujali kama ni za Kiislamu.

Mufti Simba alisema maadui wa Waislamu wanachochea watu wakorofi kuanzisha fujo na vurugu kwa kuwaunga mkono ili misaada inayotolewa na kiongozi wa Libya duniani kote ifikie mwisho.

“Sisi hapa Dodoma tumepata msaada mkubwa kutoka Libya ni huu msikiti tuliuomba na tukaupata bila matatizo,” alisema Mufti Simba.

Hata hivyo, alisema maombi yamewezesha maadui wa Gaddafi waliolenga kupiga nyumba yake kumkosa kwa kuwa ana hifadhi ya Mwenyezi Mungu kwa kuwa ibada anazofanya ni kubwa na ni mtu aliyehifadhi Kurani katika mwili wake.

Aliyashutumu mataifa makubwa ya Magharibi kwa kuelekeza vita nguvu zao kuipiga Libya kwa kutoa mali kuwasaidia waasi.

Wakati huo huo, Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mustafa Shaaban aliwahimiza waumini kulinda utamaduni na kuenzi ustaarabu wa Kiislamu kwa kuepuka sera na utamaduni wa nchi za Magharibi unaolenga kutumia nguvu kuathiri mila na desturi za Kiafrika.

Alisema utamaduni wa Magharibi unalenga kuvuruga tabia za vijana kwa kuwafanya waige mambo yanayokiuka maadili.

Alitoa mwito wa kuiga mfano wa China na Japan zilizokataa kufuata sera na utamaduni wa nje na hivyo kuweza kupiga hatua ya maendeleo.
 
MUFTI wa Tanzania, Shehe Mkuu Issa bin Shaaban Simba amewataka Waislamu kuwaombea dua wenzao waliouawa katika vita inayoendelea Libya na wengine wanaodhulumiwa haki zao duniani. Huyu jamaa vipi? Dua lilihitajika kwa Osama!
 
Anayepaswa kuombewa ni yeye Mufti ambaye anachanganywa na vijisenti toka kwa Gadaffi kiasi cha kutaka kuuingiza umma kwenye utumwa wake wa pesa. Koma mufti tafadhali.
 
MUFTI wa Tanzania, Shehe Mkuu Issa bin Shaaban Simba amewataka Waislamu kuwaombea dua wenzao waliouawa katika vita inayoendelea Libya na wengine wanaodhulumiwa haki zao duniani. Huyu jamaa vipi? Dua lilihitajika kwa Osama!
Huyu mzee bana yaani hoja zake ni afadhali ya mwanangu gaude anayesoma chekechea!gadhafi kahifadhi korani mwilini mwake?duuh kazi kweli kweli
 
Ndiyo. Akikumbuka mchango alioutoa kwa wa Tz wakati wa vita ya kumng'oa nduli Amin, Uganda. Kwa hilo anaona Ghadafi anafaa sana. Ghadaf oyee, hoi? Oh Wadanganyika wepes kusahau. Kweli Wabongolala.
 
MUFTI wa Tanzania, Shehe Mkuu Issa bin Shaaban Simba amewataka Waislamu kuwaombea dua wenzao waliouawa katika vita inayoendelea Libya na wengine wanaodhulumiwa haki zao duniani.

Alitoa mwito huo kwenye hotuba yake katika Msikiti wa Gaddafi mjini Dodoma mwishoni mwa wiki.

Alisisitiza waumini wamwombee Kiongozi wa Libya, Kanali Muammar Gaddafi ambaye amekuwa msaada mkubwa kwa Waislamu duniani na wanyonge katika nchi zote bila kujali kama ni za Kiislamu.

Mufti Simba alisema maadui wa Waislamu wanachochea watu wakorofi kuanzisha fujo na vurugu kwa kuwaunga mkono ili misaada inayotolewa na kiongozi wa Libya duniani kote ifikie mwisho.

"Sisi hapa Dodoma tumepata msaada mkubwa kutoka Libya ni huu msikiti tuliuomba na tukaupata bila matatizo," alisema Mufti Simba.

Hata hivyo, alisema maombi yamewezesha maadui wa Gaddafi waliolenga kupiga nyumba yake kumkosa kwa kuwa ana hifadhi ya Mwenyezi Mungu kwa kuwa ibada anazofanya ni kubwa na ni mtu aliyehifadhi Kurani katika mwili wake.

Aliyashutumu mataifa makubwa ya Magharibi kwa kuelekeza vita nguvu zao kuipiga Libya kwa kutoa mali kuwasaidia waasi.

Wakati huo huo, Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mustafa Shaaban aliwahimiza waumini kulinda utamaduni na kuenzi ustaarabu wa Kiislamu kwa kuepuka sera na utamaduni wa nchi za Magharibi unaolenga kutumia nguvu kuathiri mila na desturi za Kiafrika.

Alisema utamaduni wa Magharibi unalenga kuvuruga tabia za vijana kwa kuwafanya waige mambo yanayokiuka maadili.

Alitoa mwito wa kuiga mfano wa China na Japan zilizokataa kufuata sera na utamaduni wa nje na hivyo kuweza kupiga hatua ya maendeleo.


Dodoma........... Basi wao pekee ndio wamuombee dua!!!!!!!!!!!
 
MUFTI wa Tanzania, Shehe Mkuu Issa bin Shaaban Simba amewataka Waislamu kuwaombea dua wenzao waliouawa katika vita inayoendelea Libya na wengine wanaodhulumiwa haki zao duniani. Huyu jamaa vipi? Dua lilihitajika kwa Osama![/QUOT

Kutegemea vya bure karne hii ni aibu, Kuna neno linalosema "amtegemeaye mwanadamu.............." Ona sasa Gadafi ndiyo tiamajitiamaji, atakate asitake safari imewadia tena akichelewa yatampata yale ya Saddam, sasa mtu kama huyo akiondoshwa inamaana ndiyo mwisho wa uislam?. Mashehe wajipange wasimame wenyewe, wakitegemea vya kupewa watakuwa watu wa kutoa matamko tu na kupiga dua huku wenzao wakifyeka mapori na kufanya maendeleo kwa nguvu zao!!!!.
 
Itakuwa kazi kama na aksofu wa Lutheri akisema tumuombee Lowasa , Sheikh wa Tabora akisema tumuombee RA na may be Pengo akisema tumuombee Chenge.

Just bcs wanatoa sadaka kubwa kubwa na kusaidia jamii isifanye watu watu wawe vipofu na viziwi.

Wanahohitaji kuombewa ni wanachi wa kawaida wa libya. na wala si Gaddafi.
 
Ndiyo. Akikumbuka mchango alioutoa kwa wa Tz wakati wa vita ya kumng'oa nduli Amin, Uganda. Kwa hilo anaona Ghadafi anafaa sana. Ghadaf oyee, hoi? Oh Wadanganyika wepes kusahau. Kweli Wabongolala.

Kiongozi kwa hili nitawatetea wadanaganyika wengi wenye akili kidogo, huyu anaye mtetea Ghadaf ni kuwa upeo wake mdogo alionao. Misaada ya kujengewa nyumba za ibada nayo tunaiona kuna ina tija...huu ni uwezo mdogo sana wa kufikiri. It's like mdogo wangu mmoja nilikuwa nae middle east wakati Uprising inaanza, alilia sana na kusema kwanini wana mpiga Ghadaf mtu mwema, mcha mungu na aliwajengea Msikiti mkubwa sana Dodoma. Nilidhani aliyasema hayo kwa sababu ya umri wake...kumbe hata viongozi wake nao the same...aibu sana. Eeeh vita ya 1978-79 wakati huyu ndugu akimsaidia Idd Amini ( bila shaka kwasababu ya Imani yake pia) ilikuwa ni sahhihi? Mbona mnajifanya hamnazo wazee wazima?......Nachukua sera za Magharibi sometime lakini si kwa hili, tumtetee Ghadaf kwa kuzingati mambo mengine kabisa tofauti na huu upupu unaoelezwa na the so called Kiongozi.
 
Sasa yupi kati ya Gadafi au wananchi wa Libya ndio wa kuonewa huruma?kwenye familia ya Gadafi wamekufa watatu je wananchi ni wangapi wameshafariki na maelfu kukosa makazi????Mufti umechemka sn
 
Hii ni sawa na kumwombea dua hitler, osama,sadam na waislamu wengine wachafu km hao............kweli uislamu ni unafiki................kuombea adui mkubwa wa haki?....ili iweje?.....km wananchi hawataki uwaongoze wewe unang'ang'ania ili umuongoze nani?.......jeuli na kiburi cha viongozi wa kiafrica na wale wengi wa kiislamu wasiotaka mabadilijko ndiyo chanzo cha migogoro mingi duniani.....
Waislam wa tz msipoteze kuombea magaidi iombeeni tz yenye neema ambayo watu wake ni masikini wa kutuopwa isonge mbele acheni unafiki
.-muombeeni kikwete aachane na mafisadi
-iombeeni ccm iache kuwagawa watz kwa misingi ya dini kwa kuweka kwenye ilanai yao baadhi ya mambo ya dini fulani
-vinginevyo tutakuwa km wabwbwajaji wazuri wa kitz
 
jamani mufti try to think before you speak, ghadafi anaonewa kwa lipi? haya ndio matokeo ya mtu kung'ang'ania madaraka kwa muda mrefu na pale wananchi wako wanapokuja juu kuhoji mtu anatumia nguvu ya jeshi kuwazima, ningemshauri mufti amuangalie ghadafi kama ghadafi namatendo yake kama kiongozi na sio ghadafi kama muislam.
 
Back
Top Bottom