Mubarak refuses to stand down

Hizo source zako hazina tofauti na Tanzania Daima, au Mwanahalisi! Mubarak yuko Misri na atahutubia Taifa usiku huu huenda akaachia madaraka kwa mujibu wa Katibu mkuu wa chama tawala cha Misri! na sasa naangalia live Aljazeera English hakuna hicho unachokipakazia! angalia hapa: Al Jazeera English: Live Stream - Watch Now - Al Jazeera English

Na hii issue haina uhusiano wowote na TZ! sisi tunayo Serikali iliyochaguliwa na Wananchi na sio haki kulinganisha Utawala wa Egypt chini ya Hosni Mubarak alie tawala nchi hiyo miaka zaidi ya 30 sasa!
Sisi katiba yetu hairuhusu Rais kutawala zaidi ya miaka 10! na nchi yetu ni ya vyama vingi sio kama Egypt huko hakuna demokrasia wala uhuru wa vyombo vya habari! TZ uhuru huo upo ndio maana magazeti kama Mwanahalisi yanaweza kumuita Rais Jakaya kuwa ni mwizi na fisadi!

Hivyo msichanganye mambo! h



Kuna tofauti gani kati ya miaka 30 ya utawala wa Mubarak na miaka 50 ya CCM kuwa madarakanio Tanzania?! Mimi sioni tofauti yoyote maana inachokifanya CCM ni kuhakikisha demokrasia ya vyama vingi inakiukwa ili wao wabaki madarakani, tofauti pekee ni kubadilisha sura za watu lakini sio mfumo. Kwangu mimi CCM inapractice mfumo wa kipekee kabisa wa kidikteta ambao lengo kuu ni chama kuhodhi madaraka forever kwa manufaa ya wachache walio madarakan tofauti na classical dictatorship.

Unaposema Tanzania kuna uhuru na demokrasia zaidi ya Egypt unadhihirisha kabisa ni jinsi gani usivyojua nini maana ya uhuru na demokrasia. Matukio mawili ya maandamo yaliyotokea hivi karibuni katika nchi hizi mbili ni kielelezo tosha, tumeona wanajeshi wa Egypt walivyokuwa wanajua nini maana demokrasia tofauti na kule Arusha amabko watu waliuawa kwa risasi za moto kutoka kwa polisi. Usitake kunidanganya kwamba Kikwete anaweza kuruhusu maandamo kama haya ya Egypt yakafanyika na kuonyeshwa kwenye TV ya taifa.
 
We are definitely living in very exciting times!

"Power tends to corrupt, and absolute power corrupts absolutely. Great men are almost always bad men." John Emerich Edward Dalberg Acton

"Unlimited power is apt to corrupt the minds of those who possess it." William Pitt, the Elder, The Earl of Chatham

Yanayotokea huko Misri ni somo kubwa kwetu sote!
 
Mkuu Mushi1, kuna nchi za weusi zenye wasomi wengi lakini hawana kitu. Fikiria nchi kama Nigeria, ni nchi yenye kiwango kizuri cha elimu. Raia wake wengi wana elimu nzuri tu. Lakini hakuna viongozi na serikali iliyo-corrupt kama Nigeria. Wananchi wanaishi kwa mateso makubwa. Lakini wako tayari kufa kwa shida hizo kuliko kukabiliana na viongozi wabovu. Shida? Ni woga!!! Nilikuwa naongea hivi karibuni na rafiki yangu mmoja kutoka Nigeria, alikubaliana na mimi kwamba hakika sisi weusi tuko waoga kujitoa muhanga ili - hata kama tusipofaidi sisi - wafaidi vizazi vijavyo.
Mkubwa,nakubali kuwa corruption Africa hatujambo,hata hivyo issue hapa ni kwanini wananchi walio wengi hawashtushwi na hilo?maybe ni kwasababu in reality,wameshindwa ku grasp madhara halisi ya corruption...?Wameshindwa kufanya hivyo kwasababu wale wanaoathirika zaidi ambao ni wengi,hawako kwenye nafasi ya kufanya mapinduzi kama ilivyo kwa wenzao wa Misri...

However,ni vyema ukatoa analysis based on facts ie demographics.
Kwa mujibu wa world Bulletin.net(http://www.worldbulletin.net/?aType=haber&ArticleID=69560),asilimia kubwa ya wananchi wa Egypt wana miaka 30 ama chini ya miaka 30(Two thirds of the population).In Egypt,elimu hadi chuo kikuu ni bure,na hao two thirds of population wana account for 90% of the jobless population,so unaweza kuona hawana kazi baada ya kumaliza shule,na kiujumla,wao ndiyo wengi zaidi ndani ya nchi.At the same time literacy rate yao ni way higher than Nigeria ambayo wao ni namba moja kwa population in Africa wakifuatiwa na Egypt ambao wanashare both middle east and African status.
Kwa ujumla according to the CIA Fact book,overall literacy rate ya adults wa Egypt(age 15-64) ni 71.4% while Nigeria has 54% Nafikiri pia literacy rate ya Egypt is even higher kwenye hiyo under 30 years age structure.
 
swali langu ni mubarak bado ni rais au madaraka kampa makamu wa rais?
According to different media sources (CNN, Al Jazeera, e.t.c) Mubarak delegated power to Vice president Suleiman, but he didn't step down.
 
Mubarak hajaachia ngazi!!!!! Kamgawia madaraka Makamu wake. Wanaharakati bado wapo Tahrir kama kawa na inasemekana leo Ijumaa ndo wataonyesha nguvu yao kubwa ya UMMA. Lakini Wamasri wasisahau kuwa Nasser, Sadat na Mubarak ni wanajeshi waliovaa nguo za kiraia. Nasser aliondoka madarakani kwa kifo cha Presha baada ya kupigwa vibaya na Waisraeli. Saddat aliuwawa kwa risasi. Mubarak ndo atoke kirahisi rahisi kwa shinikizo!! Atatoka kama alivyoahidi au vinginevyo anaweza liachia jeshi. Bado ukombozi unaendelea toka walivyofanya mapinduzi ya kuung'oa ufalme. Tanzania pia ina safu kubwa ya viongozi wa juu wanajeshi aliyoijenga Mwalimu. Kelele za mlango hazimsumbui ..............!!!
 
Back
Top Bottom