MUAJI YA KINYAMA ARUSHA: Mwema, Nahodha na Kikwete Mjipime Kubakia Madarakani

Uwezo Tunao

JF-Expert Member
Nov 14, 2010
6,942
1,190
Popote pale duniani sababu kuu ya kuwepo kwa chombo kinachoitwa SERIKALI katika jamii fulani ni kuhakikisha wakati wote kwamba wanawalinda raia wote salama na mali zao kwa usawa.

Sasa pale ambapo SERIKALI ndiyo inayoonekana kufadhili udhalimu katika chaguzi mbali mbali nchini, kuwanyima wananchi fursa ya kuwakilishwa jinsi wachaguavyo wenyewe kwa hiari yao, na kuamua kuwashamubulia kwa risasi za moto, kujenga mazingira ya kusababisha uharibifu wa mali na hata kuua kabisa kinyama kama ilivyotokea hivi karibuni mkoani Arusha, basi hapo mantiki ya kuwa na kitu SERIKALI haipo tena.

Kwa msingi huu wa kushambuliwa mara kwa mara raia nchini mwetu na kuuaua, viongozi wao kudhalilishwa, huduma za kiserikali kutolewa kwa raia kwa misingi ya itikadi zao kisiasa basi NI SHARTI WATU KUWAJIBIKA MARA MOJA kwa sababu waliokufa Arusha sio nzi, Walioua UDOM na kufichwa sio panzi na yule alieuaua Shinyanga na polisi wala sio mende hivyo kuwajibika viongozi wa juu hapa hakuna mjadala.

HOJA YANGU:


Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete, Waziri Mkuu Mizengo Pinda, Waziri Bora Utawala Mzee Tyson, Waziri Mambo ya Ndani Shamsi Vuai Nahodha, Waziri Serikali za Mitaa George Mkuchika, IGP Said Mwema, Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Meya wa CCM Arusha na Mama Chitanda, nyote kwa pamoja, wakati umefika wa nyinyi kwa nafasi zenu wenyewe KUJIPIMA KWA MISINGI YA MAUAJI HAYA YA KINYAMA JIJINI ARUSHA na muone kama kweli bado ni sahihi kwenu kuendelea kuongoza katika taifa hili TUPENDE TUSIPENDE.

Haya mauaji ya raia kwa kasi kubwa hii ya ajabu si mambo madogo na kuyapuzia mbali hata kidogo kama bado tunaipenda kweli nchi yetu na kuitakia ustawi mzuri huko tuendako. Tukumbuke usemi wa wahenga; mdharau mwiba miguu huota tende, tuliwataka kujiuzulu wakati mlipompiga na kudhalilisha mbunge wa Arusha akiwa kazini jimboni kwake na mkaipuuzia mbali bila hata mtu mmoja kuwajibika na hivi sasa taifa zima hatushinikizi tena bali tunawaangalieni kwa karibu sana katika hili!!!
 
Hawajapiga risasi wao why wajiuzuru? hata waliosign mikataba mibovu isiyo na tija ndio hao hao viongozi wetu
 
Binafsi nadhani endapo wananchi tutaendelea kudharauliwa kiasi hiki, kutendewa unyama wa kutisha tofauti kabisa na tamaduni zetu Tanzania, na mbaya zaidi viongozi kuonekana kuendelea kutupuuza bila watu kuwajibika kwa wakati muafaka basi nahofia ya kwamba huenda utendaji na ufanisi wa serikali huenda usiwe mzuri sana vile.

Ni juu yenu sasa kutafakari na kuchukua hatua au kutokufanya lolote pia. Mauaji ya Arusha na Pemba huenda yakawa yamefungua ukurasa mpya kabisa nchini mwetu huku tukiwa na uhakika ya kwamba wananchi sisi kujiandikia Katiba ya nchi yetu wenyewe safari hii haina mjadala wala pa kukwepea hata kuletwe kikosi cha mzinga mpaka kieleweke.

Mauaji ya Arusha kwa sasa yametuimarisha azma yetu leo kuhusu harakati za kuleta mabadiliko ya kweli nchini kuliko hata pale kabla hamjaamrisha jeshi hilo tunaloligharamia sisi wenyewe kuja kutuua. Kamwe haturudi nyuma hata hatua moja kuhusu mabadiliko nchini.
 
hapo ni kutapatapa kwa CCM na serikali ya kuchongwa inavyo onyesha kwa wananchi.Mauwaji yanatokea Arusha kesho yake rais anaendelea na sherehe ikulu.Imefikia muda wa kuwalazimisha kutoka madarakani kwa nguvu maaana kama hawajali maslahi ya raia basi hatuwahitaji tena
 
Watu wameingia madarakani kwa gharama kubwa leo simple tu unasema wajiuzulu!!
Huwafahamu viongozi wa Africa wewe??
 
Serikali ndiyo wavunjifu wa amani ya Tanzania, wakisaidiwa na Mheshimiwa "Mwema na watu wake" Viongozi wetu wamekua wanahubiri demokrasia isoyoonekana! Wanawaua wenzetu kama wanyama wa pori lisilolindwa!! Hii tunasema hatukubaliani nao kabisa, lazima wawajibike! Chadema waliandaa maandamano ya amani, na walitembea kilomita 2 bila kuleta vurugu, sasa kilomita chache zilizobaki kufika uwanjani ndiyo wangeleta hizo vurugu? kwa kweli polisi ndiyo walioleta vurugu, IGP na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha mnatakiwa kuwajibika mara moja. Watanzania siyo wapole kama mnavyofikiri, tunazijua haki zetu, na Polisi mkiendelea kuwaua ndugu zetu itafika mahali tunashindwa kuvumilia "Point of no return" na mtapambana na nguvu ya uma!
 
hapo ni kutapatapa kwa CCM na serikali ya kuchongwa inavyo onyesha kwa wananchi.Mauwaji yanatokea Arusha kesho yake rais anaendelea na sherehe ikulu.Imefikia muda wa kuwalazimisha kutoka madarakani kwa nguvu maaana kama hawajali maslahi ya raia basi hatuwahitaji tena
aisee inasikitisha sana!
 
tatizo viongozi wa Afrika hawana utaratibu wa kujiuzulu, hebu angalia Rais wa German alikaa madarakani miez mitatu tu, lakini wakati anaingia madarakani aliahidi kuondoa majeshi Afghanstan kwa siku themanini lakin mpaka siku ta tisini hakufanya hinvo ikambidi ajiuzulu, lakin hapa kwetu viongozi wanaua lakin wala hawashtuki.
 
hapo ni kutapatapa kwa CCM na serikali ya kuchongwa inavyo onyesha kwa wananchi.Mauwaji yanatokea Arusha kesho yake rais anaendelea na sherehe ikulu.Imefikia muda wa kuwalazimisha kutoka madarakani kwa nguvu maaana kama hawajali maslahi ya raia basi hatuwahitaji tena

hivi wanaotapatapa ni CCM au CHADEMA? you sound confused!
 
Hawajapiga risasi wao why wajiuzuru? hata waliosign mikataba mibovu isiyo na tija ndio hao hao viongozi wetu

Askari waliua jijini Arusha walifanya hivyo kwa kutii amri za kutoka juu kwa viongozi hawa ndio maana viongozi huhitajika tulitunzia heshima serikali husika kwa kujiengua mwenyewe madarakani.

Pia, kama bado tunaye hata kiongozi mmoja tu ambaye japo vichembe chembe vya USTAARABU KAMA ULE WA MZEE MWINYI MIAKA YA NYUMA HUKO alivyowahi kufanya baada ya mauaji ya raia kutokea akawa nayo kiongozi yeyote wa kipindi chetu hiki hapa basi na wao tumewataka kujipima na kujiamulia wenyewe kama ni sahihi kuendelea kuongoza watu wasiokua na imani na wewe tena kufuatia kushindwa kwako kutumia mamlaka uliopewa na sheria zetu na katiba tukufu kuzuia vifo ambavyo vingeweza kuzuilika endapo madaraka hayo yangetumika kwa wakati mwafaka, kwa misingi ya haki na inje ya mipaka ya itikadi za kisiasa.

Kwa mfano Waziri Mkuu alikua na mamlaka kutengua uchaguzi wa Meya Arusha, Mbeya na sehemu nyingine nyingi tu ambayo uliodaiwa kutokuzingatia sheria, kanuni na taratibu lakini Mhe Pinda hakufanya hivyo. Mhe Kikwete na Vuai tumewapa vyombo vyote vya usalama ili tuwe salama wakati wote lakini wakashindwa kulizingatia jukumu lao hilo la msingi. Mbunge wa Viti Maalum Tanga, Chitanda, ajipenyeza kiajabu kupiga kura kuchagua meya Arusha na kusababisha mikanganyiko isiyo ya lazima na kutufikisha kwenye washikadau kuigomea na mwishoni kuuaua huku waziri wa utawala bora akiwa amelifumbia macho hilo jambo na wala Mkuchika kutokuizuia kutoke.

Bila watu kujiuzulu hapa kwa idadi yao hii kashfa ya jiji la Arusha huenda likageuka jinamizi sugu la kuinyima kabisa serikali za CCM tangu pale Pemba 2001 na sasa hapa Arusha na hata kwa vipindi vijaavyo huenda ikashinwa kabisa kutekeleza majukumu yake kwa jamii yetu hii ya Kitanzania kote mijini na vijijini.
 
JF kulitokea nini mpaka mtandao ukawa hauonekani, mbona hamjatuhabarisha?

Au tatizo ilikua ni hii THREAD kutaka baadhi ya viongozi walioshindwa kuzuia mauji ya Arusha wajipime wenyewe kama wanajiuzulu au wanaendelea tu na kazi kimabavu?

Modes (hasa yule alioko zamu mtamboni) hebu mtujuze, shida ilikua ni nini kati ya saa tatu na nusu mpaka nne na nusu?
 
2001 nani alijiuzuru?

MASKOFU NA MASHEHE, KABLA YA WADHIFA WAO KWANZA NI WATANZANIA HIVYO KUKEMEA MAOVU HAKI YAO

Nashangaa mtu kutaka kulazimisha harufu ya udini katika hoja hii kwa kujaribu kuwapaka masizi MAASKOFU MJINI ARUSHA. Maana mpaka dakika hii MAASKOFU hawamtambui MEYA WA CCM JIJINI ARUSHA, ambaye naye ni MKRISTO SAWASAWA na hao maaskofu.

Kimsingi MAASKOFU walisema wazi kwamba wanachokipinga kwa meya huyu wa CCM wala si maovu ya kuwa mwana-CCM, si maovu ya UKRISTO wake isipokua MAOVU WANAYOYAKEMEA ni sheria na taratibu za uchaguzi zilivyopindishwa kumuingiza madarakani kupitia mlango wa nyuma.

Sasa viongozi wetu wa kiroho wasipokemea maovu kama haya, ukimya wao juu ya jambo hatari kama hili tafsiri yake ni kwamba wameunga mkono huo uchafu na ubakaji wa DEMOKRASIA, ndivyo watu mnavyotaka????????????????

Kama shida ni kuhusu vifo vya raia wa Tanzania na hata yule wa nchi rafiki na jirani Kenya, nadhani mtu asijaribu kuziba wengine midomo. Mauaji ya pemba 2001 vingozi wa dini walipiga kelele sana na kuikemea serikali ya Mhe Mkapa wakisema nguvu nyingi kupita kiasi imetumika dhidi ya wananchi. Katika kundi hilo kulikwepo Mashehe, Maaskofu, Mapadri na Wachungaji kwa mchanganyiko wake.

Hivyo kutokana na ukweli huu ambao iko mikononi mwao waandishi wa habari mpaka leo hii, ni matumaini yangu kwamba hauna maana yoyote kutaka kutuambia ya kwamba kama kilio cha Watanzania hakikusikilizwa tulipoipigia kelele mauaji ya Pemba basi leo hii raia tunapouaua tusiseme kwa sababu kule hatukusilizwa vile vile.

Pia, sitaki niaminishwe ya kwamba mweka hoja hii anajaribu kutuambia kwamba MAUAJI YA KINYAMA ARUSHA kwa vyovyote vile yalitekelezwa na MTU AU WATU anaowajua yeye ILI KUSAIDIA KUMLIPIA KISASI CHA MAUAJI YA PEMBA leo hii hivyo anaona hadi sasa ngoma ni droo na wala kusilalamike mtu?

Mwisho, imekuaje mtoa mada umekwepa kujiuliza maswali yote ya msingi hapa; Je, MASHEHE NA MAIMAMU kukaa kimya bila kukemea mauaji ya kinyama Arusha hadi kujitokeza tu kutetea Mhe kwa sura nyingine ya ajabu ajabu tu inamaana wanayo agenda gani?????????
 
Popote pale duniani sababu kuu ya kuwepo kwa chombo kinachoitwa SERIKALI katika jamii fulani ni kuhakikisha wakati wote kwamba wanawalinda raia wote salama na mali zao kwa usawa.

Sasa pale ambapo SERIKALI ndiyo inayoonekana kufadhili udhalimu katika chaguzi mbali mbali nchini, kuwanyima wananchi fursa ya kuwakilishwa jinsi wachaguavyo wenyewe kwa hiari yao, na kuamua kuwashamubulia kwa risasi za moto, kujenga mazingira ya kusababisha uharibifu wa mali na hata kuua kabisa kinyama kama ilivyotokea hivi karibuni mkoani Arusha, basi hapo mantiki ya kuwa na kitu SERIKALI haipo tena.

Kwa msingi huu wa kushambuliwa mara kwa mara raia nchini mwetu na kuuaua, viongozi wao kudhalilishwa, huduma za kiserikali kutolewa kwa raia kwa misingi ya itikadi zao kisiasa basi NI SHARTI WATU KUWAJIBIKA MARA MOJA kwa sababu waliokufa Arusha sio nzi, Walioua UDOM na kufichwa sio panzi na yule alieuaua Shinyanga na polisi wala sio mende hivyo kuwajibika viongozi wa juu hapa hakuna mjadala.

HOJA YANGU:


Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete, Waziri Mkuu Mizengo Pinda, Waziri Bora Utawala Mzee Tyson, Waziri Mambo ya Ndani Shamsi Vuai Nahodha, Waziri Serikali za Mitaa George Mkuchika, IGP Said Mwema, Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Meya wa CCM Arusha na Mama Chitanda, nyote kwa pamoja, wakati umefika wa nyinyi kwa nafasi zenu wenyewe KUJIPIMA KWA MISINGI YA MAUAJI HAYA YA KINYAMA JIJINI ARUSHA na muone kama kweli bado ni sahihi kwenu kuendelea kuongoza katika taifa hili TUPENDE TUSIPENDE.

Haya mauaji ya raia kwa kasi kubwa hii ya ajabu si mambo madogo na kuyapuzia mbali hata kidogo kama bado tunaipenda kweli nchi yetu na kuitakia ustawi mzuri huko tuendako. Tukumbuke usemi wa wahenga; mdharau mwiba miguu huota tende, tuliwataka kujiuzulu wakati mlipompiga na kudhalilisha mbunge wa Arusha akiwa kazini jimboni kwake na mkaipuuzia mbali bila hata mtu mmoja kuwajibika na hivi sasa taifa zima hatushinikizi tena bali tunawaangalieni kwa karibu sana katika hili!!!

Wahuni wasipotii amri halali ya serikali yetu tuliyoichagua, mambo kama haya hutokea. Na mkirudia tena uhuni wenu basi mtakufa tena. she***zi taip
 
Watu wameingia madarakani kwa gharama kubwa leo simple tu unasema wajiuzulu!!
Huwafahamu viongozi wa Africa wewe??

Ndibalema, are you a sympathiser of Nation of Islam? hiyo picha unayoitumia ni nzuri sana na inabidi pia ufuate itikadi za shujaa huyo wako.
 
Wahuni wasipotii amri halali ya serikali yetu tuliyoichagua, mambo kama haya hutokea. Na mkirudia tena uhuni wenu basi mtakufa tena. she***zi taip

Sitaki kuamini kwamba Watanzania katika kutekeleza sehemu ya haki yao kudai mabadiliko ya kweli ndio sasa Ndugu Nancy Tweed uwaone kuwa ni WAHUNI!!! Nadhani utakua umechanganya mada hapa au uko baa.
 
Waziri Mkuu kama msimamizi mkuu wa shughuli za serikali hajatoa tamko mpaka hivi sasa. Hebu fikiri tena kuhusu credibility na accountability ya viongozi wetu wa Africa.
Huyu mzee ni hypocrite kama mara ya mwisho anakataa gari mpya ambayo ishanunuliwa na inatumika na mtu mwingine as we speak.
Wakati Mr president anaendelea na cocktail party kama hakuna kilichotokea.ridiculous!!!!!
 
Back
Top Bottom