dos santos
JF-Expert Member
- Nov 22, 2010
- 256
- 128
Baada ya chama cha CUF kufanya maridhiano na CCM juu ya uundwaji wa serikali ya umoja wa kitaifa huko visiwani Zanzibar,chama cha CHADEMA kilikuwa mstari wa mbele kupinga na kubeza maridhiano hayo,huku kikiishutumu CUF kama CCM B.Uundwaji wa serikali ya umoja wa kitaifa unatokana na kura za maoni ya wazanzibar.Hivyo uundwaji wa serikali hiyo umetokana na maamuzi ya wananchi.
Majuzi CHADEMA wameafikiana na serikali ya CCM juu ya kuridhiana mwenendo wa uratibu wa uundwaji wa tume ya kuratibu maoni ya katiba mpya.Wamekubali muswada usainiwe(tayari umeshasainiwa jana) na kama wana maoni yao basi wapeleke bungeni mwezi januari.Wamekubali na kutia saini kitu ambacho hata wenyewe hawajui maslahi yake.Bila shaka walipenda kwenda ikulu,waliwahi kuahidi kwa gharama yoyote watafika ikulu.Na kweli wamefika na Juice wamekunywa.
Sasa angalia baina ya miafaka hii miwili CCM,CUF na CCM,CHADEMA upi bora na wenye tija kwa wananchi,na ambapo kulikuwa na ulazima wa kukaa meza moja na kufanya maridhiano?
Majuzi CHADEMA wameafikiana na serikali ya CCM juu ya kuridhiana mwenendo wa uratibu wa uundwaji wa tume ya kuratibu maoni ya katiba mpya.Wamekubali muswada usainiwe(tayari umeshasainiwa jana) na kama wana maoni yao basi wapeleke bungeni mwezi januari.Wamekubali na kutia saini kitu ambacho hata wenyewe hawajui maslahi yake.Bila shaka walipenda kwenda ikulu,waliwahi kuahidi kwa gharama yoyote watafika ikulu.Na kweli wamefika na Juice wamekunywa.
Sasa angalia baina ya miafaka hii miwili CCM,CUF na CCM,CHADEMA upi bora na wenye tija kwa wananchi,na ambapo kulikuwa na ulazima wa kukaa meza moja na kufanya maridhiano?