Mtwara Mkoa masikini unaoendesha serikali ya Tanzania

Tangu nikiwa mdogo nilikuwa nikiambiwa mikoa ya kusini hasa mkoa wa Mtwara ni masikini sana, na kutokana na umasikini huo serikali ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania haiwezi kuendeleza kusini kwa kujenga miundo mbinu mbalimbali kama barabara, kupanua bandari, reli, hospitali, Shule pamoja na vyuo vya elimu ya juu, maji na nisharti. Sababu kubwa ni kwamba mkoa huu unachangia kiasi kidogo cha mapato ya serikali. sina hakika sana kama majibu haya yaliyotolewa na wengi yalikuwa ya kweli lakini yalielekea kuwa ya kweli maana yalisemwa na wengi tena wengine wenye nafasi kubwa kubwa kwenye ofisi zao.

Ahaa!!! leo hii kwa mujibu wa takwimu za TRA "TRA Quaterly Revenue collection 2011_2011". Mkoa wa Mtwara ni wa 7 katika kuchangia kwenye pato la taifa kwa kodi. Kwa lugha nyepesi ndio wanunuzi wakubwa wa mashangingi ya serikali, au ndiyo wachangiaji wakubwa wa mafuta ya Jet stream ahaa na posho za wabunge, looh na posho za vyama vya siasa.

Swali langu: Imekuwaje mbona hayo maendeleo tuliyonyimwa tangu uhuru kwa kisingizio cha uchangiaji mdogo kwenye pato la taifa hayaletwi
hivi sasa tunapochangia kwa kiasi kikubwa au vigezo vimebadilika?

Tafadhali naombeni mchango wenu na ushauri wenu kwetu sisi wana Mtwara.

Nimeambatanisha jedwali la makusanyo kwa mujibu wa report za TRA: www.tra.go.tz

RegionMillion TShsMillion TShsMillion TShsMillion TShsRanking
Direct TaxIndirect Tax Customs and ExciseTotal
Ilala 56,801.9 32,545.3 - 89,347.2 1
Kinondoni 32,858.7 16,414.7 - 49,273.4 1
Temeke 12,987.0 10,677.7 - 23,664.6 1
Arusha 15,101.3 10,111.9 9,383.1 34,596.3 2
Coast 1,478.9 562.4 91.1 2,132.5
Dodoma 3,787.6 1,385.8 17.5 5,190.8
Iringa 3,471.4 1,941.9 20.5 5,433.9
Kagera 967.1 1,082.9 1,938.7 3,988.7
Kigoma 694.5 342.1 786.5 1,823.1
Kilimanjaro 6,834.2 2,947.3 11,389.3 21,170.8 3
Lindi 284.2 154.5 22.9 461.5
Mara
1,264.0 914.4 13,882.2 16,060.7 4
Mbeya 2,605.4 2,241.0 7,446.3 12,292.8
Morogoro 5,359.6 2,427.2 70.2
7,857.0
Mtwara 7,608.5 6,838.5 270.4 14,717.4 7
Mwanza
8,905.0 3,889.9 4,577.3 17,372.2 5
Ruvuma 667.1 469.8 32.7
1,169.6
Shinyanga 1,355.0 1,068.8 37.8 2,461.6
Singida 331.0 269.1 51.3 651.4
Tabora 1,087.4 896.2 15.1 1,998.7
Tanga 2,849.7 2,231.8 9,755.7 14,837.3 6
Rukwa 748.1 235.4 97.6 1,081.2
Manyara 686.2 263.6 - 949.9

Kweli nkonde chi ntu!
Hizo ranking zenye green ndio vipi?
 
Nakusihi uvute subira kwani baada ya mwaka mmoja tu resources za Mafuta na Gesi ndizo zinategemewa kufadhili AHADI NA NGONJERA ZOTE TULIZOSIKIA kipindi cha kampeni iliyopita. Kwa namna hiyo inategemewa kwamba CDM watafungwa migoli ya kisigino come 2015.
Kwa hiyo, then Mtwara inategemewa kuwa mkombozi. hii ngonjera kanisimulia juha flani akiota mchana kweupeee!

Unadhani Taifa likiwa chini ya CDM kusini itapata heshima stahiki na haki kwa watu wake.... mbona hata hivi sasa walikuwa na kila sababu ya ku-invest kisiasa kule lakini wapi hawaendi na hawaamini kama kuna ndugu zao kule. Hii inareflect hata awamu za serikali za CCM yenyewe hebu check maumivu aliyoyagawa Mwl. Nyerere, then Mzee Mwinyi. Kwa kukupa mwanga tu tembelea maeneo ya maghalani na ndipo utakapogundua kuwa uchumi wa Mtwara ulikuwa strong by 50 -70th na early 80th na serikali ya hawa jamaa kwa upendeleo wakaua kila kitu. Na hata huyu mzee wa Bwagamoyo anamaliza muda wake hajafanya kitu huku. (Hao ni wale wale).
 
Kweli nkonde chi ntu!
Hizo ranking zenye green ndio vipi?

Haibadilishi hoja labla mbona hujauliza hizo zingine ambazo hazijawekewa hata hiyo ranking.......bila shaka wewe pia ni wale wazee waliopata kielimu kidogo kwa kuangalizia hawatafakali concept na hawawezi kuwa na jipya. pengine hapa ungejisikia safi kama ningeanzisha thread ya mapambano ya CCM na CDM.
 
Utasemaje Mtwara inaongoza uchumi wa nchi wakati mchango wake haufiki hata 5% ya makusanyo ya nji jote

Kwanza wewe binafsi unachangia shiling ngapi kwenye pato la taifa.....halafu sijasema inaongoza uchumi wa nchi nimesema mkoa unaendesha serikali ya Tanzania au wewe hulipi kodi ni mla kodi za watu basi sasa wenyewe tunadai maendeleo siyo kuchukua kodi zetu tu.
 
.

Barubaru umenena mambo ya msingi kabisa ni kweli tuna rasilimali nyingi na za maana ambazo hata nchi nyingi za Africa, asia na europe hawana lakini mipango haieleweki bandari ni natural resource mojawapo tu bado tuna gesi, mbuga za wanyama na mazao ya kueleweka ya biashara bila kusahau mito yenye uwezo wa kuzalisha chakula cha kutosha.

Mbali ya kuwa kupanga ni kuchagua nadhani tuna tatizo la mipango mingi kufanywa kwa upendeleo, nilipokuwa chuoni niliweza kufanya research ya haraka haraka nikagundua zaidi ya 90% ya wanafunzi na wakufunzi pale wametembea karibu mikoa yote isipokuwa Lindi na Mtwara na hao ndiyo wako maofisini leo hii ndiyo tunaowategemea kupanga mipango ya kuliendeleza eneo hili maana ndiyo waliohodhi mamlaka na wanakomba kila kitu kinachopatikana kule kama ulivyoona kwenye hizo takwimu.

nakubaliana na wewe kwa silimia zote. Hata mimi nilipokuwa nafanya kazi Serikalini niliona wazi watu wakihamishiwa huko Kusini basi na kazi wana acha. sababu kubwa miundombinu hususan barabara zilikuwa hakuna kabisa ondolea mbali huduma za kijamii kama mashule, hospital na social activities zilikua almost zero.

lakini kumbuka kuna potential kubwa sana hasa Bandari, gesi na mazao kama karanga, ufuta na korosho na kubahatika kuwa na beach nzuri sana za mikindani na Msanga mkuu na zile za Lindi.

Hakika huku hakuitaji nguvu kubwa kukusukuma kiuchumi kama kukiwa na miundombinu bora tu ya barabara basi mengine yatajileta yenyewe hususan sector ya viwanda.

Natumaini kabisa kama barabara itakuwa nzuri kutoka Dar mpaka Mtwara na bandari ikaimarishwa basi Mtwara ;AZIMA UTAKUWA MJI WA PILI KIUWEKEZAJI NYUMA YA DAR NA hivyo watakuwa wa pili kuchangia pato la taifa katika TRA.

Wachumi wenzangu Tanzania mko wapi kuona fursa hizo. Acheni siasa okoeni nchi yenu kwenye lindi la umasikini
 
nakubaliana na wewe kwa silimia zote. Hata mimi nilipokuwa nafanya kazi Serikalini niliona wazi watu wakihamishiwa huko Kusini basi na kazi wana acha. sababu kubwa miundombinu hususan barabara zilikuwa hakuna kabisa ondolea mbali huduma za kijamii kama mashule, hospital na social activities zilikua almost zero.

lakini kumbuka kuna potential kubwa sana hasa Bandari, gesi na mazao kama karanga, ufuta na korosho na kubahatika kuwa na beach nzuri sana za mikindani na Msanga mkuu na zile za Lindi.

Hakika huku hakuitaji nguvu kubwa kukusukuma kiuchumi kama kukiwa na miundombinu bora tu ya barabara basi mengine yatajileta yenyewe hususan sector ya viwanda.

Natumaini kabisa kama barabara itakuwa nzuri kutoka Dar mpaka Mtwara na bandari ikaimarishwa basi Mtwara ;AZIMA UTAKUWA MJI WA PILI KIUWEKEZAJI NYUMA YA DAR NA hivyo watakuwa wa pili kuchangia pato la taifa katika TRA.

Wachumi wenzangu Tanzania mko wapi kuona fursa hizo. Acheni siasa okoeni nchi yenu kwenye lindi la umasikini

Ni heri umeyaona barubaru nchi hii ina wachumi feki kabisa wamejaa kisiasa na wanawaza kisiasa (5 years term) hata wachumi waliopostiwa kwenye halmashauri za huku sijuwi walisoma wapi au wanawaza nini au pengine tuseme wamekosa uzalendo. Maana hata hawazishauri halmashauri kuwekeza kwenye miradi yenye kuleta tija ya muda mrefu ukiangalia kituo cha mabasi Mtwara hakuna kinachofanyika kuboresha na kuthibiti mapato, wangeweza kuwekeza pia kwenye, masoko ya pale mjini, kivuko, bajaji zipo kiholela tu, pikipiki zipo zipo tu, daladala usiseme, taxi waww nk. Lakini wapi wapowapo tu wanasubiri amri kutoka Dar kwa waziri pinda ndipo watekeleze majukumu. Wameshindwa hata kuanzisha masoko ya mnada. Na matokeo yake hata kuhudumia mazingira ni ndoto round about zimechakaa. Ni watu wa hovyo kabisa hawa.
 
Ndugu yangu pato kubwa la taifa linamegwa na wale jamaa zetu wa kaskazini. au hukusikia ile hotuba ya sendeka bungeni? kimkoa kidogo kuliko wilaya yake ya simanjiro lakini kinabajeti ya kujenga km 300 za lami wakati wengi hata hapa dar hakuna hiyo kitu. hawa wenzetu ni wakuogopwa kama ukoma.
 
Kuna matatizo katika hizo data kwani Mwanza ndo ilitakiwa kuwa ya 4 the mara ya 5, acheni uchakachuaji.
Hapa suluuu ni serikali za majimbo, mimi kama mzawa wa mara, kama ndo kiasi tunachochangia katika pato la taifa alafu hali zetu ndo kame vile hapa. Pesa zichukuliwe mara zipelekwe kwa wakwere wanaochimba shimo moja ya choo kwa 75mil
 
Mtwara mambo mengine tunajitakia wenyewe kwa kuwa so cheap kwa watawala wanaweza kudanganya au kufanya chochote na bado tukajib kidumu!wenzetu wanapelekewa maendeleo kutokana na umoja wa wakilishi wao!wabunge wa kusin wanaona fahar wananchi wanavyojaa milangon mwao na kuombaomba.wasomi ambao inabid walete changamoto wote wanagombea kupitia ccm wakikosa wanarud dsm wote hawaamin kma wanaweza kushinda kupitia vyama vingine(angalia cv za wagombea wa upinzan mtwara 2010)
 
Si Mtwara tu, mikoa yote ya Tanzania yenye Waislaam iliuliwa makusudi na Nyerere. Hilo ni wazi kabisa. Na ndio vitu vinavyopelekea atake kupewa utakatifu, sababu za kupewa utakatifu ndio hizo za kuwadidiza Waislaam kila alivyoweza. Kuna sabau ipi nyingine zaidi ya kumpa nyerere utakatifu?
 
Na hivi karibuni tu tutaona ukanda wa pwani hususan Mtwara, Pwani. Itavyokuwa ni namba moja kwa pato la Taifa baada ya kugunduliwa kiasi kikubwa cha Gas na soon Mafuta.
 
Na hivi karibuni tu tutaona ukanda wa pwani hususan Mtwara, Pwani. Itavyokuwa ni namba moja kwa pato la Taifa baada ya kugunduliwa kiasi kikubwa cha Gas na soon Mafuta, hapo sasa utaona watavyohaha kuwa ooh, inajengwa Mtwara tu, sisi tunasahauliwa. Mie naoina ni wakati muafaka Tanzania igawanywe Waislaam wabaki walipo wengi na dini zingine wabaki walipo wengi, kama India tu na Pakistan. Tusileteane ubabe kwenye mali.
 
Na hivi karibuni tu tutaona ukanda wa pwani hususan Mtwara, Pwani. Itavyokuwa ni namba moja kwa pato la Taifa baada ya kugunduliwa kiasi kikubwa cha Gas na soon Mafuta, hapo sasa utaona watavyohaha kuwa ooh, inajengwa Mtwara tu, sisi tunasahauliwa. Mie naoina ni wakati muafaka Tanzania igawanywe Waislaam wabaki walipo wengi na dini zingine wabaki walipo wengi, kama India tu na Pakistan. Tusileteane ubabe kwenye mali.

Aiseeee!!!! Mbona kuna miji ya ki-mission kabisa au hujui hilo!!!???? Unaweza ukaongelea mada husika na ukaachana na mambo ya udini???? Maana mi mwenyewe natokea huko na ni Mkristo, nikae upande upi wa huo mgawanyo unaoutaka???
 
Si Mtwara tu, mikoa yote ya Tanzania yenye Waislaam iliuliwa makusudi na Nyerere. Hilo ni wazi kabisa. Na ndio vitu vinavyopelekea atake kupewa utakatifu, sababu za kupewa utakatifu ndio hizo za kuwadidiza Waislaam kila alivyoweza. Kuna sabau ipi nyingine zaidi ya kumpa nyerere utakatifu?

Si kweli, historia ndiyo imeiharibu Kusini kabla hata ya Nyerere kuchukua nchi! Mgawanyo uliokuwa umefanywa na wakoloni ulikuwa ni kwamba Kaskazini ilikuwa ndiyo kitovu cha uzalishaji ila cheap labours walitokea Kusini!!! Nenda maili sita Moshi kwa uthibitisho zaidi na uulize asili ya wale watu waliobaki pale (manamba), wengi walitokea Singida na Kusini mwa TZ!!!
 
Ndugu yangu pato kubwa la taifa linamegwa na wale jamaa zetu wa kaskazini. au hukusikia ile hotuba ya sendeka bungeni? kimkoa kidogo kuliko wilaya yake ya simanjiro lakini kinabajeti ya kujenga km 300 za lami wakati wengi hata hapa dar hakuna hiyo kitu. hawa wenzetu ni wakuogopwa kama ukoma.

Ni kweli na yanafanywa haya huku yakiwekewa propaganda chungu mzima, mfano ona maneno yaliyotolewa baada ya awamu ya mkapa kuanzisha ujenzi wa daraja la umoja (TZ to Moz). Na hata waliopo kule kikazi wengi ni wahujumu ushahidi upo wanaiba na kuhujumu kwa kisingizio cha kuwa watu wa kusini hawajasoma.....lakini najiuliza kwani kusoma maana yake kuiba na kuhujumu mipango ya maendeleo????
 
Back
Top Bottom