Mtwara kumekucha; Maandano ya kupinga kusafirisha gesi yaja

Status
Not open for further replies.
Kila kitu dar? Haifai...watu wanajenga fly overs dar akati singida na dodoma maji shida...huuu si ujinga kabisa?? Nawaunga mkono wana mtwara...na kila mkoa ukifanya hivi hakika maeneo yote yataendelea
 
Mtwara na Lindi sina uhakika kama waweza fanya mambo makubwa hivi....ila ingekuwa Mbeya ningekuwa na uhakika wa100% ges isingeondoka pangechimbika!

inaonesha hata darasani ulikuwa unapenda sana
kucrem na si kuelewa pole kwa tatzo lako
 
Kwa kweli huwa sijui kama mipango yetu ya Kitaifa hasa ya maendeleo kama hufanywa na watalaamu. Kama ndivyo basi hatuna watalamu kitu ambacho siamini. Kwa mtu wa akili ya kawaida tu siye mtaalamu wa uchumi wala wa nishati hawezi kutotambua yafuatayo kuhusu gesi au mafuta yaliyogunguliwa huko kusini mwa Tanzania:

1. Tunataka yazalishe umeme ili tupate unafuu wa bei ya umeme. Umeme huo unaweza kuzalishwa huko huko kusini na kuingizwa kwenye grid ya Taifa huko huko kusini. Kwani mbona huko Mtera, Tanga n.k. wanazalisha umeme huko huko na kuingizwa kwenye grid ya Taifa? Sasa sijui sisi ni majuha au vipi, tunataka umeme huo tukauzalishie Dar kwa kuisafirisha hiyo gesi gafi kwenye bomba lenye kipenyo cha urefu wa mtu (over 1.5 m) na urefu wa over 550 km la gharama ya over TShs 3 trions! Mitambo iliyopo pale Ubungo ya Symbions, PTL, Songas n.k. bei yake kila moja haizidi TShs 150 billion. At most yote kwa pamoja haizidi TShs 1 trion. Tungeweza hata kui dismantle na kuisafirisha na kuifunga huko Mtwara kwa gharama ndogo zaidi. Au tungeweza kununua mitambo mingine mipya mingi kuliko iliyopo Ubungo na kuifunga huko Mtwara kwa chini ya bei ya hilo bomba, na kuweza kuzalisha umeme kwa gharama ndogo. Viwanda vya Dar vinaweza kuendelea kupata gesi kwa kutumia meli toka Mtwara ambazo gharama zake ni nafuu kuliko bomba au lori. Wastage kwenye bomba ni mkumbwa sana, kwanza lazima lijae (over 1 trion cubic metre) excess ndiyo itafika Dar. Njiani cho chote kinaweza kutokea kwenye hilo bomba na inaweza ikawa disaster tupu.

2. Matumizi mengine ya hiyo gesi ni majumbani, kupikia hivyo kuokoa mazingira kwa kupunguza kukata miti kwa ajili ya mkaa au kuni hasa kule vijijini. Kuna sababu gani gesi hiyo isijazwe kwenye hiyo mitungi au containers za gas za Oryx n.k. huko huko Mtwara na kusafirishwa kwa meli au malori hadi huko Dar na kwingineko ambako inahitajika?

3.Kwa hiyo hata mafuta ya petroli yatakapoanzwa kuchimbwa huko kusini yatabidi yasafirishwe gafi kwenye bomba hadi Dar kwa refinary badala ya hizo refineries kujengwa Mtwara?

4. Mhhhh, ndiyo maana tunashindwa kufunga mitambo ya kufua umeme unaosemekana wa zaidi Megawatts 5,000 huko kwenye mafuriko ya Steinghlet kwa sababu tunashindwa kuyahamishia hayo mafuriko Dar? Vivyo hivyo kwa makaa ya mawe na hata uranium zingekuwa Dar mambo yangekuwa poa! Jamani Tanzania si Dar peke yake na wawekezaji waambiwe hivyo, wapo watakaoelewa tu. Wasiolewa waachane na sisi, yote ni kwa faida yetu sote kwani gharama zitakuwa nafuu kwa wote wala si Mtwara peke yao. Vinginevyo wananchi watashindwa kuwaelewa kwa maamuzi kama haya yasiyokuwa na logic. Watafikiri kuna mlungura umetembea! Si vizuri, muwaelimishe.

Big up Mtwara corridor, keep up and we all stand to benefit.

HAPA kuna 10% katika mikakati na mipango ya kununua mabomba ya kusafirisha gesi hadi DAR,tena mikataba wa kazi kama hizi inawezekana TAIFA halipati tija bali ni kuingiza TAIFA katika madeni yasiyolipika.
 
Kujaza kila kitu dar ni uvivu wa ubunifu wa viongozi wetu. Ningependelea viwanda vihamie lindi na mtwara. Shughuli za kiserikali zihamie dodoma. Kidogo dar ipumue. Miundombinu iliyopo haisupport idadi ya watu na shughuli zote za kiuchumi.
 
Wewe kweli ni Maamuma kama jina lako linavyosomeka!

Hujakosea Mheshimiwa.
Sikujua kwamba kuomba kuelimishwa ni kosa, nisamehe bure. Nilidhani bado tuko enzi zile za "nitatumia elimu yangu kwa faida ya wote". Hata hivyo nashukuru, nimepata majibu niliyohitaji kutoka kwa wachangiaji wengine. Naendelea kukushukuru na kukutakia baraka za Mwenyezi Mungu. Aliyekupa wewe kiti ndiye aliyenipa mimi kumbi.
 
Hujakosea Mheshimiwa.
Sikujua kwamba kuomba kuelimishwa ni kosa, nisamehe bure. Nilidhani bado tuko enzi zile za "nitatumia elimu yangu kwa faida ya wote". Hata hivyo nashukuru, nimepata majibu niliyohitaji kutoka kwa wachangiaji wengine. Naendelea kukushukuru na kukutakia baraka za Mwenyezi Mungu. Aliyekupa wewe kiti ndiye aliyenipa mimi kumbi.
Mkuu mimi kosa langu nini?nilichokifanya ni kutaja tu jina lako ambalo wewe mwenyewe ulijibatiza!
 
Matumizi ya Gesi naona watu wengi hawaelewi lengo sio kupeleka Dar peke yake bali nchi nzima Dar ni mwanzo tu. Vilevile leo la mbali ni kupeleka kila nyumba kama ilivyo Europe kwa matumizi ya nyumbani. Dar ni kituo tu lakini Gesi inatakiwa kutawanywa Tanzania nzima. Gesi ambayo itaenda nje inatakiwa kupakiwa kitaalamu kutoka Mtwara na hii ndiyo Investment kubwa vilevile Gesi inatakiwa kutawanywa Mtwara na Lindi pia.
 
Matumizi ya Gesi naona watu wengi hawaelewi lengo sio kupeleka Dar peke yake bali nchi nzima Dar ni mwanzo tu. Vilevile leo la mbali ni kupeleka kila nyumba kama ilivyo Europe kwa matumizi ya nyumbani. Dar ni kituo tu lakini Gesi inatakiwa kutawanywa Tanzania nzima. Gesi ambayo itaenda nje inatakiwa kupakiwa kitaalamu kutoka Mtwara na hii ndiyo Investment kubwa vilevile Gesi inatakiwa kutawanywa Mtwara na Lindi pia.

Obviously something of what you have just said is the main intention in the long run (it's just commonsense). Tatizo hapa ni poverty ambayo inawafanya watu wa invoke their fatalism ideas and feel being cheated sijui hiyo gesi wanataka fanya nayo nini huko Mtwara yote.

If you look at the bigger picture ni kwamba many are beggining to loose hope, and those without other means of surviving will always cling to fatalism and my gosh the gas is their way out. Wanasahau kuwa hayo mahospitali na mashule waliokuwa nayo yametoka kwenye mifuko ya miji mingine to some extent.

Kuna watu hapa wanaanza kuchochea vitu wasivyojua athari zake in the long run huo ndio wasiwasi wa watu wengine. Ni kweli CCM imeshindwa kuongoza Taifa na imekosa dira la kitaifa lakini watolewe responsibly.
 
ndugu zangu wana janvi, serikali ya ccm imezoea kufanya mambo kiubabe ata kwenye maswala nyeti ambayo ndio maisha ya watanzania,wamezoea kupora mali na propaganda nyingi kudanganya wananchi leo imetokea mtwara,wananchi wameomba kijengwe kiwanda ambacho gess izalishiwe pale pamoja na kiwanda cha mbolea na bandari zifanye kazi ili zipatikane nafasi za ajira,je kikwete alivyosema maisha bora kwa kila mtanzania alitegemea kuyashusha toka mbinguni?matokeo yake waziri wa nishati ambaye naye ni msanii anageuza maneno eti watu mtwara hawataki gess itumiwe na watanzania wote na kunukuu katiba leo ndio wananukuu katiba wakati nchi hii kikwete anaiendesha nje ya katiba.SERIKALI YA CCM IACHE KUPOTOSHA WATANZANIA,HAKUNA MTANZANIA MPUMBAVU MUDA WOTE NI DIGITALE.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom