Mtuhumiwa wa EPA aandaa Harambee CCM katika hoteli ya Kempisky

GAMBLER

JF-Expert Member
Nov 22, 2009
303
11
Mtuhumiwa EPA adaiwa kuandaa harambee CCM
broken-heart.jpg

*NI MARANDA, WAMWALIKA RAIS KIKWETE

Sadick Mtulya

MTUHUMIWA wa wizi wa fedha kwenye Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), Rajabu Maranda anadaiwa kuandaa harambee kwa ajili ya kuichangia CCM mkoani Kigoma kwa ajili ya uchaguzi mkuu, harambeee ambayo Rais Kikwete amealikwa kuwa mgeni rasmi.

Habari za kuaminika zimesema harambee hiyo itafanyika Februari 6 jijini Dar es Salaam kwenye Hoteli ya Kilimanjaro Kempisky.

Kwa mujibu wa vyanzo vyetu, Maranda, ambaye ni kada wa CCM, ndiye aliyeratibu harambee hiyo.

"Harambee kwa ajili ya kuchangia CCM mkoa wa Kigoma kwa ajili ya kampeni za uchaguzi mkuu wa Oktoba 25, itafanyika Februari 6, mwaka huu, Maranda ndiye mratibu wa hili jambo na Rais Kikwete atakuwa mgeni rasmi," alisema mpashaji wetu wa habari hizo.

"Na kuna kamati imeundwa kwa ajili ya kufanikisha hilo... Maranda ameteuliwa kuwa katibu wakati mwenyekiti wake ni mzee Iddi Simba."

Hata hivyo, alipozungumza na Mwananchi jana kwa njia ya simu, Maranda alikiri kuwepo kwa kamati hiyo lakini akasema hawezi kuzungumzia lolote kuhusu harambee hiyo kwa kuwa yeye ni mjumbe tu wa kamati.

"Kweli kamati ipo, lakini mimi ni mjumbe na wala si katibu. Siwezi kuzungumza lolote kuhusu hii harambee kwa kuwa sio katibu wala mweyeketi," alisema Maranda.

"Kama unataka maelezo zaidi wasiliana na mwenyekiti au katibu wa mkoa wa Kigoma kwa kuwa wao ndiyo wenye shughuli hiyo. Mimi sielewi chochote kwa kuwa ni mjumbe tu na pia sijahusika na kitu chochote katika kufanikisha harambee hiyo."

Kwa mujibu wa habari tulizonazo kikao cha mwisho cha maandalizi ya harambee hiyo kilifanyika Januari 12, mwaka huu kwenye hoteli hiyo ya kiwango cha nyota tano na habari zinawataja waliohudhuria kuwa ni Maranda, Iddi Simba, mbunge wa jimbo la Muhambwe, Felix Kijiko, katibu CCM Kigoma, Mama Kastiko pamoja Katunda ambaye ni mfanyabiashara maarufu Dar es Salaam na Kigoma.

Maranda amedaiwa kuhusishwa moja kwa moja na kuandaa harambee hiyo kutokana na kwamba ndiye katibu wa fedha na uchumi mkoani Kigoma.

"Kimkoa yeye ndiye anayepaswa kuweka na kuandaa mipango mbalimbali ya mkoa kupata fedha kwa ajili ya kuendesha shughuli za kichama mbali na vile vitega uchumi vinavyojulikana mkoani Kigoma. Ndio maana ameshiriki moja kwa moja kuratibu na kufanikisha kufanyika kwa harambee hii," alisema mdokezaji huyo.

Hata hivyo, katibu wa CCM Kigoma, Mama Kastiko alisema kuwa haoni kikwazo kwa mkoa huo kufanya harambee hiyo.

"Cha ajabu nini? Kigoma kufanya harambee! Hili jambo ni la kawaida na linafanywa siku zote, na vyama mbalimbali, taasisi na hata watu binafsi," alisema Kastiko.

Alipoulizwa tarehe ya harambee hiyo, Kastiko alikataa kuitaja kwa madai kuwa bado hawajakuwa tayari kuitangaza hadharani.

"Aliyekuambia hizi taarifa ndiye akuambie na tarehe. Kifupi siwezi kukueleza tarehe ya harambee hiyo kwa kuwa muda wa kufanya hivyo bado na ukifika tutakuiteni waandishi na kukuelezeni," alisema.

Hata hivyo, Kastiko alifafanua kwamba kufanyika kwa harambee hiyo ni agizo la makao makuu ya chama.

"Isitoshe mikoa yote inatakiwa kufanya harambee ya kuchangia fedha kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 25," aliongeza.

Kwa mujibu wa habari tulizonazo ni harambee hiyo ilipangwa kufanyika kwa siri.

Maranda, Farijala Hussein na wafanyakazi watatu wa Benki Kuu (BoT), Imani Mwakosya, Ester Komu na Bosco Kimela, wamefunguliwa mashtaka ya kula njama na kuiibia benki hiyo zaidi ya Sh207 milioni baada ya kudanganya kuwa kampuni yao ya Russias T Ltd ilipewa deni na kampuni ya General Marketing ya India. Washtakiwa hao wako nje kwa dhamana.
 
Hotel inaitwa Kilimanjaro Hotel Kempinski na si Kempisky.

Kama mwandishi wa habari hawezi ku-invest muda na dakika moja kutafuta herufi sahihi za hotel ambayo inajulikana sana basi ananitia shaka na uchunguzi wa habari zake kwa ujumla, Hawa ndiyo waandishi habari wetu wa Tanzania kazi bado tunayo.

MJ
 
hii habari ni wazi kabisa sijui kwa nini kuna ubishi. hakuna wa kugusa wezi wa epa, waliba kufanikisha kampeni za kikwete na sasa anakutana nao kufanya mkakati mwingine kama huo
 
Jamani mimi nauliza hivi...
KISHERIA Mtuhumiwa huwa anapoteza haki/fursa ya kushiri katika shughuli yeyote ile iwe ya kijamii au hata ya kisiasa?
Au tu kutokana na UTUHUMIWA wake husababisha muonekano HASI mbele ya jamii?
nauliza tu......
 
Hotel inaitwa Kilimanjaro Hotel Kempinski na si Kempisky.

Kama mwandishi wa habari hawezi ku-invest muda na dakika moja kutafuta herufi sahihi za hotel ambayo inajulikana sana basi ananitia shaka na uchunguzi wa habari zake kwa ujumla, Hawa ndiyo waandishi habari wetu wa Tanzania kazi bado tunayo.

MJ
Hilo lisikupe taabu sana mkuu. Pitia vyombo vyetu vyote vya habari (hata TV) mara kwa mara, ikija kwenye suala la usahihi wa herufi hasa za majina utachoka. Hii haina maana habari yenyewe ni wasiwasi; ni kiwango tu cha elimu ya lugha (zote) tulichonacho siku hizi.
icon10.gif
 
Kwani harambee za JK 2005 ziliendeshwa na kina nani?

Si hawa hawa mafisadi wa EPA , walikuwa wakitajwa mara Lukaza kachanga milioni 200.
Mara Jeetu kachanga milioni 300.
Mara Lema kachanga 120 milioni.

Wameanza tena sasa kujipanga , JK bila EPA hawezi kuiona ikulu.
 
Jamani mimi nauliza hivi...
KISHERIA Mtuhumiwa huwa anapoteza haki/fursa ya kushiri katika shughuli yeyote ile iwe ya kijamii au hata ya kisiasa?
Au tu kutokana na UTUHUMIWA wake husababisha muonekano HASI mbele ya jamii?
nauliza tu......

Kisheria hakuna kinachomzuia lakini katika ulimwengu uliostaarabika na wenye jamii makini, haiyumkiniki mtu mwenye kiwingu cha wizi juu yake kufanya shughuli ya aina hiyo. Kama vile ambavyo huwezi kumkabidhi mwenye tuhuma za ubakaji binti yako amsindikize shule. Ndio maana huo mshikemshike unaouona ndani ya CCM kwa kiasi kikubwa unatokana na kuwa na watuhumiwa wakuu wa ufisadi ndani ya CC na NEC yake. Imani ya wananchi makini itatoka wapi hapo.
icon10.gif
 
CCM ni sikio la kufa ......... Hiki chama full kuoza hata mkiseme au kukiosha namna gani uvundo hautoki. Dawa ni kukiondoa tu,kibaki historia vitabuni basi,
 
hehehe
na muungwana atatokea bila shaka kuchangia harambeee
only in Tanzania
 
hili swala la harambee za kuchangia gharama za kampeni za CCM ni mwendelezo tu wa wizi na ufisadi mkubwa tanzania
 
Back
Top Bottom