babykailama
JF-Expert Member
- Mar 5, 2012
- 251
- 243
Naam vipo, vitu vinne duniani vilivyo vidogo, lakini vina akili nyingi sana:
CHADEMA kama Mchwa ni viumbe wenye nguvu ndogo maana hawana jeshi, hata hivyo huweza kujenga hoja ambazo sisi CCM tunaziona ndogo na za kawaida zikawa kubwa kutoka vishimo hadi vichuguu vikubwa kila mtu akaviona na kushtuka.
CHADEMA ni viumbe vyenye uwezo mdogo maana hawaongozi Serikali yenye chombo cha habari kama TBC, wala hawakusanyi kodi za wananchi tena ni wachache sana Bungeni hata hivyo huwasimamisha wale wachache wenye uwezo mzuri na walio mahiri katika chaguzi na wakiwa bungeni hujenga kambi yao ya upinzani mahala pagumu mjengoni kama walivyo Pelele wawezao kujitengenezea nyumba zao kwenye miamba.
CHADEMA hawana Rais lakini kama Nzige wasio na Mfalme, pamoja na malumbano ya hapa na pale, hujitahidi kwenda pamoja vikosi vikosi, wakisaidiana kutatua matatizo yao ki-Chama na kujengana kuliko sisi CCM ambao tunazidi kugawanyika na kusambaratishana wenyewe kwa sababu za maslahi binafsi na muendelezo wa makundi ya wenye-magamba, wasio-magamba na walio katikati ya hao .
CHADEMA kama Mijusi wanaweza kushikwa kwa mkono na kupelekwa polisi, lumande na hata kuhukumiwa chap-chap hata hivyo huonekana katika majumba ya kifalme na kupenyeza katika vyombo vya Usalama, Wizarani na Wavuti-zamivu (deep-web) wakapata siri kupitia top clandestine and reconnaissance gears mithili ya zile za uzao wa Juliana Paul Assange toka kwa watu waliokula viapo kutozitoa, wakaanika mwaaa! ukweli au kile kiitwacho classified information.
Naam, yuko mtu mmoja anasisimua na atavuta lukuki katika mwendo wake, naye ni Tundu Lissu. Kama simba, mwenye nguvu na kwa madaha miongoni mwa wanyama wengine wa kawaida sana kama mtu wetu Mh. Gosbert Begumisa Blandes au Mh. Murtaza Magungu ambao wakati, jasiri Mh. Lissu anakiita kinyesi jina lake halisi mavi, wao wangependa ayalembe na kupoteza maana kwa lugha ndefu isiyo na tija kuwa ni chakula adhimu kipitacho utumbo mwembamba na kutokea tundu linalomalizikia na silabi -ndu.
Hili ndilo balaa linalotujongelea sisi wana CCM, ambapo Wananchi wanatuona tuna mzaha na hatuna juhudi za dhati toka moyoni kupambana na harufu mbaya ya rushwa, ukiukwaji wa taratibu za nchi tulizokubaliana, mgawanyo usio matiki wa keki ya Taifa Bungeni na uzembe makazini!
Mwenye masikio ya kusikia na asikie neno hili ambalo Babykailama:A S-baby: anawaambia wanaCCM wenzake na wote wapenda maendeleo.
Naibu Spika, Mh. Ndugai, uvaapo vazi lenye nakshi na kukaa mahala pa juu palipoinuka katika kiti cha madini ukilindwa kikatiba na ishara ya Siwa inayoashiria mamlaka, huna haja wala si kazi yako kutolea maelezo wala ku- dilute tuhuma zilizoletwa na Mbunge, wacha Wahusika (aliyetoa tuhuma au majibu ya aliyetuhumiwa) yaletwe panapostahili ukweli ujulikane. Kazi yako ni kutoa miongozo, maagizo, kuongoza majadiliano na kutangaza matokeo au adhabu husika. Jifungie maktaba na utembelee Kanuni za Kudumu za Bunge (LETU SIO LAKO), sehemu ya 5 Ibara ya 63, kama kuna mtu kasema uongo na si vinginevyo. Naam, moja au yote ni dhahiri kati ya haya mawili yafuatayo:
Ama baadhi ya WanaCCM ndani ya Serikali wamechoka na hali ya kutojirekebisha kwa watu tuliowapa dhamana na hivyo kuamua kwa makusudi kutoa taarifa hizo kwa Wapinzani au ni kwamba WanaChadema wametuzidi akili na ujuzi wa kutumia nafasi walizo nazo kuimba korasi za nyimbo wanazopenda Wananchi kwa kujenga hoja (ikibidi kuzikuza kwa ufundi) hadi sisi tunabaki kuonekana hafifu!
Vyovyote ilivyo, sauti ya mwanadamu inanyamaa sasa kwa kuwakumbusha kuwa shoka limekwisha wekwa tayari kila mti usiozaa matunda mema utakatwa na kutupwa motoni 2015! :A S cry: